Hii ndiyo Tanzania tunayoitaka

Jizalendo.
Nani akufanyie utafiti huo? Nenda kafanye mwenyewe halafu u-prove point yako hapa. Jinsi unavyouliza inaonakena unajua kitu ila hutaki kianzie kwako. Watu wengine bwana.....
 
Jizalendo,
Usimbambikizie maneno baba wa taifa. Nyerere never said Kambona si raia ni Mnyasa. Haya yalisemwa na Malecela.
Kama una issue na Mwalimu sema, lakini si kubambikiza maneno asiyoyasema. Na unapowaita wengine wadini jiangalie mwenyewe kwanza kwenye kioo.
 
Mkandara umetoa somo la uhakika utafiri Harub othman anmwaga vitu vya DS darasani pale UDSM!

Kama jizalendo hataelewa basi pumzika mkuu!
 
Mzee Jasusi,

Kambona ndiye aliwafikisha Balozi Lusinde na ndugu yake JM, kisiasa walipo sasa, halafu JM akatoka hapo akaenda kumsema Kambona kuwa sio raia na ni mnyasa, mbona alikubali nafasi za kupewa na Mnyasa? Lini hiyo na wapi bro ninaomba elimu kidogo bro??

Kuhusu hii mada, sina uhakika na nia na madhumuni yake, lakini wananchi wana haki ya kuzungumza, aliyeianzisha hii mada ana haki ya kusema anayotaka, labda tatizo liwe contest ya hoja zake, lakini it does not matter kama ni Mwalimu, Sokoine, Samora, au Dr. Kleruuu, anayeongelewa kusiwe na uyanga na simba hapa, wakiguswa mnaowataka basi mwananchi amefanya makosa, NO!

Viongozi wote wajadiliwe bila jazba, hilo darasa la Mkandara hapo juu halina noma yoyote kwa wale tunaotaka kuelimishwa juu ya Mwalimu, kama kuna anyeona tofauti na mtoa mada, basi ajibu hoja sio ukali na vitisho, Mzee uliyetoa mada hii weka vitu mwanangu tupate elimu!

Kumjadili Mwalimu, aliyetuwekea dubwi na mpaka leo tunagawiwa umeme ni fair game, na pia ni huyo huyo Mwalimu baba wa taifa letu aliyeamua kuwa Jk asubiri baada ya Mkapa kumaliza temu zake, na ikawa kama alivyoamua na sasa wote tunalia tena humu kwenye forum,

sasa eti kuna anyesema kumjadili Mwalimu baba wa taifa letu ni ujinga? Are you kidding me?
 
Wanabodi,
Natoa shukran zangu kwa kupata kunielewa vizuri hapo juu bila hoja nzito. uwanja huu unatisha jamani!.. unapopewa tano shurti kuinua mikono na kushukuru....baraza zito sana!
Mzee Es,
Tunakaribisha mengi kutoka pande zote, mazuri na mabaya lakini sii sawa mabaya ya Mwinyi, Mkapa au JK kumsindikia Nyerere hali hawa ni viongozi ambao tumewapigia kura.... ikiwa tunafahamu Nyerere alikuwa mkosa kwa nini bado tuliwachagua?..
Nitazidi kusema Nyerere hakuwa mtume, naye pia alifungiwa kanyaboya na huyo Mwinyi, Mkapa na hata huyu JK. Wote walikuwa simba wenda kimya na hakika wanakula nyama! enzi za Nyerere walikuwa wasikivu huwezi kuamini kama ndio hawa wa leo.
Je, tulifanya nini baada ya miaka mitano ya Mwinyi pindi Nyerere aliposema Mwinyi hakuwa chaguo lake isipokuwa ilitokea tu kwa sababu ya Muungano!...Na ilijulikana kabisa kuwa chaguo lake lilikuwa SAS isipokuwa hakupitishwa kabisa na baraza la mapinduzi, na kama unakumbuka Wazenj walikuja juu ile mbaya wakaanzisha zengwe la kutaka muungano uvunjike ikabdidi Nyerere mwenyewe apange ziara ya Unguja bila kupenda. Alipotoka huko ndipo tuliposikia jina la Mwinyi...haya baada ya mika mitano, badala ya sisi kushtuka kukazidi kumpa sifa zaidi Mwinyi na hiyo RUKSA yake tukamzawadia miaka mitano mingine. Alipotoka alisema Mtanikumbukaaa! akiwa na maana Mkapa atatutoa KAPA.
Akaja Mkapa naye baada ya miaka mitano ya kwanza, Nyerere alikubali kupotea na kusema huyu ni kiongozi anayetoa maamuzi usiku kitandani anapolala na mkewe!..lakini bado tulimchagua kushika awamu ya pili.
JK inajulikana kabisa Nyerere hakupenda toka mwanzo wakati akimweka Mkapa. Na ni wakati huo wa Mkapa vilipozuka vikundi ndani ya CCM. Boys to men wakazuka wakiongozwa na mzee wao Mwaikambo. Mengine unayafahamu yote!
Yes, tunakubali Nyerere kuwa na makosa ktk uongozi lakini iwe basi ktk kipindi chake. Kuna mengi ya kuzungumzia kama vile Ujamaa na hayo maazimio yake zipo kasoro kibao. Lakini haya ya Nkapa na JK, kila mmoja wetu kaupanda mkenge huo ikiwa ni pamoja na Nyerere mwenyewe.
 
