#HISTORIA #NA #KUMBUKUMBU #YA #VITA #YA #KAGERA:

Vita yaingia awamu ya tatu.

#Sehemu #ya - 14.

Katika toleo lililopita tuliona mji wa Masaka ulivyotekwa na majeshi ya Tanzania.Kazi hiyo ilifanyika usiku wa kuamkia Jumamosi ya Februari 24, 1979 baada ya mji huo kuzingirwa na JWTZ kwa pande tatu.

Brigedi zilizoshiriki ni ile ya 201 na 208. Sehemu ya kwanza kushambuliwa ilikuwa ni kambi ya jeshi ya kikosi cha "Suicide" kilichoachwa peke yake kuulinda mji wa Masaka.
Kutekwa kwa Masaka kulikuwa ni mwisho wa awamu ya pili ya vita. Kilichofuata baada ya hapo ni awamu ya tatu.

Endelea…....

WANAJESHI wa Tanzania walipokuwa wamejipumzisha katika miji ya Masaka na Mbarara waliyoiteka walikuwa pia wakichora mpango wa awamu ya tatu ya vita.

Lakini Rais Julius Kambarage Nyerere,kwa kuhofia lawama za kimataifa alitaka jeshi la Tanzania lisijipeleke mbele sana bali liwaache waasi wa Serikali ya Idd Amin wafanye hivyo halafu JWTZ lije nyuma yao.

Hapo ndipo walipokuja kuingizwa akinaTito Okello na Yoweri Kaguta Museveni Rais wa sasa wa Uganda, ambaye alipewa eneo la Mbarara ambako angewafundisha wapiganaji wake na Paulo Muwanga akapelekwa Masaka.

Ingawa Muwanga ni wa kabila la Baganda kama wakazi wa Masaka,alionekana zaidi kuwa ni mtu wa Dk. Milton Obote.Baada ya muda mfupi Museveni alifanikiwa kupata wapiganaji kiasi cha 2,000 kutoka Mbarara.

Wakati haya yakifanyika,JWTZ nalo lilikuwa linajipanga upya kutokana na hali ilivyokwenda,ingawa tayari walikwishateka miji ya Masaka na Mbarara,Iddi Amin bado alikuwa madarakani na alikuwa mjini Kampala.JWTZ ikaanza safari ya kwenda Kampala aliko Amin.

Brigedi mbili za Minziro na ya 206 zikaungana kuunda kikosi kazi. Wakati huu ndipo Silas Mayunga alipopandishwa cheo kutoka Brigedia na kuwa Meja jenerali,kisha akakabidhiwa kikosi kazi hicho.

Brigedia Roland Makunda, ambaye alikuwa mkuu wa jeshi dogo la maji alikabidhiwa kusimamia Brigedi ya 206,na Brigedia Ahmed Kitete akakabidhiwa Brigedi ya Minziro.

Baadaye kikosi kazi kikagundua kuwa Kikosi cha Simba ambacho walikishambulia hawakukiteketeza chote.

Baada ya kuukimbia mji wa Mbarara kikosi hicho pamoja na kingine kutoka Kambi ya "Mountains of the Moon" walikuwa wamekimbilia Kaskazini mwa mji huo kujiimarisha.

Walishtukiwa baada ya kuanza kuwarushia mabomu wanajeshi wa Tanzania.Lakini JWTZ ilipojibu mapigo, walitoweka.

Jumatatu ya Machi 19, 1979 Redio Uganda iliripoti kuwa Idd Amin aliwatembelea wanajeshi wake walioko mstari wa mbele eneo la Mbarara, na kujadiliana mambo mengi na makamanda wa vikosi vya Simba na Chui (Tiger) na kwamba walipanga mikakati mipya ya kuwang’oa kabisa maadui kutoka ardhi ya Uganda.

Lakini baadaye ilibainika kwamba redio hiyo ilitangaza uongo,na jambo hilo halikutokea.
Lakini angalau hicho kikosi cha Simba kiliendelea kupigana huku kikikimbia.

Divisheni ya 20 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania, ambayo ilikuwa inaelekea Uganda, ikakumbana na tatizo jingine la miundombinu wakati kinakaribia eneo la Lukaya,kiasi cha kilomita 40 Kaskazini mwa mji wa Masaka.

Barabara yenye umbali wa kiasi cha kilomita 20 ilikuwa imeharibika vibaya,kutokana na mvua iliyonyesha barabara hiyo ilijaa madimbwi makubwa ya maji na matope.

Hakuna gari lolote lililoweza kupita barabara hiyo,njia pekee ya kufika huko na kwa kutumia barabara hiyo.

Jijini Dar es Salaam bado Nyerere alikuwa anakuna kichwa.Aiteke Kampala na kumkamata Idi Amin halafu avumilie masuto ya jumuiya ya kimataifa?

Au aepuke masuto hayo lakini arudishe majeshi yake nyuma na amwache Idd Amin akiendelea kutawala Uganda?

Iddi Amin alijua mpango wa Tanzania wa kuiteka Kampala,na ilisemekana kuwa baadhi ya wanamkakati wake wa kivita walimshauri kuwa ili Kampala isitekwe kwa urahisi kama Masaka na Mbarara,basi walipaswa kuharibu maeneo fulani ya barabara eneo fulani Kaskazini mwa Lukaya ili kuvunja mawasiliano ya barabara.

