Hivi haya madai ya waziri Nyalandu dhidi ya Wabongo waishio ughaibuni yamekaaje?

NAIBU Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Lazaro Nyalandu, amesema sehemu kubwa ya Watanzania wanaoishi nje ya nchi, wamekua walalamikaji tu kuhusu taratibu za uwekezaji, lakini hawachukui hatua.

"Watanzania waache kulalamika tu kwenye mablog. Wengi wamekuwa walalamikaji tu, lakini hawachukui hatua," alisema Nyalandu.

jibu lake hili hapaKwa upande wake, Ndunguru aliishauri serikali iangalie na kuzifanyia kazi changamoto mbalimbali za uwekezaji ukiwemo mlolongo mrefu kuhusu mchakato wa uwekezaji.

Alisema mchakato wa uwekezaji n chini ni mrefu, jambo linalowafanya Watanzania wengi walioko nje, wakate tamaa, na kwamba hiyo inachangiwa na tatizo la kutakiwa kutumia muda mrefu katika kumilisha taratibu za uwekezaji.

"Tataratibu zetu bado ni ngumu, maana mtu anatumia muda mrefu na gharama na kubwa, jambo linalowakatisha tamaa Watanzania wengi kuja kuwekeza nyumbani," alisisitiza.
.

baada ya kuwakandia watu wanalalamika tu, na ndunguru nae akalalamika sijui jamaa alijisikiaje
 
Hivi Nyalandu anatumia ID gani hapa jamvini? Najua ni member by his words
 
Nimesoma naye kidato Kimoja Ilboru seconadry, ni kweli alikuwa anapenda sana mademu na njia aliyokuwa anatumia ni UKWATA, na kweli alikwenda Marekani through sponsoship the kwenye Religion Organiazation,then akiwa marekani akawa anacoordinate watu kwenda Summer holiday, Watu wakawa wanazamia ikafutwa hiyo Programme
 
Hivi huyu jamaa soo lake la kumbaka msichana wa ki Namibia kule Waldorf College liliishaje?

Hata Arusha alikacha demu ambae ni mtoto wa mchungaji anafanya ZAIN. Jamaa hamna kitu ni limbukeni tu mpenda mamis utafafikiri Masha. Aikuwa na usongo wa uwaziri siku nyingi sana kwahiyo anakuja na speed ili amfunike Chami.
 
Nasikia huyu jamaa aliishi Marekani kwa Muda Mrefu, Je katika Kipindi cha kuishi kwake Marekani alishawahi kufanya Uwekaji wowote au na yeye alikuwa mlalamikaji kwenye Blog mpaka akaja kuwekeza Kwenye Ubunge?


Umenisaidia kufahamu kuwa anazungumza kupitia uzoefu.

Ame universalize character yake na kusahau kuwa wako wengi wanaochangia maendeleo. Au kwake kuchangia maendeleo mpaka uje uwekeze kwenye ndege na mashamba makubwa na kuchangia kampeni zao???

Nyalandu. kama wewe ulikuwa mpiga soga bila kufanya lolote la maana wakati uko ugaibuni, tunao wengi tunawafahamu wanafanya kweli
 
Hao wabeba box watawekeza kwenye biashara gani? ya kuuza dagaaa!
ET

Hii ni dharau kubwa sana kwa watanzania wenzako wenye moyo na mapenzi na nchi yao... wewe umeshafanya nini cha kufikia kusema haya? Kumbuka kwamba ni haohao ndio wanaolipia ada, kodi na hata huduma za matibabu ndugu zao walio bongo

usisahau kwamba kama anaweza kuja burushi na alfu sana na akawa tajiri, kwanini na walio nje wasiwe na moyo wa kuwekeza kwa namna yoyote? Labda niseme potentials kubwa za walio nje (ukiondoa wachache wenye ubishoo wa kitoto) ni kama vile

