Jiji la Arusha lisubiri sana kwa Dar Es Salaam

kikaniki

JF-Expert Member
Nov 20, 2014
502
938
Tarehe 4 februari 1993 niliikanyaga Dar Es Salaam kwa mara ya kwanza. Na kilichonipeleka Dar ni masomo ya Sekondari katika shule ya Sekondari Azania. Nilipomaliza masomo yangu ya O-level, nilichaguliwa kuendelea na masomo katika shule ya Sekondari Tambaza. Na kisha Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam.

Kipindi hicho majengo marefu Dsm yalikuwa machache sana. Nadhani jengo refu zaidi lilikuwa ni lile la Kitega Uchumi cha Bima (Posta), Jengo la NASACO, Faculty of Social Science, Hall 2 na Hall 5 yote ya UDSM, Jengo zilipo studio za Channel Ten (zamani lilikuwa linaitwa ghorofa la CTN na baadae Ghorofa la Ushirika.

Kipindi kile usafiri ulikuwa ni mabasi ya UDA (Kwa sehemu kubwa) na Chai maharage (KIA) kwa routes ndefu kama ya Kariakoo Chanika au Kisarawe.

Nilikuwa na ndugu yangu anaishi Pugu Kajiungeni. Asilimia kubwa kuanzia Mwisho wa Lami hadi Pugu Kajiungeni yalikuwa ni mapori tu. Enzi hizo ukiwa Kipawa, ghorofa la CTN unaliona. Kwa sasa jiji la Dar limebadilika mno. Zuri na uzuri wake ni wa kuvutia.

Kwa sasa nimehamia Arusha kikazi. Nina miaka zaidi ya minne sasa.

HOJA YANGU NI IPI?
Hoja yangu ni hii hapa..Kwa tathmini yangu, Arusha inabidi ijengwe kwa zaidi ya miaka 20 ili iifikie Dar ya mwaka 1995. Wakati huo Arusha ikijengwa, Dar iwe imesimama hata tofali moja halijengwi.
 
Kwanza aliekuambia arusha inashindana na dar ni nani?

Lazima ujue aina ya life wanayoishi dar si wanayoishi arusha.
Arusha is different ,jamii different so even maendeleo yatakuwa different
 
Upuuzi mtupu kuwaza kushindanisha mikoa kila siku!! Hizi ni akili au matope,???

Alfajiri yote hii unawaza ujinga, badala ya kuwaza namna kuikomboa nchi yako!!? Wewe Dar au Arusha, au Mwanza au Lindi au mkoa mwingine wowote umejenga magorofa mangapi?

Na aliyekuambia Simiyu inashindana na Mwanza, au Mwanza inashindana na Arusha au Arusha inashindana na Dar nani?

Kila mkoa unafanikiwa na kuwa invested kutegemeana na mtu anavyoona wapi atafanikiwa kwa haraka. Kumbuka pia Dar ilikuwa makao makuu ya nchi so hela nyingi za nchi zimekuwa invested hapo!! So hamna cha kushangaza!!
 
Upuuzi mtupu kuwaza kushindanisha mikoa kila siku!! Hizi ni akili au matope,???

Alfajiri yote hii unawaza ujinga, badala ya kuwaza namna kuikomboa nchi yako!!? Wewe Dar au Arusha, au Mwanza au Lindi au mkoa mwingine wowote umejenga magorofa mangapi?

Na aliyekuambia Simiyu inashindana na Mwanza, au Mwanza inashindana na Arusha au Arusha inashindana na Dar nani?

Kila mkoa unafanikiwa na kuwa invested kutegemeana na mtu anavyoona wapi atafanikiwa kwa haraka. Kumbuka pia Dar ilikuwa makao makuu ya nchi so hela nyingi za nchi zimekuwa invested hapo!! So hamna cha kushangaza!!
mkuu jua kutofautisha kati ya alfajiri na asubuhi
 
Wewe ukiangalia thread yake ameandika asubuhi? Mimi ndo nimecomment asubuhi, yeye kaanzisha mada 0358hrs, hii ni asubuhi au alfajari?
huo uzi umeanzishwa saa 12 na dakika 58 asubuhi mkuu au mm simu yangu mbovu
 
Arusha nimekaa zaidi ya miaka kumi sioni jipya, Hakuna jengo refu lolote la maana. Kitu pekee kirefu huku ni misokoto ya bangi...
Hebu tuoneshe huo msokoto mrefu Dada

Bibie usipende kuamini kila unachokisikia kuhusu Arusha na kupokea umbea, hao wahuni wanaoongelewa hawapo kwa jinsi wanavyoongelewa...ni wana swaga hizo tu

Lakini kiuhalisia vijana wa kule ni wapambanaji sanaa, mpaka kupasua kukoto, mawe, kwenda mererani kwa mining, kufuga, kulima n.k
 
Dar ndio Tz ndio nyumbani kwa kila Mtanzania ...Kila mkoa una ladha yake na watu wataendelea kuishi .
 
Tatizo DSM ni kuchafu sana, kunanuka sana majalala, vinyesi kwenye chemba, Shombo za samaki hasa Ferry na Shombo za Ushoga hasa Kinondoni na Temeke

Kingine watu hawana asili ya kupenda kufanya usafi, joto kali sana is also disgusting

DSM ni mahali pazuri pa kuchuma pesa kwasababu kuna Idadi kubwa ya watu na ndivyo tunavyofanya lakini kwa kuishi...Hapafai

Wanaoishi vuzuri kwa Dsm ni wachache sana hasa Wanasiasa na Watumishi wakubwa serikalini pamoja na Wafanyabiashara wakubwa

Wengine ilimradi tu siku ipite
 
Tatizo DSM ni kuchafu sana, kunanuka sana majalala, vinyesi kwenye chemba, Shombo za samaki hasa Ferry na Shombo za Ushoga hasa Kinondoni na Temeke

Kingine watu hawana asili ya kupenda kufanya usafi, joto kali sana ni sababu nyingine

DSM ni mahali pazuri pa kuchuma pesa kwasababu kuna Idadi kubwa ya watu na ndivyo tunavyofanya lakini kwa kuishi...Hapafai

Wanaoishi vuzuri kwa Dsm ni wachache saba hasa Wanasiasa na Watumishi wakubwa serikalini

Wengine ilimradi tu siku ipite
Dsm unaweza kufanya kazi ila ukawa unaishi kama digidigi unatoka mapema kuwahi foleni na unarudi usiku kwa sababu ya foleni ,umetoka alfajir unarudi kwako saa 2 usiku ..


Kuna siku panakuwa na foleni mpaka unapata hasira kama una gari unatamani kuiacha ili upande bodaboda uwahi.
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Hebu tuoneshe huo msokoto mrefu Dada

Bibie usipende kuamini kila unachokisikia kuhusu Arusha na kupokea umbea, hao wahuni wanaoongelewa hawapo kwa jinsi wanavyoongelewa...ni wana swaga hizo tu

Lakini kiuhalisia vijana wa kule ni wapambanaji sanaa, mpaka kupasua kukoto, mawe, kwenda mererani kwa mining, kufuga, kulima n.k
Bibie ww mamaa
 
Tarehe 4 februari 1993 niliikanyaga Dar Es Salaam kwa mara ya kwanza. Na kilichonipeleka Dar ni masomo ya Sekondari katika shule ya Sekondari Azania. Nilipomaliza masomo yangu ya O-level, nilichaguliwa kuendelea na masomo katika shule ya Sekondari Tambaza. Na kisha Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam.

Kipindi hicho majengo marefu Dsm yalikuwa machache sana. Nadhani jengo refu zaidi lilikuwa ni lile la Kitega Uchumi cha Bima (Posta), Jengo la NASACO, Faculty of Social Science, Hall 2 na Hall 5 yote ya UDSM, Jengo zilipo studio za Channel Ten (zamani lilikuwa linaitwa ghorofa la CTN na baadae Ghorofa la Ushirika.

Kipindi kile usafiri ulikuwa ni mabasi ya UDA (Kwa sehemu kubwa) na Chai maharage (KIA) kwa routes ndefu kama ya Kariakoo Chanika au Kisarawe.

Nilikuwa na ndugu yangu anaishi Pugu Kajiungeni. Asilimia kubwa kuanzia Mwisho wa Lami hadi Pugu Kajiungeni yalikuwa ni mapori tu. Enzi hizo ukiwa Kipawa, ghorofa la CTN unaliona. Kwa sasa jiji la Dar limebadilika mno. Zuri na uzuri wake ni wa kuvutia.

Kwa sasa nimehamia Arusha kikazi. Nina miaka zaidi ya minne sasa.

HOJA YANGU NI IPI?
Hoja yangu ni hii hapa..Kwa tathmini yangu, Arusha inabidi ijengwe kwa zaidi ya miaka 20 ili iifikie Dar ya mwaka 1995. Wakati huo Arusha ikijengwa, Dar iwe imesimama hata tofali moja halijengwi.
Kilwa na na Dar es salaam upi ni mji wa zamani au ulioanza kujengwa?je leo kilwa ina hatua gani na Dar ina hatua gani?
 
Back
Top Bottom