Waliambiana kuwa kwa kufanya hivyo kungeyachelewesha zaidi majeshi ya Tanzania kufika Kampala na hivyo majeshi ya Iddi Amin yangepata muda mzuri zaidi wa kujipanga upya kukabiliana na maadui.

Lakini Idi Amin hakukubaliana na pendekezo hilo,akitoa hoja kwamba ikiwa watavunja madaraja ili Watanzania wasivuke, hatimaye hata yeye mwenyewe hangeweza kuvuka kuwakimbia majeshi ya Tanzania kutoka kwenye ardhi ya Uganda.

Imani ya Idd Amin ya kuwafukuza majeshi ya Tanzania kutoka Uganda ilikuwa kwa kiongozi wa kijeshi wa Libya,Kanali Muammar Gaddafi.
Tangu alipopashwa habari kuwa majeshi ya Tanzania yamevuka mpaka na kuingia Uganda,kila mara alikuwa katika mawasiliano na Gaddafi ambaye aliamini kuwa Uganda ni nchi ya Kiislamu ambayo imevamiwa na jeshi ya nchi ya Kikristo.

Kwa hiyo wakati Amin akikataa wazo la askari wake la kuvunja madaraja nchini kwao kama walivyovunja lile la Mto Kagera,alikuwa tayari amepata ahadi kutoka kwa Gaddafi kwamba alikuwa anamwandalia askari na silaha ambao wangetumwa Uganda kupambana na JWTZ.

Hii ilimpa Amin matumaini mapya,sasa aliamini kuwa hatimaye ushindi ungekuwa upande wake.
Kwa hiyo hakukuwa na sababu yoyote ya kuharibu madaraja mazuri ambayo wangelazimika tena kuyajenga baada ya Tanzania kushindwa vita.

Hadi kufikia wakati huu askari wa Libya walikuwa hawajaonekana vitani Uganda.Walioonekana ni Wapalestina waliokuwa wamevaa skafu za PLO na wengine walibeba vitambulisho.

Jumanne ya Machi 13, 1979, kupitia Redio Uganda, Idd Amin alitangaza hadharani kuhusu ushiriki wa PLO kwamba, “majeshi ya Palestina yanapigana bega kwa bega mstari wa mbele.”
Kitendo cha Idi Amin kutangaza hadharani kiliwafanya PLO kushindwa kukanusha.

Lakini walijaribu kujinasua na walisema mamia ya watu wao waliopo Uganda walikuwa huko kwa ajili tu ya mafunzo ya kijeshi na si zaidi ya hapo.
Lakini hawakuweza kukanusha kama walikuwa wanapigana bega kwa bega na majeshi ya Amin.

Hata hivyo PLO walifadhaika kiasi kwamba waliamua kutuma ujumbe wao mjini Dar es Salaam kusisitiza uhusiano mzuri na mwema na Tanzania.

Jumatano ya Machi 21, 1979 ujumbe huo ukaitisha mkutano na waandishi wa habari na kusema, “Hakuna Mpalestina anayepigana bega kwa bega na majeshi ya Idi Amin.”

Lakini hilo halikuondoa ukweli kwamba ushiriki wa PLO katika jeshi la Amin ulikuwa mkubwa,pamoja na ukweli huo,Rais Nyerere hakuvunja uhusiano kati ya Tanzania na PLO.

Ni wakati gani askari wa Libya walliingia uwanja wa mapambano!?

Endelea na sehemu 15.........
 
#HISTORIA #NA #KUMBUKUMBU #YA #VITA #YA #KAGERA

Mji wa Lukaya,eneo la maafa kwa JWTZ.

#Sehemu #ya - 15.

Toleo lililopita tuliona jinsi waasi wa Palestina wa PLO walivyoshiriki katika vita ya Uganda dhidi ya Tanzania.Ingawa PLO ilituma ujumbe wake Dar es Salaam kusisitiza kuwa haikuwa kweli,Mwalimu Nyerere hakutoa kauli yoyote.

Hata hivyo,baadaye kiongozi wa kijeshi wa Libya naye alituma jeshi lake kuingia vitani upande wa Iddi Amin.Walifanikiwa kuukomboa mji wa Lukaya kwa saa chache tu lakini baadaye JWTZ ikaurejesha na kuwatawanya askari wa Libya.

Sasa endelea….......

MPANGO wa kuingia Lukaya ulizishirikisha brigedi tatu ambazo ni 201, 207 na 208. Brigedi ya 201 iliyoongozwa na Brigedia Imran Kombe ilikuwa imejaa wanamgambo ambao wengi wao walikuwa hawajawahi kukabiliana na mapambano ya silaha za moto.
Kile kikosi cha Waganda waliompinga Amin kilichoongozwa na David Ojok kiliingizwa pia katika brigedi hii.

Alfajiri Jumamosi ya Machi 10, 1979 vikosi vya Tanzania viliushambulia mji wa Lukaya kwa makombora na kuuchakaza,kisha wakasubiri kupambazuke.

Lakini bila kutambua,kikosi kikubwa cha jeshi la Libya na askari wa Iddi Amin walikuwa wamekusanyika upande wa Kaskazini wa Kinamasi na walikuwa wamepewa amri na Iddi Amin mwenyewe kuurejesha mji wa Masaka mikononi mwa Uganda ndani ya saa tatu au chini ya hapo.

Askari wa Libya walikuwa wameingia Uganda jana yake,wakiwa na ndege kadhaa ambazo pia zilibeba silaha ndogo na kubwa kama vifaru na mizinga, zilijaza mafuta Nairobi, Kenya kabla ya kuingia Uganda.

Ndani ya ndege hizo yalikuwamo pia magari ya kijeshi kama Land Rover. Lakini silaha iliyotisha zaidi ni “Katushka” ambayo ilitumika kufyatua makombora makubwa.

Silaha hiyo ilitengenezwa Korea Kaskazini na haikuwa imetumiwa vitani kabla ya hapo.Jeshi hilo lilikuwa na maelfu ya askari wa Libya na waasi wachache wa PLO,ilisemekana kuwa ni kikosi kikali katika vita.

Jeshi la Amin na Gaddafi liliingia kazini saa za magharibi wakati giza lilipoanza kutanda. Walipoona brigedi ya Imran Kombe,askari wa Libya wakaanza kufyatua roketi za Katushka.

Ingawa roketi hizo hazikuwapiga wanajeshi wa Tanzania,milio mikubwa iliyotokana nazo na miale mikali na mwanga uliotokana nazo zilivyopita juu ya vichwa vya wapiganaji wa Tanzania ilitosha kabisa kuwatia kiwewe wapiganaji wa brigedi ya Kombe ambao wengi hawakuwahi kukutana na mapigano ya risasi,achilia mbali makombora makali kama Katushka.

Baadhi ya wapiganaji katika brigedi hiyo walikimbia, hata waliobaki walijikuta hawawezi kufanya chochote.

Hata hivyo hakuna hata mmoja aliyeuawa,lakini Amin sasa akawa ameurejesha na kuukalia mji wa Lukaya.

Kama askari wa Amin na wale wa Libya wangeendelea na mashambulizi makali zaidi, wangeweza kuyasogeza majeshi ya Tanzania na hata kuutwaa mji wa Masaka kwa sababu kwa wakati huo kilichokuwako katikati ya mji wa Lukaya na Masaka ni vifaru vitatu tu vya Tanzania ambavyo visingeweza kupambana na Katushka ya Libya.

Lakini kwa kuzubaishwa na kile walichoona kuwa ni ushindi wa kuurejesha mji wa Lukaya,wao waliamua kupumzika Lukaya.

Mara moja amri ikatolewa kwa vikosi vyote vya Tanzania kubadili mbinu za kivita ili kuichukua tena Lukaya kabla hali haijawa hatari zaidi.

Brigedi ya 208, ambayo sasa ilikuwa umbali wa kilomita 60 Kaskazini-Magharibi mwa Lukaya,ilipewa amri ya kugeuka na kurudi kuelekea Lukaya kwa kasi yoyote iliyowezekana na kuvunja mawasiliano ya barabara kati ya majeshi ya Amin na mji wa Kampala.

Vifaru vya Tanzania viliamriwa kusonga mbele na kuanza kushambulia vikali zaidi.
Wakati madereva wa vifaru hivyo walipoanza kuonesha hali ya kusita kwenda kushambulia bila kuwa na askari wa kikosi cha miguu, Jenerali Msuguri alimtuma ofisa mwandamizi wa JWTZ kwenda uwanja wa vita kuhakikisha kuwa amri yake inatekelezwa.

Kikosi cha Amin kikisaidiwa na Libya kilikuwa na silaha kali na kingeweza kushinda katika mchezo lakini hakikuwa kimejipanga.

Kwenye njia ya kuelekea Lukaya kulikuwa na Watanzania,askari wa kuikomboa Uganda,majeshi ya Idi Amin pamoja na askari wa Libya.

Watu walikuwa wakipishana,lakini kwa kuwa usiku huo mwanga pekee uliokuwapo ni mbalamwezi,ilikuwa ni vigumu kutambuana.

Kama vile ni aina fulani ya kituko,kikundi cha Kikosi maalumu cha kuikomboa Uganda kilichokuwa kinaongozwa na David Ojok nacho kilipita barabara hiyo kama walivyopita askari wa Amin na wale wa Tanzania na wale wa Libya.

Kwa wakati mmoja wote hawa walipita barabara hiyo bila kutambuana.
Askari wa Ojok,wakati wakiwa katika barabara hiyo,waliweza kuwasikia watu wakizungumza kiswahili na kuwachukulia kuwa hao walikuwa marafiki.

Ghafla mmoja miongoni mwao akazungumza Kiluo lugha ambayo haitumiki Tanzania.

Alisikika akisema “Subiri kupambazuke na tutawaponda hawa Waacholi wajinga.”

Kusikia hivyo,Ojok akaamuru wapiganaji wake washambulie.Kwa sababu ya kiza na mwanga hafifu wa mbalamwezi hawakuwa na hakika kama walilenga shabaha zao.

Katika mapigano ya usiku huo mmoja,Watanzania wanane na askari mmoja wa Ojok walipoteza maisha.

Wakati hayo yakiendelea, Brigedi ya 208 ilikuwa ikisonga mbele kwa kasi kuelekea Lukaya. Kulipokaribia kupambazuka ilianza kushambulia na kuwarudisha tena nyuma askari wa Amin na wale wa Libya.