Mzee ES,
Sawa kabisa kumzungumzia Mwalimu. Hiyo si tatizo langu. Tatizo linakuja pale mtu anapoweka uwongo kuwa Mwalimu alisema Kambona si raia. Katu Mwalimu hakusema hivyo. Aliyoyasema hayo ni Malecela baada ya Kambona kurudi nyumbani wakati wimbi la multiparty limeanza. Kambona may have been Malecela's friend at one time lakini kumbuka wakati huu Kambona alikuwa kwenye chama tofauti na Malecela akiwa CCM damu damu na kuhofia kuwa Kambona may have an effect in Tanzania's politics wakaanza kumbomoa. That is a fact na hata ukiangalia magazeti ya wakati huo utaikuta hiyo statement. That was the point I was driving home. Let the debate continue.
 
Jasusi,

Nimekuelewa mzee wangu, na you have a point ingawaje Kambona aligeuka kuwa bomu ambalo hatukutegemea, aliporudi akasema kuwa atasema ukweli juu ya mali walizonazo Mwalimu na Kawawa nje ya nchi,

alipoambiwa aziseme akaishia kuwa bubu, wanasiasa uchwara!

Bob weka vitu mwanangu, huu uwanja unaingiwa na wakali wa nchi ni lazima tuuweke sawa, maana tunajua pumba iko wapi so is mchele!
 
Tarehe 10/23/2006
SIASA
\MWANANCHI
Waislam: Hatuna cha kujifunza kutoka kwa Wakatoliki

Mohamed Said
IMEBIDI kuandika makala hii kutokana na makala iliyoandikwa na Kaanaeli Kaale yenye kichwa cha habari ‘Kusigana kwa matokeo baina ya shule za Kikatoliki na Kiislamu' (Mwananchi 17 Oktoba 2006). Makala ilikuwa inaeleza yaliyojadiliwa katika mkutano ulioandaliwa na Shirika la Elimu ya Sheria Tanzania (TANLET) katika moja ya harakati za kumuenzi hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Katika mkutano huo, ilielezwa kuwa shule za Kikatoliki ndiyo shule bora zinazoshika nafasi ‘kumi bora' kwa kutoa matokeo mazuri ya mitihani na shule za Kiislam ndiyo ‘zinazoshika mkia' katika kutoa matokeo mabaya.
Ama taarifa hizo za shule za Wakatoliki kufanya vyema katika mitihani si habari mpya ni jambo linalotangazwa na vyombo vya habari kila mwaka kwa hiyo linafahamika. Ila kitu cha kushangaza ni kuwa kimezidi nini hii leo hadi ikawa ni muhimu kujadili ufanisi wa shule za Waislam hadharani kisha tukapewa ushauri kuwa Waislamu tujifunze kutoka kwa Wakatoliki ili nasi shule zetu zifanye vyema kama zao ili huu upogo wa elimu kati ya Waislam na Wakristo utoweke?
Ushauri huu umenitia simanzi kubwa na ndiyo hasa sababu ya kuandika makala hii. Bubu alizungumza kwa uchungu wa mwanaWe ni msemo mashuri. Leo hii sisi Waislam tumekuwa watu wa kusaidiwa na Wakatoliki tuelimike! Waswahili tuna msemo ‘Akutukanae hakuchagulii tusi.'
Laiti hao wanaotushauri wengeijua tarikh (historia) yetu wasingetamka hayo. Wamishionari wameingia nchi hii wamewakuta babu zetu pwani yote ya Afrika Mashariki na bara kulikokuwa na Uislam wakijua kusoma, kuandika na kuhesabu. Lakini haya tuyaache yanahitaji muda kueleza. Turudi kwenye mada husika.
Awali ya yote ni kumkejeli hayati Mwalimu Julius Nyerere kwa kuadhimisha kifo chake kwa mkutano wa kuzungumza kubaki nyuma kwa Waislam katika elimu kwa kuwa, kwa kauli yake mwenyewe alisema kuwa upogo katika elimu baina ya Waislam na Wakristo uliorithiwa na serikali yake kutoka kwa Waingereza yeye ameuondosha katika kipindi cha utawala wake.
Kauli hii aliitoa Novemba 5, 1985 katika hotuba aliyoitoa Ukumbi wa Diamond Jubille akiwaaga Wazee wa Dar es Salaam. Kabla hajastaafu urais, Mwalimu Nyerere alikuwa na haya ya kueleza kuhusu suala la elimu ya Waislam:
"Waislam wametupa nafasi kupitia sera yetu ya elimu, kurekebisha upogo. Sasa nipo katika hali ya kufurahia kwa kuwa wakati mwingine sielewi kama mbunge mpya, waziri, au katibu mkuu katika wizara zetu za serikali, ni mwislam au mkristo au hana dini labda pale jina lake la kwanza linapotoa utambulisho. Na hata hivyo hiyo siyo njia ya kuaminika kutoa utambulisho wa dini kwa kuwa tuna wakristo wenye majina ya Kiislam, na waislam wenye majina ya Kikristo. Kuvumiliana huku ndiyo sababu; nilichofanya mimi ni kuzungumzia maadili haya kwa niaba yenu."
Sasa ikiwa Baba wa Taifa keshawanyanyua Waislam katika elimu na kafurahishwa na kazi yake nzuri, hawa wanaokuja leo na kusema kuwa Waislam wako nyuma wanataka kumshika uongo Mwalimu Nyerere?
Wanataka hii leo kumsimamisha Baba wa Taifa kizimbani ajibu tuhuma za kuwakandamiza Waislam katika elimu? Kwa hakika si adabu wala ustaarabu kupinga kauli ya Mwalimu Nyerere kuwa hakusema kweli katika tatizo la elimu ya Waislam.
Je, hawa waliokuja na hoja hii nyeti wanatambua uzito wa kauli zao hasa katika kipindi hiki ambapo Kanisa Katoliki lipo katika mchakato wa kumfanya Mwalimu Nyerere kuwa mtakatifu? Hivi hawasikii nchi nzima inavyomtukuza Mwalimu Nyerere kwa sifa za uadilifu? Majibu wanayo wenyewe. Hili la kwanza.
Waswahili tuna msemo mwingine "Asiekujua hakuthamini.' Historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika ni ushahidi wa juhudi za Waislam katika kujitafutia elimu. Wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika tatizo la elimu ya Waislam ndiyo chanzo cha kuanzishwa chama cha upinzani Tanganyika All Muslim National Union (AMNUT) pale akina Ramadhani Mashado Plantan na wenzake walipotoka TANU mwaka 1958, sababu kuu wakihofu Wakristo waliokuwa na elimu kuja kushika madaraka peke yao katika Tanganyika huru na kuwaweka Waislam pembeni.
Suala hili lilileta mjadala mkubwa katika TANU. Ukipenda unaweza ukarejesha msuguano huu ndani ya TANU nyuma kidogo mwaka huo huo wa 1958 pale Sheikh Suleiman Takadir (aliyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU Dar es Salaam) alipomkabili Nyerere uso kwa uso na kumtuhumu kwa udini.
 
