The Boss,
Wadamu sisi ni watu wa ajabu sana, tunajua kuna mabaya na wabaya katika jamii zetu. Tunajua kuwa kuna makosa wanadamu tunafanya (regardless ni kwa bahati mbaya ama nzuri), na tunaelewa si wakati wote tunaweza kupata kile tunachokitaka ama kupanga.
Pamoja na kuelewa yote haya, bado huwa tunajisahau na kila mmoja wetu kupenda kujiona yupo special na hawezi kujitazama kwa misingi ya makosa ila kama malaika tu. Tunapenda sana kutafuta wa kumlaumu kila litokeapo lile ambalo hatujalipenda katika maisha yetu. Mfano huo wa mahusiano umetoa ni mfano mzuri sana, mafanikio ama kushindikana kwa mahusiano it takes two. Ni nadra utakuta mtu ata acknowledge mazuri ya ex wake, mara zote tunapenda kujipaka rangi ya kuwa ulikuwa bora kuliko mwenzio na lawama kibao.
Tukijifunza kukubali kuwa wanadamu tuna kasoro na madhaifu (na kwamba na sis ni moja wa wanadamu hao), kutakuwa na hekima na busara kabla ya kulamu.
snowhite, I am humbled. Nashukuru pia Dearest.