Mizinga mikubwa ya Tanzania ikaanza kuwasambaratisha Walibya. Wanajeshi wa Iddi Amin waliogopa sana kiasi kwamba hawakuthubutu hata kufyatua risasi.

Kwa jinsi askari wa Libya walivyochanganyikiwa, walilazimika kukimbia.
Mashambulizi yalipokoma baadaye,askari wa Tanzania walihesabu maiti wakakuta karibu askari 500 wa adui wameuawa katika tukio hilo moja.

Miongoni mwa hao waliouawa,zaidi ya 200 walikuwa ni askari wa Libya.
Ni askari mmoja tu wa Libya ambaye hakuuawa,alikamatwa na kuchukuliwa mateka.

Pamoja na ushindi huo, makamanda wa JWTZ waliichukulia Lukaya kuwa ni sehemu ya maafa kwa Watanzania.
Kama isingekuwa ni ama uzembe au kutokujimudu kwa jeshi la adui,kwa hakika jeshi la Tanzania lingeondolewa kabisa katika ardhi ya Uganda.

Lakini wakati ikikabiliana na matatizo ya Lukaya, jeshi la Tanzania pia lilikuwa linakabiliwa na hali ngumu katika eneo la Sembabule ambalo lilikuwa kiasi cha kilomita 60 Kaskazini-Magharibi mwa mji wa Masaka.

Nini kilikuwa kinaendelea huko Sembabule?
Endelea kufuatilia makala hizi ili uzidi kuhabarishwa juu ya vita hii iliyopiganwa na majirani hawa wawili wa Jumuia ya Afrika Mashariki.

Itandelea kesho........
 
#HISTORIA #NA #KUMBUKUMBU #YA #VITA #YA #KAGERA

Mji wa Lukaya,eneo la maafa kwa JWTZ.

#Sehemu #ya - 15.

Toleo lililopita tuliona jinsi waasi wa Palestina wa PLO walivyoshiriki katika vita ya Uganda dhidi ya Tanzania.Ingawa PLO ilituma ujumbe wake Dar es Salaam kusisitiza kuwa haikuwa kweli,Mwalimu Nyerere hakutoa kauli yoyote.

Hata hivyo,baadaye kiongozi wa kijeshi wa Libya naye alituma jeshi lake kuingia vitani upande wa Iddi Amin.Walifanikiwa kuukomboa mji wa Lukaya kwa saa chache tu lakini baadaye JWTZ ikaurejesha na kuwatawanya askari wa Libya.

Sasa endelea….......

MPANGO wa kuingia Lukaya ulizishirikisha brigedi tatu ambazo ni 201, 207 na 208. Brigedi ya 201 iliyoongozwa na Brigedia Imran Kombe ilikuwa imejaa wanamgambo ambao wengi wao walikuwa hawajawahi kukabiliana na mapambano ya silaha za moto.
Kile kikosi cha Waganda waliompinga Amin kilichoongozwa na David Ojok kiliingizwa pia katika brigedi hii.

Alfajiri Jumamosi ya Machi 10, 1979 vikosi vya Tanzania viliushambulia mji wa Lukaya kwa makombora na kuuchakaza,kisha wakasubiri kupambazuke.

Lakini bila kutambua,kikosi kikubwa cha jeshi la Libya na askari wa Iddi Amin walikuwa wamekusanyika upande wa Kaskazini wa Kinamasi na walikuwa wamepewa amri na Iddi Amin mwenyewe kuurejesha mji wa Masaka mikononi mwa Uganda ndani ya saa tatu au chini ya hapo.

Askari wa Libya walikuwa wameingia Uganda jana yake,wakiwa na ndege kadhaa ambazo pia zilibeba silaha ndogo na kubwa kama vifaru na mizinga, zilijaza mafuta Nairobi, Kenya kabla ya kuingia Uganda.

Ndani ya ndege hizo yalikuwamo pia magari ya kijeshi kama Land Rover. Lakini silaha iliyotisha zaidi ni “Katushka” ambayo ilitumika kufyatua makombora makubwa.

Silaha hiyo ilitengenezwa Korea Kaskazini na haikuwa imetumiwa vitani kabla ya hapo.Jeshi hilo lilikuwa na maelfu ya askari wa Libya na waasi wachache wa PLO,ilisemekana kuwa ni kikosi kikali katika vita.

Jeshi la Amin na Gaddafi liliingia kazini saa za magharibi wakati giza lilipoanza kutanda. Walipoona brigedi ya Imran Kombe,askari wa Libya wakaanza kufyatua roketi za Katushka.

Ingawa roketi hizo hazikuwapiga wanajeshi wa Tanzania,milio mikubwa iliyotokana nazo na miale mikali na mwanga uliotokana nazo zilivyopita juu ya vichwa vya wapiganaji wa Tanzania ilitosha kabisa kuwatia kiwewe wapiganaji wa brigedi ya Kombe ambao wengi hawakuwahi kukutana na mapigano ya risasi,achilia mbali makombora makali kama Katushka.

Baadhi ya wapiganaji katika brigedi hiyo walikimbia, hata waliobaki walijikuta hawawezi kufanya chochote.

Hata hivyo hakuna hata mmoja aliyeuawa,lakini Amin sasa akawa ameurejesha na kuukalia mji wa Lukaya.