  1. wamekua exposed na mambo yaliyo straight
  2. wanaweza kusema bila kuwa intimidated
  3. wanaweza kuwa na exposure na baadhi ya technology ambazo kwetu bado
  4. ni wazalendo na ndio maana wana moyo huo
  5. ni wazawa na si magabachori
Think positively mkuu, pamoja twaweza
 
Hivi nauliza, ndege mbili tena ndogo na zinabeba watu 6 kila moja yaani watu 12 kwa zote, hivi hizi ndege unaweza kusafiria kutoka dar hadi kigoma kwa usalama kweli? Huu sio uwekezaji kwa manufaa ya wazawa ila kaleta vindege kwa ajili ya kubeba watalii, hata kama ndio achievement basi asipigiwe makeke na kumpa sifa kibao kwa kuleta hivyo vindege ambavyo havina tija sana kwa wazawa, chukua mfano wa precision wale ni wa ukweli sio huyu wa Nyarandu na viteksi vyake huu ni ujinga tuwe seriuous na aina ya uwekezaji sio kila anayewekeza kisa mzawa ndio tumsifu na kumnyenyekea, ndege yenyewe km ile ya watu 12 ukitoka nayo mwanza hadi arusha roho iko juu ukifika hoi sembuse hii ya watu sita? Nyarandu uwe serious ndugu yangu utatubore mapema.
 
Hili jamvi si ndio ma-blogu yenyewe anayosema Waziri?

Toka lini hapa umeona mada ya watu wakisema "tufanye hiki, tunafanya hiki, tumefanya kile Tanzania"?

Kazi yetu kuchonga kuhusu ngono na siasa za wanavijiji, wana vijiji wenyewe hata hawa vote, hawapo!

Uongo?
 
Hili jamvi si ndio ma-blogu yenyewe anayosema Waziri?

Toka lini hapa umeona mada ya watu wakisema "tufanye hiki, tunafanya hiki, tumefanya kile Tanzania"?

Kazi yetu kuchonga kuhusu ngono na siasa za wanavijiji, wana vijiji wenyewe hata hawa vote, hawapo!

Uongo?

Sasa kama ni hivyo,kipi kilikuwasha hadi ukajiunga nasi hapa?Kama wewe ndio mpenda kuchonga kuhusu ngono usijaribu ku-generalise ugonjwa wako kwa kila MWANA-JF.

OVYOO!!!
 
"Zamani biashara hii ilitawaliwa na Wahindi na Waarabu ambao walitujengea hisia na dhana kwamba huduma hiyo ni ya gharama kubwa sana na kwa hiyo ni ya watu maalumu tu. Hii si kweli, hata Mtanzania wa kawaida anaweza kumudu gharama za usafiri huu," alisema.

Huyu ana laana sijui ya nani??!!! Hivi kweli watanzania wa kawaida tokalini tukaweza kumudu gharama za usafiri wa ndege???!! Kwa maisha gani bora kwa kila mtanzania waliyotuletea????!!! Imbecile!!!

...ha ha!

Unajua, 'aliyevimbiwa' ni ngumu sana kumuelewa mwenye njaa;...

CCM candidate to use chopper in remaining campaign days Tuesday, 26 October 2010 10:27 digg

By Michael Matemanga,
Citizen Correspobndent

Singida. The Singida North parliamentary candidate on Chama Cha Mapinduzi (CCM) ticket, Mr Lazaro Nyalandu is planning to use helicopter during the last two days of campaigns.

Apart from CCM and Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) presidential candidates, Mr Jakaya Kikwete and Dr Willibrod Slaa respectively, no other candidate has used helicopters for campaigning.

Mr Nyalandu said he has decided to hire the chopper so as to be able to go through all the wards in the constituency to remind voters to elect him when they go to vote next Sunday.

...and he didn't disappoint them...

IMG_3775.jpg


Mh. Nyalandu na mai waifu wake Faraja Kota
wakiwasili mkutanoni kwa chopa


source; MICHUZI

...madhali hakuna aliyehoji mazingira na gharama za ukodishwaji Helicopter, basi tuendelee kufunika kombe 'mwanaharamu apite.'
 
yanaweza yakawa na ukweli kwa wakati fulani, tunapolalamikia kitu fulani ni lazima tuwe na njia mbadala sio kulalamika tu..
 
