Hii ni aibu Marine Hassan!

Hii ni aibu Marine Hassan!

Hivi kuna ulazima gani kuongea kingereza kwa vipindi vya mahojiano kama anavyoendesha marine?.kwanza huwa najiuliza wanatumia kingereza kwa manufaa ya nani kwasababu jamii ya watanzania lugha yao ya mawasiliano ni kiswahili ,ili ujumbe ufike kwao asilimia zaidi ya 70 ni lazima kiswahili kitumike.tbc ni kituo ambacho watazamaji wake zaidi ya 90% ni waongeaji wa kiswahili(watanzania ) ,sasa wakiongea/kutangaza kingereza ni kwa faida ama wanamlenga nani hasa?.kingekuwa kituo cha kimataifa ni sawa kutumia kingereza ,ila sio kituo cha kimataifa.
Hii ni moja ya matumizi mabaya ya kodi za wananchi.kituo chetu halafu kisitumie lugha tunayoifahamu.! Aibu kubwa
 
Nilikuwa naangalia kipindi cha Jambo Tanzania, Marine Hassan alikuwa na wageni ambao mmoja wao katokea S Africa. Marine Hassan alikuwa akimuhoji kwa kiingereza ambacho ni aibu tupu!!! Kwa Mfano " Before you to coming here how many countries you are visited?" Pia wakati wa kumuaga, " Ok! Mr Sami you are welcome again there!". Hili ni jambo la aibu kwa mwandishi kama yeye. Ni bora angegoma kumuhoji bila kuwa na mkarimani, kwanza ndo angekipromoti kiswahili. Nawasilisha

Wewe mwenyewe Kiswahili kinakupiga chenga, rekebisha.

Tutaaminisha vipi kama hicho Kiingereza hujakosea kukiandika au umesikia upendavyo? ikiwa Kiswahili ni lugha yako ya Taifa mambo ndio hayo, jee Kiingereza utakuwaje?
 
Mimi naona ana tofauti na Mbowe!
Ukimsikia Mbowe akiongea Kiingereza ni kama Marine tu, wala sio aibu ni kawaida tu
TBC wampe kazi Law Masha, hakuna mbogo anae weza kumfikia. Nashangaa sana watu Nyamagana kumwaga!
 
Mimi toka nizaliwe sijawahi kumsikia Mbowe akiongea kiingereza

Siku akiongea itakuwa balaaa!
Jamaa nafikiri ni std seven au kama kafika form four atakuwa alipata div zero
 
Wapelekeni shule hawa jamani.
Wasiende CHUO kabla ya Primary and secondary school.
zanzibaris4.jpg
huko kuna ukafiri na uongo wa kumkanusha Mungu ! Tunamuogopa Mungu kuliko raha za dunia. Tuko bize na kesho. Soma wewe na wanao muendeleze ufisadi !
 
Nilikuwa naangalia kipindi cha Jambo Tanzania, Marine Hassan alikuwa na wageni ambao mmoja wao katokea S Africa. Marine Hassan alikuwa akimuhoji kwa kiingereza ambacho ni aibu tupu!!! Kwa Mfano " Before you to coming here how many countries you are visited?" Pia wakati wa kumuaga, " Ok! Mr Sami you are welcome again there!". Hili ni jambo la aibu kwa mwandishi kama yeye. Ni bora angegoma kumuhoji bila kuwa na mkarimani, kwanza ndo angekipromoti kiswahili. Nawasilisha

wachina,wahindi, wahabesh,wanakuja na kiingereza cha ajabu sana hapa tz hata siku1 hujawaandika, iweje marine hasan? We utakuwa na m..ndio .. Brayan
 
TBS ni tv ya taifa, na lugha yetu ya Taifa ni Kiswahili; kulikuwa na ulazima gani wa Kilaza Marine kuungaunga maneno ya kiinglishi? Ilitakiwa aandae mkalimani tu, ili mazungumzo yawe na tija kwa jamii nzima ya Watanzania; au walengwa walikuwa Wasauzi? meeeeeeeeeeeee!
 
Na Muislam Safi anaona elimu bora ni ile inayomfanya mtoto aweze kusoma na kuandika KIARABU!
kuisoma na kuielewa Quran, na si Kiarabu, katika Quran kuna History, Geography, Biology nk.
 
TBS ni tv ya taifa, na lugha yetu ya Taifa ni Kiswahili; kulikuwa na ulazima gani wa Kilaza Marine kuungaunga maneno ya kiinglishi? Ilitakiwa aandae mkalimani tu, ili mazungumzo yawe na tija kwa jamii nzima ya Watanzania; au walengwa walikuwa Wasauzi? meeeeeeeeeeeee!
ndio chanel gani hiyo
 
Back
Top Bottom