Haya yalitokea baada ya Uchaguzi wa Kura Tatu pale TANU ilipoteua Wakristo kusimama kugombea nafasi za Legislative Council na kuwaweka Waislam wana TANU pembeni. Lakini katika hili palikuwa na sababu maalum za msingi. Hapa si mahali pake kuzieleza. Kipande hiki cha historia kinaogopwa sana na kwa ajili hiyo nami sitokiendeleza.
Baada ya uhuru kupatikana mwaka 1961 Waislam kwa pumzi ile ile waliyopigania uhuru wakaingia katika harakati za kutafuta elimu. Hawakusubiri wajengewe shule na serikali. Wazee wetu waliitisha mkutano chini ya taasisi zao - Daawat Islamiyya (Mwito kwa Waislam), Jamiatul Islamiya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika na Muslim Education Union kujadili nini kifanyike ili Waislam wapate elimu waliyodhulumiwa na wakoloni.
Mipango ikatayarishwa ya kujenga shule Tanganyika nzima na mwishowe kujenga Chuo Kikuu cha kwanza kwa Waislam katika Afrika ya Mashariki. Huu ndiyo ukweli wa historia ya Waislam.
Waislam hatuna sifa ya uvivu wala kusubiri misaada kutoka Ulaya. Ufupi wa maneno ni kuwa shule sabini zilijengwa na EAMWS na jiwe la msingi la Chuo Kikuu liliwekwa na Mwalimu Nyerere mwenyewe kwa mkono wake. Sasa la kujiuliza ni kuwa juhudi hizi zote za kutafuta elimu ziliishia wapi na nini sababu yake?
Ufupi wa mambo ni kuwa Mwalimu Nyerere alipiga marufuku jumuia zote za Kiislam mwaka 1968 na akwaundia Waislam Baraza Kuu la Waislam Tanzania (Bakwata). Historia ya TANU na uhusiano wa Mwalimu Nyerere na Waislam ina majibu ya swali hili.
Mzee Rashid Mfaume Kawawa yu hai na ni shahidi wa yote yaliyopita katika kipindi kile. Mzee Kawawa anaweza kutoa majibu ya kitendawili hiki. Hili la pili.
Waswahili tuna msemo mwingine ‘Chokochoko mchokonoe pweza binadamu hutamuweza.' Imekuwa vyema leo hii, hili tatizo la elimu ya Waislam limesemwa na wasiokuwa Waislam maana laiti tungelisema Waislam tungeambiwa ‘siasa kali' tunataka kuvuruga ‘amani na utulivu' kama alivyosakamwa marehemu Profesa Kighoma Abdallah Ali Malima alipoionya serikali kuhusu hujuma dhidi ya Waislam kama alivyoikuta ndani ya Wizara ya Elimu.
Mwaka 1987 Profesa Malima aliteuliwa kuwa Waziri wa Elimu akiwa Muislam wa kwanza kushika nafasi hiyo. Mawaziri wanane waliopita walikuwa Wakristo. Kulikuwa na malalamiko kutoka kwa Waislam kuwa wizara hiyo imegeuzwa jimbo la Wakristo hasa Wakatoliki, maana ilifika hadi padri (Simon Chiwanga) kuteuliwa na Mwalimu Julius Nyerere kuongoza wizara hiyo.
Profesa Malima aliposhika wizara hiyo aliona upo umuhimu wa kufanya marekebisho kadhaa ili kurejesha imani ya Waislam katika wizara hiyo. Kulikuwa na tuhuma kuwa Wizara ya Elimu ilikuwa ikiwabagua vijana wa Kiislam kupata nafasi katika vyuo vya elimu ya juu na ilikuwa ikizuia kupanda vyeo kwa Waislam.
Tatizo hili liliwekwa wazi kwa mara ya kwanza mwaka 1981 na wanafunzi wa Sheikh Malik na ndiyo ikawa sababu ya yeye kufukuzwa nchini.
Profesa Malima alipoona dhulma ile iliyokuwapo katika wizara ile dhidi ya Waislam, aliwateua Waislam wanne kushika nafasi katika kurugenzi mbalimbali. Halikadhalika Profesa Malima alibadili mtindo uliokuwapo wa kutumia majina badala ya namba katika mitihani.
Baada ya mabadiliko yale mwaka ule idadi ya wanafunzi Waislam walifaulu kuingia sekondari ilipanda kwa asilimia 40. Profesa Malima akaandika taarifa ya siri kwa Rais Ali Hassan Mwinyi kumtaarifu udini ulioota mizizi Wizara ya Elimu.
Katika taarifa ile kwa rais Mwinyi, Profesa Malima alieleza kuhusu kudumazwa kwa Waislam kwa makusudi katika mgawo wa elimu. Taarifa hii ilivujishwa kwa vyombo vya habari na kwa Wakristo wengine.
Katika watu walioipata taarifa hii ni Mwalimu Nyerere akiwa mstaafu lakini akiwa Mwenyekiti wa CCM. Hiki kisa ni kirefu inatosha tu kusema kuwa yaliyomkuta Profesa Malima kwa kutaka kutenda haki hakuna asiyeyajua. Alisimamishwa kizimbani mbele ya Kamati Kuu ya CCM kwa udini na akatolewa Wizara ya Elimu.
Lakini kabla hatujatoka katika nukta hii ningependa kueleza kuwa katika moja ya sababu kuu iliyofanya serikali ikifungie kitabu kilichoandikwa na Profesa Hamza Mustafa Njozi Mwembechai Killings and the Political Future of Tanzania ni kule kuanika hadharani mbinu zinazotumika nchini kuwanyima Waislam elimu. Profesa Njozi's aliandika:
"…Arabia (May, 1985) wrote under the heading "A Closed Door to the Corridors of Power": ‘The majority of pupils in Tanzanian primary schools are Muslim (80 percent), a percentage which dwindles to 15-20 percent in secondary schools, sinking to a mere five percent at University level'. Almost fifteen years later, on 2 February, 1999 the Member of Parliament for Kigamboni Hon. Kitwana Kondo told the parliament that out of every 100 students who sat for the standard seven examination in Dar es Salaam in the year 1998, 71 were Muslim and 29 Christian. But out of every 100 students selected to join government secondary schools only 21 were Muslim while 79 were Christian. The MP wanted to know whether Muslim children were inherently dull (An-Nuur, February 5-11, 1999).
Yaliyomfika Mzee Kondo nayo yanafahamika. Yapo mengine mengi yaliyofichuliwa katika kitabu hicho yanayohusu mbinu zinazotumiwa katika kuhakikisha Waislam wanabaki nyuma lakini hapa hii leo si mahali pake. Hili la tatu.
Sasa leo Waislam tunaambiwa tukajifunze mbinu za Wakatoliki ili tuboreshe shule zetu…tukajifunze mbinu gani? Kuhodhi madaraka na nafasi katika Wizara ya Elimu na kujipendelea kwa kuwanyima Wakristo nafasi za elimu ya juu? Hili ni muhali kwa Waislam.
Hata kama tungekuwa na uwezo nalo Uislam unakataza vyote kudhulumu na halikadhalika kukubali kudhulumiwa. Kwa Waislam elimu ni fardh jambo ambalo ni lazima litekelezwa na kwa kushindwa kufanya hivyo mja huandikiwa dhambi. Hatuhitaji kujifunza kwa yeyote yule kuhusu umuhimu wa elimu. Historia ya Waislam wa Tanganyika inapingana na dhana hiyo.
Sasa tuzungumze kuhusu matokeo mabaya ya shule za Waislam. Kwangu mimi kwa uzoefu wangu na yale ambayo nayaelewa kuhusu historia ya Waislam wa Tanganyika hili linahitaji uchunguzi zaidi ili tudhihirishe kuwa kweli shule za Waislam zinashika mkia na za Wakatoliki ndiyo zinazotawala ‘kumi bora' miaka nenda miaka rudi kwa haki au ndiyo hizo hizo mbinu alizotahadharisha marehemu Profesa Malima na Mzee Kondo akahoji katika Bunge na zilizosababisha kitabu cha Profesa Njozi kifungiwe na serikali ya Rais Benjamin William Mkapa?
Katika Vita Kuu ya Pili ya Dunia, Wajerumani walikuwa wakiwakamata Wayahudi Poland na kwingineko Ulaya wakawatoa katika nyumba zao nzuri na kuwarundika katika ghetto. Umati mkubwa wa watu waliokuwa na nafasi na heshima zao katika jamii wakajikuta wanaishi katika sehemu finyu, chafu isiyo na mifereji ya maji taka wala maji safi.
Wajerumani wakawa wanatuhumu na kuwakashifu Wayahudi kwa uchafu. Katika hali kama hiyo vipi utategemea mtu awe msafi? Huu ndiyo mfano wetu Waislam hii leo.
Hatuna fursa sawa kama walizonazo Wakristo, shule zetu duni na juu ya hayo bado tunahujumiwa kisha tunalaumiwa kwa kutotoa matokeo mazuri. Hili la nne ambalo ningependa lizingatiwe.
Kwa taarifa kwa wale wasiojua ni kuwa Organisation of Islamic Conference (OIC) walitaka kujenga Chuo Kikuu Dar es Salaam. Watendaji Wakristo katika Wizara ya Elimu walipiga vita mradi huo na mwisho chuo hicho kikajengwa Mbale, Uganda.
Darul Iman ya Saud Arabia ilitaka kujenga shule ya ufundi Kibaha na yale yaliyoikuta OIC na wao yaliwafika sawia. Huu ndiyo ukweli wa nchi yetu. Waswahili tunapokabiliwa na mtu mwingi wa mbinu na ghilba tuna msemo maarufu tunautumia kumweleza mtu huyo. Tunasema ‘Kwa nyakanga hakwishi nyimbo.'
Kichwa kinaniuma kutaka kujua hii agenda ya kudumazwa kwa Waislam katika elimu iliyozuka ghafla bin vuu ni ya nani hasa, yao wenyewe TANLET au wametumwa na mtu? Kama wametumwa, nani huyu kawatuma na kwa maslahi ya nani?
Agenda hii si ndiyo iliyomfanya Profesa Malima aandamwe na hatimaye kufukuzwa Wizara ya Elimu? Agenda hii si ndiyo iliyomfanya Mwalimu Nyerere amfukuze Tanzania Bara Mufti Sheikh Hassan bin Ameir na kumrejesha Zanzibar chini ya ulinzi mkali na kuwaweka kizuizini wafuasi wake?
Agenda hii si ndiyo iliyomfanya Sheikh Hussein Malik afukuzwe nchini na serikali ya Mwalimu Nyerere baada ya wanafunzi wake kupitia taasisi yao ya Waandishi wa Kiislam (Warsha) kuzungumza kuhusu tatizo la elimu ya Waislam? Hii leo kimebadilika nini? Wakati una majibu kwa kila jambo, Waislam tusubiri.
 
