JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,309
- 5,464
Nimerekodi video hii jana asubuhi Machi 20, 2024 nilipokuwa napita mitaa ya Kariakoo, hapa ni jirani na kilipo Kituo cha Mwendokasi pale Gerezani, kama unavyoona mwenyewe hali ya barabara si nzuri.
Magari na watu wote kwa pamoja wanapata changamoto ya kupita, mvua ikinyesha hali ndio inakuwa mbaya zaidi, hay maji yametokana na mvua iliyonyesha siku moja iliyopita kabla ya kurekodiwa kwa video hiyo.
Serikali iangalie, Kariakoo ni sehemu ya katikati ya Jiji, kuna watu wengi wakiwemo wafanyabiashara wanaotoka nje wanafika hapo, wanapoona hali kama hii inashusha hadhi ya Jiji.