Kama askari wa Amin na wale wa Libya wangeendelea na mashambulizi makali zaidi, wangeweza kuyasogeza majeshi ya Tanzania na hata kuutwaa mji wa Masaka kwa sababu kwa wakati huo kilichokuwako katikati ya mji wa Lukaya na Masaka ni vifaru vitatu tu vya Tanzania ambavyo visingeweza kupambana na Katushka ya Libya.

Lakini kwa kuzubaishwa na kile walichoona kuwa ni ushindi wa kuurejesha mji wa Lukaya,wao waliamua kupumzika Lukaya.

Mara moja amri ikatolewa kwa vikosi vyote vya Tanzania kubadili mbinu za kivita ili kuichukua tena Lukaya kabla hali haijawa hatari zaidi.

Brigedi ya 208, ambayo sasa ilikuwa umbali wa kilomita 60 Kaskazini-Magharibi mwa Lukaya,ilipewa amri ya kugeuka na kurudi kuelekea Lukaya kwa kasi yoyote iliyowezekana na kuvunja mawasiliano ya barabara kati ya majeshi ya Amin na mji wa Kampala.

Vifaru vya Tanzania viliamriwa kusonga mbele na kuanza kushambulia vikali zaidi.
Wakati madereva wa vifaru hivyo walipoanza kuonesha hali ya kusita kwenda kushambulia bila kuwa na askari wa kikosi cha miguu, Jenerali Msuguri alimtuma ofisa mwandamizi wa JWTZ kwenda uwanja wa vita kuhakikisha kuwa amri yake inatekelezwa.

Kikosi cha Amin kikisaidiwa na Libya kilikuwa na silaha kali na kingeweza kushinda katika mchezo lakini hakikuwa kimejipanga.

Kwenye njia ya kuelekea Lukaya kulikuwa na Watanzania,askari wa kuikomboa Uganda,majeshi ya Idi Amin pamoja na askari wa Libya.

Watu walikuwa wakipishana,lakini kwa kuwa usiku huo mwanga pekee uliokuwapo ni mbalamwezi,ilikuwa ni vigumu kutambuana.

Kama vile ni aina fulani ya kituko,kikundi cha Kikosi maalumu cha kuikomboa Uganda kilichokuwa kinaongozwa na David Ojok nacho kilipita barabara hiyo kama walivyopita askari wa Amin na wale wa Tanzania na wale wa Libya.

Kwa wakati mmoja wote hawa walipita barabara hiyo bila kutambuana.
Askari wa Ojok,wakati wakiwa katika barabara hiyo,waliweza kuwasikia watu wakizungumza kiswahili na kuwachukulia kuwa hao walikuwa marafiki.

Ghafla mmoja miongoni mwao akazungumza Kiluo lugha ambayo haitumiki Tanzania.

Alisikika akisema “Subiri kupambazuke na tutawaponda hawa Waacholi wajinga.”

Kusikia hivyo,Ojok akaamuru wapiganaji wake washambulie.Kwa sababu ya kiza na mwanga hafifu wa mbalamwezi hawakuwa na hakika kama walilenga shabaha zao.

Katika mapigano ya usiku huo mmoja,Watanzania wanane na askari mmoja wa Ojok walipoteza maisha.

Wakati hayo yakiendelea, Brigedi ya 208 ilikuwa ikisonga mbele kwa kasi kuelekea Lukaya. Kulipokaribia kupambazuka ilianza kushambulia na kuwarudisha tena nyuma askari wa Amin na wale wa Libya.

Mizinga mikubwa ya Tanzania ikaanza kuwasambaratisha Walibya. Wanajeshi wa Iddi Amin waliogopa sana kiasi kwamba hawakuthubutu hata kufyatua risasi.

Kwa jinsi askari wa Libya walivyochanganyikiwa, walilazimika kukimbia.
Mashambulizi yalipokoma baadaye,askari wa Tanzania walihesabu maiti wakakuta karibu askari 500 wa adui wameuawa katika tukio hilo moja.

Miongoni mwa hao waliouawa,zaidi ya 200 walikuwa ni askari wa Libya.
Ni askari mmoja tu wa Libya ambaye hakuuawa,alikamatwa na kuchukuliwa mateka.

Pamoja na ushindi huo, makamanda wa JWTZ waliichukulia Lukaya kuwa ni sehemu ya maafa kwa Watanzania.
Kama isingekuwa ni ama uzembe au kutokujimudu kwa jeshi la adui,kwa hakika jeshi la Tanzania lingeondolewa kabisa katika ardhi ya Uganda.

Lakini wakati ikikabiliana na matatizo ya Lukaya, jeshi la Tanzania pia lilikuwa linakabiliwa na hali ngumu katika eneo la Sembabule ambalo lilikuwa kiasi cha kilomita 60 Kaskazini-Magharibi mwa mji wa Masaka.

Nini kilikuwa kinaendelea huko Sembabule?
Endelea kufuatilia makala hizi ili uzidi kuhabarishwa juu ya vita hii iliyopiganwa na majirani hawa wawili wa Jumuia ya Afrika Mashariki.

Itandelea kesho........
Safi sana tupo pamoja!

