Hivi hii kitu mmeshwai kupata experience nacho

Hivi hii kitu mmeshwai kupata experience nacho

Una amua kutoka na mtoto matembezi ya kwaida una kutana na wafanya biashara hawa labda anauza vidoli vya kuchezea watoto huna ratiba na kununua iko yeye ana enda mpa mtoto achezee kumuonjesha mtoto una mkataza ataki ana anza kukupigia kelele za kilio kitu cha 2000 mtu ana kuambia 5000 kwasababu tu mtoto kalilia sasa mm nime chukua hatua ya kumpa iyo 2000 na kusepa chap hii kitu ina kela au ni mimi tu
Unamlaumu chinga ambaye hahusiki na malezi ya mwanao. Hivi wazazi wa kisasa mwanao anapata wapi ujasiri wa kulilia kitu toka kwa strangers? Wa kwangu hata mgeni tu akifika nyumbani kwangu anaheshimika na hawezi kusumbuliwa kwa namna yoyote ile.

Mtoto lazima afundishwe mipaka ya kumiliki, ajue kutofautisha zawadi na mahitaji ya lazima. Mpe mahitaji ya lazima kwa wakati lakini zawadi mpe pale anapofanya jambo zuri ili kumuhamasisha kuwa mzuri kwenye jambo husika (sio mara zote. Mfano mtoto umemtuma akaenda, akirudi unampa pesa ya pipi/chocolate. Unamuharibu kwasababu ataamini hiyo ni haki yake na kila ukimtuma lazima umlipe) au wakati unaoona unafaa kumnunulia zawadi. Mfundishe kwamba hata akiona kitu kizuri asikitake kwa lazima, ni either akuombe au asubirie umnunulie mwenyewe. Na iwapo ataomba na ukamwambia asubirie, sharti atii.

Wa kulaumiwa ni wewe kwa kumdekeza mtoto, na sio chinga ambaye ametumia udhaifu wa mwanao kukuuzia bidhaa. Umetenda kosa kumlipa fedha pungufu bila makubaliano.
 
Niliendaga beach na mtoto,Kuna wauza Maputo/bofu wakawa wanampa mtoto,,,,mtoto akapokea si kiling'ang'ania😁,,,,mie nawatizama tu,,eti mnunulie,,,,,nikamwambia akipasua usinidai.
Beach ya Mto Ruvuma!!! Vijana mna mambo
 
Back
Top Bottom