Huyu mheshimiwa kama anataka ufumbuzi wa matatizo basi atoe mawasiliano yake ili tumsaidie kumpa mifano halisi ya usumbufu kwenye uwekezaji huko TZ.

Wengine tumesha deal na hao TIC, TRA pamoja na mabank na kweli kuna usumbufu mkubwa sana.

Angetumia huu muda kuyasoma na kuyatafutia ufumbuzi hayo yanayolalamikiwa. Huyo Ndunguru mwenyewe kalalamikia baadhi ya mambo hapo hapo.
 
Watanzania waishio nje ya nchi wana haki ya kulalamika.

Nina mifano hai.

Website za Wizara karibu zote zina information ila tatizo ni mawasiliano.

Ukiandika email kuuliza habari haijibiwi, ukiandika barua ya posta haijibiwi.

Mtu atapata huduma au habari wizarani pale tu atakapoenda mwenyewe na atoe chai kidogo.

Nyalandu Kwanza haijui wizara, aulize kwanza.

Pili awafunde hao maafisa hapo wizarani ili wajibu email za watu walioko nje.

Inabidi mtu apate information kwanza ndipo ajue wapi pa kuanzia au nini cha kufanya.

Sio wizara hiyo tu, hata wizara ya kilimo, ofisi ya waziri mkuu .

Wizara ya Mali asili na Utalii angalau wanajibu
 
Hiyo kauli ina ukweli fulani ndani mwake...

Arudi kwanza marekani akajibu kesi zinazomkabili. Au Miss TZ ndo anampa ushauri mbovu kama Salma kwa JK?
Huyu mtu hazimo kichwani kabisa, fyatu tu. Utakuta upupu wa Masha ndo anayoanzisha tena na kuendeleza
 
Nyalandu amesoma Wardof College kwa miaka sijui miwili. Mama Mkapa amefinance biashara zake nyingi tuu. Na ni mama Anna Mkapa ambae amekwiba bila uruma.

Watanzania walio nje wana support local economy kuliko hata Barric Gold, angalia Remittance kutoka Western Union kwenda Tanzania. Ni zaidi ya pesa ya Tax ambazo mnakusanya kutoka kwenye makampuni ya kifisadi.

Kingine, hebu mwambieni atazame ni blue print ngapi zimeibwa pale TIC na kwenda kuuzwa kwa wahindi na Vodacom? Watanzania wanahujumiwa kuanzia bandarini, wahindi wameshika hatamu.

Yeye Nyarandu akake chini na wabunge wenzie waangalie why Tanzania inakumbana na brain drain.
 
huyo nyalandu na nduguru wasittuletee ubaguzi hapa,haijalishi upo wapi as long as sisi sote ni watanganyika(spendi kutumia tanzania).kama wanataka tukae kimya wajirekebishe.
 
huyo nyalandu na nduguru wasittuletee ubaguzi hapa,haijalishi upo wapi as long as sisi sote ni watanganyika(spendi kutumia tanzania).kama wanataka tukae kimya wajirekebishe.
 
Sasa kama ni hivyo,kipi kilikuwasha hadi ukajiunga nasi hapa?Kama wewe ndio mpenda kuchonga kuhusu ngono usijaribu ku-generalise ugonjwa wako kwa kila MWANA-JF. OVYOO!!!
ukweli wa waziri unakuuma.

mimi siko nje huko, ndo maana nina moral legitimacy ya kujadili mambo humu, we ushakimbia

wana blogu waishio nje ya nchi hawana lolote zaidi ya kujaza ma page ya discussions za matatizo ya Tanzania. Utakosoaje mapungufu yetu wakati we ulishayakimbia?

basi hata kama ni kupiga domo mpigie domo ya maana, wapi, kazi kujadili jinsi ya kuongoza urefu wa sehemu za siri, ndo mada zetu humu kutwa
 
Back
Top Bottom