Sent from my TECNO-C9 using JamiiForums mobile app
 
😂 😂 😂
Ndio maana bongo wahitimu wa vyuo hawaajiriki kwa kucopy and kupaste hata kazi za masomo, yakitoka hapo, asilimia kubwa ni mazwazwa tu

kama kazi sio ya kwako, lazima umtabue mwadishi na kumtaja, sio unaiba halafu wakaimbiwa unatoa majibu yao ni matusi kwa kwenda mbele

Pia sema kama umeongezea utopolo wako ndani kazi ya mtu mwingine usiokuwa na ukweli wowote. Fiction
 
😂 😂 😂
Ndio maana bongo wahitimu wa vyuo hawaajiriki kwa kucopy and kupaste hata kazi za masomo, yakitoka hapo, asilimia kubwa ni mazwazwa tu

kama kazi sio ya kwako, lazima umtabue mwadishi na kumtaja, sio unaiba halafu wakaimbiwa unatoa majibu yao ni matusi kwa kwenda mbele

Pia sema kama umeongezea utopolo wako ndani kazi ya mtu mwingine usiokuwa na ukweli wowote. Fiction
Hapa watu wanatumia fake Id sasa ww unajuaje kama yeye ndo aliandika makala hii gazeti la Mwananchi? Wkt mwingine si kila kitu kujifanya mnajua au kupinga tu by they hajajipatia pesa kwa kazi ya mtu mwingine hapa unasoma bure unaondoka .
 
😂 😂 😂
Ndio maana bongo wahitimu wa vyuo hawaajiriki kwa kucopy and kupaste hata kazi za masomo, yakitoka hapo, asilimia kubwa ni mazwazwa tu

kama kazi sio ya kwako, lazima umtabue mwadishi na kumtaja, sio unaiba halafu wakaimbiwa unatoa majibu yao ni matusi kwa kwenda mbele

Pia sema kama umeongezea utopolo wako ndani kazi ya mtu mwingine usiokuwa na ukweli wowote. Fiction
Mkuu kinachokuuma nini?
Kwani movie unazotazama unanunua original? una account Netflix?
Software unazotumia kwenye computer unanunua original?

Ndio maisha yetu, movie zenyewe tunarushiana kwenye flash, torrent n.k
Window zenyewe tunatoa kwenye torrent cracked...
haya ndio maisha yetu.....
hatimiliki Africa utasubiri sana.......

Acha tuendelee kupata nondo

Mkuu Matanga shusha vyuma
 
Hivi wadau, kwenye hii vita ya kagera wengi tumeona real recorded videos za mapigano ya vita hasa zilizokua recorded na majeshi yetu imara JWTZ, vipi hakuna recorded videos zilizokua recorded na jeshi la uganda wakati wa mapigano yakiendelea. Natamani sana ningeona pia video hizo
 
Sina muda huo muda wa mipasho
Wewe ni mwizi wa hakimiliki, eti unaita hii ni kazi yako, This is plagiarism

"Plagiarism"
the practice of taking someone else's work or ideas and passing them off as one's own.
Maana:
(Uhalifu wa kuchukua kazi au maoni ya msanii mwingine na kuipitisha kama ya kwako na kukiuka sheria ya hakimiliki).

Katika sheria ya hakimiliki, msanii ametafsiriwa kama mwigizaji, mwandishi, mwimbaji, mwanamuziki, mchezaji (dancer) au mtu anayeigiza, kuchonga au kufanya maonesho jukwaani.
kifungu cha 3(i) cha sheria hii, kazi zinazolindwa na sheria hii ni zile ambazo zimetengenezwa na mtunzi wa Kitanzania au zile ambazo mtunzi wake si Mtanzania lakini ana makazi yake ya kudumu hapa nchini au kazi hiyo iliyotengenezwa kwa mara ya kwanza hapa Tanzania, au kazi ambazo ni za kusikika na kuona (audio-visual) ambazo mtayarishaji wake ni Mtanzania au makao makuu yake yakutengeneza kazi hizo zipo nchini.

Umevunja sheria..................End Off
Muache ahadithie kwani tunashindana kusahihisha thesis hapa!!?
 
Muache ahadithie kwani tunashindana kusahihisha thesis hapa!!?
Sawa..
Lakini kama hajaandika yeye, ni vizuri akasema yeye siyo mwandishi wa hii makala/hadithi
Hii ameitoa kwenye gazeti la Mwananchi, sijaona sehemu yeyeto ananukuu hivyo, hizi ni kazi za watu kama yeye sio mwandishi.....
 
#HISTORIA #NA #KUMBUKUMBU #YA #VITA #YA #KAGERA :

Nyerere aipuuza OAU,aamuru jeshi liingie Uganda.

#Sehemu #ya - 9

Sehemu iliyopita tumeona namna Uganda ilivyovamiwa na makomandoo wa Israel katika kile killichoitwa ‘Operation Entebbe’ au kama ilivyojulikana kwa wengine, ‘Operation Thunderbolt’, Jumapili ya Julai 4, 1976 na ndege zake za kijeshi kuharibiwa vibaya, Urusi iliahidi kuimarisha kikosi cha anga cha jeshi la nchi hiyo na kuwapa ndege nyingine za kivita.

Kwa ahadi hiyo uhusiano kati ya Uganda na Urusi ukaanza kuimarika tena.Marubani wa ndege za jeshi za Uganda walipelekwa mafunzoni Urusi.
Miongoni mwa hao ni Luteni David Omita,Luteni Atiku na Luteni Abusala ambao baadaye walikuja kuwa marubani wa kwanza kuishambulia Tanzania kwa ndege za kivita.

