Hii ni akili au kukengeuka?

Hii ni akili au kukengeuka?

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
39,905
Reaction score
61,636
Zamani tulikuwa tukijenga nyumba zetu, tutaweka bustani ndogo ndogo za mbogamboga na mtunda, mabanda ya mifugo midogo midogo ili utakapo hitaji chochote iwe ni rahisi kupata hapo ulipo.

Nyakati hizi hatujui ni pepo gani ametuingia, tumehama katika hizo bustani na ufugaji mdogo mdogo, na kukimbilia kwenye uoteshaji wa bustani za maua, ukoka n.k na wakati mwingine kusiliba eneo lote kwa siment au vitofali ili tusioteshe chochote. Huku ukigharamia bili za maji za kunyweshea maua yasiokuwa na faida.

Sasa, hii ni akili au kukengeuka?​
 
Inategemeana na perception ya mtu kimazingira ina faida zake na kulika mboga mboga kuna faida mengi sasa inategemeana na mtu ndani ya ubongo wake anataka kwake paweje ni suala la choice tu
Anayefanya hivyo, mbogamboga anapata wapi?
 
Zamani tulikuwa tukijenga nyumba zetu, tutaweka bustani ndogo ndogo za mbogamboga na mtunda, mabanda ya mifugo midogo midogo ili utakapo hitaji chochote iwe ni rahisi kupata hapo ulipo.

Nyakati hizi hatujui ni pepo gani ametuingia, tumehama katika hizo bustani na ufugaji mdogo mdogo, na kukimbilia kwenye uoteshaji wa bustani za maua, ukoka n.k na wakati mwingine kusiliba eneo lote kwa siment au vitofali ili tusioteshe chochote. Huku ukigharamia bili za maji za kunyweshea maua yasiokuwa na faida.

Sasa, hii ni akili au kukengeuka?​
Ni Uzungu wa ulimbukeni wa KUKENGEUKA.
 
Ukiitafakari kwa kina hii, utagundua ata utu unapotea kwa sababu ya kupenda au kutanguliza hela mbele, kwa sababu hatuwezi kuzalisha ata fungu la mchicha la 500 kwa mazingira tunayoishi.​
Wabongo tunapenda ujinga Ujinga sana ,tunapanda mikoka na kuweka pavement wakati tungeweza kupanda tembele au majani ya maboga tukapa nutrients;
 
Yap upo right ✅ ni choice tu #tunagawana majukumu tu hutaki wauza mboga waokote kwa wapanda maua mkuu
Kutokuwa na hivyo vitu, vitakupelekea kupenda sana hela na utatumia njia yoyote kupata hela, iwe kwa kufitini, uchawa, kuiba, unafiki n.k
 
Skuizi tunatofautisha nyumba na Shamba, Haiwezekani ukae na Ng'ombe nyumbani kwako wakati Tanzania hii bado ardhi ni za kuchukua tu.
Kama aliyeishi mazigira hayo ameweza kufikisha umri wa miaka 90+, hawa wanaoishi kisasa unahisi watafikisha miaka 100+?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom