Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,807
- 11,969
Contents za Rais
1. Kwa muda wote ambao nimekuwa Serikalini, tangu nikiwa Waziri, nimekuwa nasikia habari ya mradi huu wa LNG huko Lindi. Kuna wakati nikiwa Makamu wa Rais nilijaribu kuona kama naweza kusaidia kulisukuma mbele lakini lilikuwa zito kidogo na lina mambo mengi. Nilipopata nafasi hii ya kuiongoza nchi yetu, nikaazimia kwamba lazima tuutekeleza huu mradi.
2. Huu ni mradi mkubwa na wa kimkakati kwa nchi yetu. Tumekuwa ni miradi ya aina hii kwa miaka ya hivi karibuni, ikiwemo wa SGR na Bwawa la Umeme Rufiji. Mradi wa LNG una umahsusi wake kwamba sio mradi wa matumizi ya pesa bali ni mradi unaotuletea mtaji na mapato. Tutakapoukamilisha utabadilisha taswira ya uchumi wa nchi yetu.
3. Nimefarijika kwamba Wizara imekwishaliweka kwenye miliki ya Serikali eneo la mradi na kwamba kuna mpango pia wa kuanzisha Eneo Maalum la Kiuchumi (Special Economic Zone) kwenye eneo la mradi wa LNG ili kuvutia viwanda na uwekezaji mwingine. Huku ndio kufikiri kuzuri.
4. Serikali imejipanga kutoa kipaumbele maalumu kwa wakandarasi na watoa huduma wa ndani katika mradi huu. Fursa ni nyingi zikiwemo ajira rasmi na zisizo rasmi katika kipindi cha ujenzi na uendeshaji wa mradi. Hivyo basi, niwasihi Watanzania kuanza kufanya maandalizi ili kupata fursa za kushiriki katika Mradi huu.
1. Kwa muda wote ambao nimekuwa Serikalini, tangu nikiwa Waziri, nimekuwa nasikia habari ya mradi huu wa LNG huko Lindi. Kuna wakati nikiwa Makamu wa Rais nilijaribu kuona kama naweza kusaidia kulisukuma mbele lakini lilikuwa zito kidogo na lina mambo mengi. Nilipopata nafasi hii ya kuiongoza nchi yetu, nikaazimia kwamba lazima tuutekeleza huu mradi.
2. Huu ni mradi mkubwa na wa kimkakati kwa nchi yetu. Tumekuwa ni miradi ya aina hii kwa miaka ya hivi karibuni, ikiwemo wa SGR na Bwawa la Umeme Rufiji. Mradi wa LNG una umahsusi wake kwamba sio mradi wa matumizi ya pesa bali ni mradi unaotuletea mtaji na mapato. Tutakapoukamilisha utabadilisha taswira ya uchumi wa nchi yetu.
3. Nimefarijika kwamba Wizara imekwishaliweka kwenye miliki ya Serikali eneo la mradi na kwamba kuna mpango pia wa kuanzisha Eneo Maalum la Kiuchumi (Special Economic Zone) kwenye eneo la mradi wa LNG ili kuvutia viwanda na uwekezaji mwingine. Huku ndio kufikiri kuzuri.
4. Serikali imejipanga kutoa kipaumbele maalumu kwa wakandarasi na watoa huduma wa ndani katika mradi huu. Fursa ni nyingi zikiwemo ajira rasmi na zisizo rasmi katika kipindi cha ujenzi na uendeshaji wa mradi. Hivyo basi, niwasihi Watanzania kuanza kufanya maandalizi ili kupata fursa za kushiriki katika Mradi huu.