Pamoja na uhusiano huo kati ya Uganda na Urusi, wote hawa Urusi na nchi nyingine za Ulaya Mashariki walisema wako tayari kuendelea kuipa Uganda silaha na zana zingine za kijeshi,lakini sharti lilikuwa ni kulipa kwa fedha taslimu na si kwa mkopo.

Uingereza na Ujerumani Magharibi kwa upande wa Tanzania zilitoa msaada katika vita hiyo kwa njia isiyo ya moja kwa moja kwa kutoa mamilioni ya dola kusaidia wakimbizi wa Kagera.

Kwa hiyo fedha ya Tanzania iliyokuwa itumike kwa wakimbizi hao ikatumika vitani badala yake.Canada ilikuwa ikitoa silaha kwa Tanzania zikiwamo ndege za kivita na kwa mujibu wa vyanzo fulani,hata baadhi ya marubani wa ndege za jeshi walipokea mafunzo yao nchini Canada.

Muda mrefu hata kabla ya vita kuanza,Tanzania ilikuwa imeagiza ndege zake kutoka Canada.
Wakati vita ilipozuka,kwa mujibu wa kitabu cha War in Uganda,Tanzania ilijaribu kuiharakisha Canada itume ndege hizo,lakini Canada haikufanya lolote.Hata hivyo ndege hizo zilifika baada ya vita kumalizika.

Kuhusu upatikanaji wa silaha nchini Uingereza, kitabu hicho kinaandika kuwa Tanzania ilimtegemea sana Amin Kashmiri ambaye wakati vita inaanza alikuwa London Uingereza, akifanya kazi ya uwakala wa ununuzi wa silaha kwa ajili ya Tanzania na nchi nyingine za Afrika.

Kashmiri au kama wengine walivyomuita Sheikh Mohamed Ameenullah Kashmiri,ilikuwa ateuliwe kuwa mkuu wa majeshi katika mabadiliko ya uongozi jeshini ya mwaka 1974, lakini iliaminika kuwa hakupewa wadhifa huo kwa sababu ya asili yake ya India.

Wasifu wake unaonyesha kuwa Luteni Kanali Kashmiri alizaliwa mwaka 1935 mkoani Tabora na kusoma Shule ya Sekondari ya Karimjee ya Tanga (1950-1956) na baadaye chuo cha kijeshi cha Royal Academy Sandhurst nchini Uingereza (1958 - 1960).
Yeye na Mrisho Sarakikya ndio walioshiriki kikamilifu kulisuka upya Jeshi la Tanzania mara baada ya uasi wa Januari 1964.

Hata hivyo, Serikali ya Uingereza haikutaka kujihusisha waziwazi katika mgogoro wa Tanzania na Uganda.Lakini angalau vifaa vya kujenga upya daraja la Mto Kagera vilitolewa na Uingereza.
Kashmiri alifanikisha kupatikana kwa mabuti ya jeshi,mahema na baadhi ya vifaa vingine, na vikapakiwa kuletwa Tanzania.

Kupita kote huko duniani ni katika Afrika tu ndiko ambako Tanzania ilipata marafiki wa kweli.Msumbiji na Zambia walitoa hadharani taarifa za kumlaani Idi Amin kuivamia Tanzania.
Msumbiji ilitoa kikosi cha wapiganaji wake kwenda vitani Kagera,nchi za mstari wa mbele nazo kila moja zikachangia silaha.Algeria nayo ilituma meli tatu za silaha.

Lakini katika yote hayo, walioiokoa Tanzania kwa maana ya zana za kivita ni silaha za Jeshi la Uganda.
Wanajeshi wa Uganda walipokuwa wakiwakimbia wapiganaji wa JWTZ waliacha silaha nyingi nyuma yao ambazo JWTZ ilizikusanya na kuzitumia.

Shida kubwa ya Tanzania ikawa si silaha tena,bali ni namna ya kusafirisha silaha walizopata. JWTZ ilikusanya silaha nyingi sana za jeshi la Idi Amin kiasi kwamba kuliibuka utani kuwa “Idi Amin alikuwa mgavi mkuu wa silaha kwa Tanzania.”

Awamu ya kwanza ya Vita vya Kagera ikawa imemalizika kwa kuyafukuza majeshi ya Idi Amin katika ardhi ya Tanzania.
Lakini Rais wa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere hakuridhika tu na kuwaondoa katika ardhi yake kwa sababu aliamini akiwaacha watashambulia tena.

Baada ya kuwaondoa katika ardhi ya Tanzania kilichofuata ilikuwa ni uamuzi mgumu kuwaandama hadi ndani ya Uganda kwenyewe ili kuhakikisha hawabaki kuja kushambulia tena.
Lakini Nyerere alikuwa kwenye shinikizo kubwa kutoka kwa Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU) wakimtaka asitishe vita dhidi ya Uganda.

Aliyekuwa mwenyekiti wa OAU, Rais Jaafar Nimeiry wa Sudan, alianza kumkaba Rais Nyerere kuhusu vita ya Uganda akimtaka ayaondoe majeshi yake.Nyerere naye alimshutumu Nimeiry na OAU kwa kushindwa kulaani uvamizi wa Amin na kutaka kusitisha mapigano wakati Amin akiwa ameikalia ardhi ya Tanzania.