Waislamu waambiwa amkeni

Na Burhani Yakub, Tanga

WAUMINI wa dini ya Kiislamu wametakiwa kuamka na kuanza kusisitiza umuhimu wa elimu kwa watoto wao, ili kuandaa kizazi kitakachoweza kumudu na kuikabili dunia ya sayansi na teknolojia kupambana na maadui wa dini hiyo.

Wito huo ulitolewa jana na Kiongozi wa Taasisi ya Kiislamu ya Ansaar Sunnah, Sheikh Salim Barahiyan, wakati akitoa nasaha kwa Waislamu waliokusanyika katika viwanja vya Tangamano Jijini hapa na kusali sala ya Idd El Fitri.

Waislamu wengine wanasali sala ya Idd El Fitr leo baada ya kumaliza mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan kwa siku 30 zilizopita.

Sheikh Barahiyan alisema miongoni mwa mambo yanayowaacha nyuma Waislamu wa Tanzania ni suala la elimu ambalo wengi wao wamekuwa wakilipuuza na kusababisha wasiokuwa Waislamu kutumia mwanya huo kujiendeleza.

"Ni jambo la kusikitisha wakati vyuo vikuu vinavyoendeshwa na madhehebu mengine nchini hadi sasa vinafikia zaidi ya saba, lakini Chuo Kikuu cha Kiislamu ni kimoja tu tena kuanzishwa kwake kuna mkono wa serikali," alisema Barahiyan na kulaumu shule za sekondari za Kiislamu ambazo alisema zinashikilia mkia katika mitihani ya kitaifa.

Kiongozi huyo alisema hakuna njia nyingine ya kuwakwamua katika lindi la umasikini vijana wa Kiislamu nchini, ila ni kupigania elimu kwa kuwa hata Sera ya Taifa inaelekeza kuwa ifikapo mwaka 2015 hata nafasi za maafisa watendaji wa vijiji, mitaa na kata ni lazima zishikiliwe na watu wenye elimu ya shahada ya chuo kikuu.

Kwa kutambua umuhimu wa elimu kwa vijana wa Kiislamu, Sheikh Barahiyan alisema taasisi yake imefungua shule katika mikoa mbalimbali nchini, ambazo zimekuwa zikitoa ushindani mkubwa katika mitihani ya kitaifa na kwamba ipo mbioni kujenga Chuo Kikuu.

Sala hiyo ya Idd iliendeshwa na Naibu Mudir wa Taasisi hiyo, Salimu Bafadhil, ambaye aliwataka Waislamu kuendeleza mema waliyokuwa wakiyafanya wakati wa mwezi wa Ramadhani na kuwatahadharisha wanaopanga kufanya maasi kuwa watakuwa wamejiharibia.

"Sikukuu ya Idd maana yake ni kusherehekea kwa kumtaja Mwenyezi Mungu sana, kula na kunywa vinywaji vitamu na kucheza michezo iliyokuwa ikifanywa na Mtume Mohamad S.A.W na siyo kulewa, kufanya zinaa na kufanya maasi," alisema Bafadhil.

Katika hotuba hiyo aliwataka Waislamu kuwa makini na sheria zinazobadilishwa kwa lengo la kupotosha maadili na mienendo ya dini hiyo na kusisitiza kuwa sheria za Kiislamu ziko palepale kwa kuwa zimewekwa na Mungu na siyo wanadamu.


Takbir!!!
 
Misikiti iliyojengwa wakati wa utawala wa mwinyi kama ingekuwa vyuo
wangefika mbali!

Kila mkoa na kila sehemu mabli mbali ilijengwa misikiti ambya kwa ukubwa inaweza kuzidi hata baadhi ya vyuo vingi tu vya private.

Lakini hapa uswahili la lawama kibao!
 
This was in todays The Citizen..

International Anti-Drug watchdog has ranked Tanzania 3rd position of countries with high cannabis sativa use,according to a National Anti-Drug Commission official.
Tanzania is ranked behind Mexico and the US,the leading drug users world wide.
 
Aisee Zanaki, hii kitu cannabis sativa a.k.a marijuana ni mmea wa heshima!

http://en.wikipedia.org/wiki/Cannabis_sativa

Sikushauri utumie lakini, unless una kikohozi au unataka kugeuka maksai kwa muda ulime weee bila kuchoka..

Pia ni viagra-pori!(i'm kidding)

teh teh

Wameipendelea TZ tu hapo, nederland wamekuwa wangapi?
 
This' a shame on us!

Lakini si JK kapewa list ya wahusika? Sijafatilia latest juu ya hatua zilizochukuliwa. Au ndo yaleyale kuwa wajadiliwe 'kimyakimya'? Hii ndo aibu sasa!

Hata mwekezaji anatuona sisi wapuuzi flani hivi. What a shame?
Inasikitisha
 
Kulikoni said:
Mkandara,

...nadhani hata hilo swali kuja Bungeni ilikuwa ni kufuatia 'tetesi' hizi .. lakini kabla hawaja hit point wakaambiwa muda wa maswali umekwisha!

Man, $100K per month!!? ... and still halijavaliwa njuga?

Binafsi huwa nashangaa pale inapotokea limeulizwa swali nyeti spika akasimama na kusema MUDA WA MASWALI UMEKWISHA. Hii huwa inanikatisha tamaa kabisa. Suala kama hili wala si la kuletea mzaha! Heri spika akahakikisha swali la jana yake linaendelezwa kumpa haki muulizaji.

Haki inakuwa ndogo wakati mwingine bungeni! Reason_____?
 
Kumekuwapo na Kasi kubwa ya viongozi wa kisiasa wa vyama vya upinzani kujiunga na Chama Cha Mapinduzi.

Mtandao wa JamboForums.com umeanza mpango wa kupata maoni ya wananchi kuhusu masuala muhimu yanayoikabili nchi yetu hivi sasa.

Nini maoni yako kuhusu suala zima la hatma ya Vyama vya Upinzani Tanzania.
 
WATANZANIA leo wanaadhimisha miaka 45 ya Uhuru wa Jamhuri ya Tanganyika (Tanzania Bara).


Miaka 45 si haba. Ni umri wa mtu mzima, tena mwenye wajukuu. Waliozaliwa Desemba 9, 1961, wako kwenye utu uzima.


Uhuru ni kitu muhimu katika maisha ya kiumbe chochote kilicho hai. Kama wanyama wanafurahia uhuru, seuze binadamu?


Kwa vyovyote iwavyo, leo ni siku muhimu katika historia ya nchi yetu. Ndiyo siku ambayo wakoloni wa Kiingereza walifunga virago na kurejea kwao.


Waliondoka baada ya kupora utajiri wetu mwingi. Walituonea kwa mengi. Wakatuletea dini zao na kuua dini zetu, waliua utamaduni wetu, wakatufanya kila jambo letu tulione kuwa ni la kishenzi. Athari za ukoloni, zipo hadi leo hii.


Miaka 45 baada ya uhuru, tujiulize maswali. Je, Tanzania na Watanzania tuko huru? Je, malengo ya kujitawala tumeyafikia? Je, tumelifanyia nini taifa letu?


Baada ya kuuondoa ukoloni mkongwe, sasa Tanzania na mataifa mengine ya dunia ya tatu, inakabiliwa na ukoloni mpya. Utandawazi ni ukoloni mpya. Utandawazi umeshaiathiri mno Tanzania. Utandawazi ni mbinu mpya ya mataifa ya kibeberu, kuendelea kuitawala dunia.


Wazee wetu walidai uhuru na hatimaye kuupata ili lijengwe taifa la watu huru. Lakini kwa bahati mbaya, Watanzania wengi hawajawa huru. Bado kuna uonevu ndani ya jamii yetu, kuna sheria zinazozuia uhuru wa Watanzania, na kuna mengi yaliyorithiwa kwa wakoloni, ambayo kwa kweli miaka 45 baadaye, hatukupaswa kuendelea nayo.


Lakini lililo kubwa ni je, Watanzania wamelifanyia nini taifa lao? Tunaona kuwa miaka 45 baada ya uhuru, moyo wa Watanzania kujituma, kufanya kazi kwa bidii ili kulijenga taifa lao, umekuwa ukipungua siku hadi siku.


Katika miaka ya 1960 hadi mwanzoni mwa miaka ya 1980, Watanzania walikuwa hodari katika kulijenga taifa lao. Walikuwa tayari kulitumikia taifa lao katika nyanja mbalimbali, na kwa kweli maendeleo yalionekana.


Hali ni tofauti sasa. Ubinafsi umewatawala wananchi wengi. Mashirika ya umma yamefilisiwa, mali zimeibwa, utajiri wa nchi umeangukia mikononi mwa wachache, hakuna anayejali tena kulinda mazingira au kuwa na uchungu na nchi yake.


Mambo yamekwenda mrama kiasi kwamba sasa baadhi ya watu wanachowaza ni kugawana nchi.


Watanzania wamekuwa hodari sana wa kuwashutumu viongozi. Wanataka wafanyiwe kila kitu. Wanataka wabebwe kila mahali. Wanataka wahudumiwe hata kwa yale wanayoweza kujihudumia. Hawajitumi, na hawaonyeshi dalili ya kubadilika.


Kila uchao, lawama ni kwa viongozi. Sawa viongozi ndio waliopewa dhamana ya kuongoza, lakini wanaochagua viongozi hao ni kina nani? Je, viongozi tulionao wanaingia madarakani kwa mapinduzi? Kwa udikteta? Au ni kwa kupitia sanduku la kura.


Kama wanatokana na masanduku ya kura, nani wa kulaumiwa? Ni wanaopigiwa kura au ni wale wanaopiga kura?


Wakati tukisherehekea sherehe hizi kubwa na muhimu kwa taifa letu, Watanzania tunapaswa kubadilika. Tutambue kuwa bila kulitumikia taifa letu, kamwe hatutaendelea.


Marekani, Ulaya au Asia inayoonekana leo, haikujengwa kwa kusubiri viongozi wafanye hili au lile. Wananchi, kwa kuongozwa na viongozi shupavu, walisimama kidete kuhakikisha wanajenga nchi zao.


Hali ni tofauti na sisi ambao kila kitu tunataka serikali itufanyie. Kwa kuendekeza tabia hii ya ajabu, uhuru wetu utakuwa hauna maana, kwani hatukujikomboa kutoka kwa wakoloni, ili mzigo wa maendeleo tuwaachie viongozi.


Tunapaswa tukumbuke maneno ya busara ya ‘Uhuru na Kazi’. Tusibweteke. Tanzania inapaswa ijengwe na Watanzania. Kuwashutumu viongozi, sawa; lakini wananchi nasi tujiulize, tumeifanyia nini Tanzania kwa miaka 45?

Freemedia
 
sounds like another propaganda

zaidi ya 40 yrs waTZ wanaambiwa wafunge mikanda that says it all

sasa sijui hiyo safari tutafika lini
 
Shy

Bado watanzania tuna kazi kubwa sana. Chama tawala kimetawala kila nyanja za uhuru wa watanzania. Tuna safari ndefu sana. Kunahitajika watu wa kuokoa taifa letu. Mwalimu Nyerere kila jambo alilolifanya miaka ya themanini alilitolea hoja na mpaka sasa unaweza kulisoma na kulielewa na kuona mantiki yake.

Sasa hivi ubabaishaji umekuwa mkubwa mno. Mtu anasema 3% anaongea na kutoa hoja ambazo hata mtoto mdogo hawezi kuzikubali!. Watanzania wanaitaji kuelimishwa, Elimu iliyopo haijaweza kuwatoa katika usingizi. Hiki kitu kinahitaji utaalamu wa hali ya juu ktk kukabiliana na propaganda za watu wanaogawana mali za nchi.

Nilishuudia Kenya wakati wa uchaguzi wakenya wakitoka kila kona ya dunia, Wengine waliendesha magari siku takribani tano kufika Kenya wakielekea kila jimbo kuhakikisha watu wanapata elimu ya kutosha kukabiliana na siasa za KANU walishinda na kuizika kabisa na haitafufuka tena. Na kwa Tanzania hatuna budi kutoa elimu kwa wapiga kura kwa nguvu zote.
 
Back
Top Bottom