Nyerere alitangaza hadharani kuwa hafikirii kusitisha vita dhidi ya Uganda hadi awe na uhakika na usalama wa Tanzania.Msimamo huo alianza kuuonyesha siku ile alipotangaza vita,Alhamisi ya Novemba 2, 1978. Katika hotuba yake, Mwalimu Nyerere alisema: “

..Marafiki zetu wanaotuomba maneno ya suluhu waache maneno hayo.Kuchukua nchi ya watu wengine si kwamba majeshi yamekosea njia na kusema kuwa sasa sehemu hiyo umeichukua na kutangaza vita kwa nchi ile nyingine.Si sisi tuliofanya hivyo,amefanya hivyo mwendawazimu.

“Sasa rafiki zetu, kama ni marafiki wa kweli,watataka tumwondoe mtu huyu. Hawawezi kutuomba suluhu au jambo la ajabu kabisa turudishe majeshi yetu nyuma,niyarudishe wapi?”

Nigeria, ambayo huenda bado ilikuwa imekasirishwa na kitendo cha Tanzania kuitambua Biafra iliyojitenga nayo ilionyesha msimamo wake waziwazi dhidi ya Tanzania juu ya Vita vya Kagera.

Biafra ilijitenga na Nigeria Jumanne ya Mei 30 1967. Mwaka uliofuata, Jumamosi ya Aprili 13, 1968, Nyerere akaitambua.
Mkuu wa Jeshi la Nigeria, Luteni Jenerali Theophilus Yakubu Danjuma, akitokea Uganda alikokutana na Idi Amin,aliwasili Dar es Salaam Jumanne ya Novemba 14, 1978 na kukaa hadi Alhamisi ya Novemba 16.

Katika mazungumzo ya mjini Kampala, kwa mujibu wa jarida la Africa Research Bulletin, Idi Amin alimwambia Danjuma kuwa yuko tayari kuyaondoa majeshi yake mpakani iwapo tu OAU itamhakikishia kuwa Tanzania itasimamisha mapigano na “kuichokoza Uganda”.

Danjuma alikuwa na ujumbe kutoka kwa Rais wa Nigeria, Jenerali Olusegun Obasanjo kwenda kwa Mwalimu Nyerere ukimtaka kukubali mazungumzo na kusitisha mapigano.

Itaendele..
Uandishi mbovu sana, nyuma mbele mbele nyuma!
 
Uandishi mbovu sana, nyuma mbele mbele nyuma!
Kaiba kazi ya mtu mwingine halafu kachomeka utopolo wake , useless kabisa 🤣 🤣 🤣 🤣
Vita yenyewe ilikuwa miezi 6, anajaza utumbo na malapulapu utadhania ilichukua mwongo mmoja
 
Kaiba kazi ya mtu mwingine halafu kachomeka utopolo wake , useless kabisa
Vita yenyewe ilikuwa miezi 6, anajaza utumbo na malapulapu utadhania ilichukua mwongo mmoja
Bahati nzuri mm ni miongoni mwa watumiaji wa Jamii forums tangu 2014 huko naijua vizuri Sana Jf siumizwi na watu Kama wewe nasonga mbele,unasema imeandikwa kwenye mwananchi unajua mwananchi wameipata kutoka chanzo gani?? Kuongea humu uko huru kabisa wala sitakutusi una haki yako ya msingi kuandika huku ukiwa umejificha nyuma ya keyboard
Kila raheli but waache wajinga wachache wanaofuatilia hii thread please najua wewe ni much know kuliko wote wanaofuatilia hii snario
 
Bahati nzuri mm ni miongoni mwa watumiaji wa Jamii forums tangu 2014 huko naijua vizuri Sana Jf siumizwi na watu Kama wewe nasonga mbele,unasema imeandikwa kwenye mwananchi unajua mwananchi wameipata kutoka chanzo gani?? Kuongea humu uko huru kabisa wala sitakutusi una haki yako ya msingi kuandika huku ukiwa umejificha nyuma ya keyboard
Kila raheli but waache wajinga wachache wanaofuatilia hii thread please najua wewe ni much know kuliko wote wanaofuatilia hii snario
Kama ungeliweza kunijibu kistaaraabu badala ya matusi tokea mwanzo, tusingefika mbali, ningekupotezea....
Pia kwa jinsi ulivyonijibu sasa hivi na kwa kuangalia uandishi wako, nahitimisha wewe sio mwandishi wa hizi makala za vita vya kagera
 
Nimepiga kambi apa nasubili sehemu inayofata kwa hamu.

Japo kufikia apa nmegundua askari wa JWTZ walokufa vitani ni wachache saaana , lakini mboona kambi ya KABOYA wilaya ya MULEEBA ambapo kumbukumbu ya mashujaa imeifadhiwa kuna makaburi ya askari weeeengi saaaana takrbani mia 4.
Nakufikia apa inaonekana walokufa hawafiki ata 50.
 
Nimepiga kambi apa nasubili sehemu inayofata kwa hamu.

Japo kufikia apa nmegundua askari wa JWTZ walokufa vitani ni wachache saaana , lakini mboona kambi ya KABOYA wilaya ya MULEEBA ambapo kumbukumbu ya mashujaa imeifadhiwa kuna makaburi ya askari weeeengi saaaana takrbani mia 4.
Nakufikia apa inaonekana walokufa hawafiki ata 50.
Wanaficha tu ukweli ila walikufa wengi mnooo!

Sent from my TECNO-C9 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom