Hii ndiyo Tanzania tunayoitaka

Hivi huu ushenzi mpaka lini hapa bongo? Hili limepita kwa taarifa hakuna wa kuhoji wala nini kama ilivyotokea kwa EWURA.Maskini ndio wanaoumia sana na haya maamuzi ya ajabu ajabu kwani kama kodi wanalipa sana lakini haitoshi hizi agencies zilizoundwa kisiasa nazo nazo zinakuja na charges zisizo na kichwa wala miguu.
 
Hizi siasa hadi kwenye vyombo vya huduma ya umma vitatupeleka pabaya.

Kodi TCRA wanapata nyingi tu kwenye huu mda wa hewani kwenye simu za viganjani.Wameweka viwango vya juu sana kulingana na kipato cha cha M-TZ.
Kwa nini watafute tena kwa walalahoi?
Kwanza wanatuibia hasa mtandao wa VODA.

Hivi hizi kodi za TZ zitatugandamiza hadi lini??
Kila kitu ukishika ni kodi,
hata kulala Gesti unalipa kodi,
kula chakula hotelini unalipa na Kodi,
kupanda daladala unalipa na kodi,
kutumia umeme unalipa kodi kwa serikali na pia EWURA,
Kunywa maji ya uhai na kilimanjaro unalipia na kodi,
mshahara unalipa kodi,
Ardhi ya Mungu unayokaa unalipia kodi,
jengo ulilojenga mwenyewe unalipa kodi
Ukifika bandarini na uwanja wa ndege ndo usiseme hizo kodi
Bado halmashauri zinatoza kodi
Kwa kipato gani hutamudu haya??????????
 
Illegal Taxes

I am mightily disappointed to see that the TCRA is trying yet another method of milking the people. They previously tried to demand that every TV owner pay them a yearly tax. That seems to have failed, so they have now imposed a tax of US$450 on “shop owners and vendors selling TV sets, cell phones and other electronic equipment”.

What is that word again.... Yes, "Wazee wa short-cuts"
 
Hivi mnafikiri kutengeza mabilionea kama walivyosema kuwa watatengeneza mabilionea 100 kutapatikana hivihivi, no lazima wananchi wa kawaida wakamuliwe kwa kila njia ili kuakikisha hawa walipewa madaraka wananweza kuwa mabilinea, wanajilipa mishahara mikubwa sana kwa pesa wanayo wakamua mwananchi wa kawaida ambaye milo miwili ya uhakika kwa siku hana.
 
Naona Invisible ameharibu hii hoja yangu kwa kuificha ndani ya hoja nyingine. Mimi niliianzisha kama THREAD inayoitwa “Mtanyonywa Mpaka Mtajuta”. Sasa ameiondoa toka sehemu ya SIASA ambapo niliiweka, na ameichomeka ukurasa 45 wa mada TOFAUTI.

Nitajaribu kuirudisha kwenye SIASA chini ya kichwa kisemacho: TCRA Wawabambikizia Walalohoi Kodi Ya Nusu Milioni. Namwomba Invisible asiipige vita, aiche hapo. Au ana mshiko huko TCRA?

Agustine Moshi
 
TANZANIA TUNAYOITAKA IPO

Kama kweli tunataka Tanzania imara huko tuendako naamini ipo Tanzania hiyo na inatusubiri kwa hamu kwa sababu Mungu ni mwema kwa watu wote. Ni sisi kuamua kwa pamoja.

Je,kuna Mtanzania leo hataki Tanzania yenye elimu bora?,kilimo bora?, barabara safi?, maji safi na salama?,huduma bora za afya?, na miundombinu iliyo imara?

Bila shaka kila mtanzania anataka kuliona Taifa linakuwa kwa nguvu kubwa kiuchumi huku masuala ya umasikini yakipungua kwa kasi kubwa sana. Je,tuko tayari kuitengeneza Tanzania kwa pamoja?, au wengine ni kupiga kelele wakati huo tumejiweka pembeni?.

Tuko tayari kukabiliana na changamoto zinazotukabili leo ili kuitengeneza nchi yetu kuwa imara?. Kama tuko tayari lazima tuanze kupanua bongo zetu na si kupanua midomo yetu tu. Juhudi,maarifa na ujasiri ndiyo siraha ya kuleta maendeleo.

Changamoto yetu ya kuitengeneza Tanzania tunayoitaka si kukosa mawazo ya kuifanya nchi yetu kuwa imara. Changamoto tuliyo nayo ni kukosa uwajibikaji imara uliyo na sura ya kitaifa ili kukabiliana na umasikini wa watanzania.

Changamoto yetu ya kuitengeneza Tanzania tunayoitaka si kutokuwa na ardhi yenye rutuba. Changamoto tuliyo nayo ni kupuuza kilimo na kuwapuuza wakulima wetu vijijini huku tukihubiri mijini asilimia kubwa ya watanzania wanategemea kilimo na kuja na maneno tu bila kudhamiria kuwasaidia wakulima.

Changamoto yetu ya kuitengeneza Tanzania tunayoitaka si kukosa wanasiasa wa rika mbalimbali. Changamoto tuliyo nayo ni kuwa na wanasiasa wanaosimama kuwawakilisha wananchi wakati huo huo wanaonyesha kama wanajiwakilisha wao na familia zao. Pili,kuwa na wanasiasa wanaowaza kujilimbikizia mali kwa kutumia ofisi za umma.

Changamoto yetu ya kuitengeneza Tanzania tunayoitaka si kukosa njia ya kuifanya elimu yetu iwe imara na ya ushindani. Changamoto tuliyo nayo ni kuwa na viongozi wanaopeleka watoto wao kusoma nje na kusomesha watoto wao kwenye shule bora hapa nchini na kujifanya kuzipenda na kuzisifia shule za umma. Pili,changamoto yetu kubwa ni kuwapuuza walimu wetu wanaojitolea kwa nguvu na akili nyingi kila siku.

Changamoto yetu ya kuitengeneza Tanzania tunayoitaka si kukosa njia ya kutengeneza reli yetu iwe imara na ya kuleta matumaini kwa masikini. Changamoto tuliyo nayo ni kuwa na viongozi wenye ama ubia na makampuni makubwa ya malori,ama kupata chochote au baadhi kumliki kabisa na kutokuwa na moyo dhabiti wa kukabiliana na changamoto hii.

Changamoto yetu ya kuitengeneza Tanzania tunayoitaka si kukosa njia za kupunguza umasikini. Changamoto tuliyo nayo leo ni kutoumizwa na hali ya Taifa letu na kujaa ubinafsi wa kijinga kabisa. Pili,kuwa na akili finyu kuwa wawekezaji ndiyo watapunguza umasikini wetu.

Changamoto yetu ya kuitengeneza Tanzania tunayoitaka si kushindwa kupambana na rushwa. Changamoto tuliyo nayo leo ni kupinga rushwa na wakati na sisi tunaitekeleza ipasavyo yaani tunatoa na kupokea rushwa.

Changamoto yetu ya kuitengeneza Tanzania tunayoitaka si kutokuwa na wanasayansi. Changamoto tuliyo nayo leo ni kutowasaidia watu wenye upeo wa juu kisayansi na kutegemea sayansi za kigeni. Pili,kuwakamata na ama kuwafunga wale wanaovumbua sayansi. Tatu,kukosa walimu wa sayansi kuanzia elimu ya awali,na hata wakiwepo uwezo wao wa kuwafundisha vijana wetu kuwa mdogo.

Changamoto yetu ya kuitengeneza Tanzania tunayoitaka si kukosa vijana wenye maadili mema. Changamoto tuliyo nayo leo ni kutowasaidia au kulegeza kamba ya kuwasaidia vijana wanaokosa maadili mema kuanzia ngazi ya kifamilia pamoja na taasisi zetu kama mashuleni.

Changamoto yetu ya kuitengeneza Tanzania tunayoitaka si kushindwa kupambana na wanaouza na kutumia madawa ya kulevya. Changamoto tuliyo nayo leo ni kupinga biashara na utumiaji wa madawa ya kulevya wakati wanaofanya biashara hiyo ni watu wetu wa karibu na sisi tunanufaika na biashara hiyo haramu kabisa.

Changamoto yetu ya kuitengeneza Tanzania tunayoitaka si kushindwa kuwa na wahitimu bora na walioiva kimafunzo,changamoto kubwa ni kuwa na na wahitimu wanaotegemea kuajiliwa tu kwa sababu ya mitaala ya elimu yetu. Pili, kuwa na vyuo vingi vinavyotegemea wahisani ndipo vifanye Tafiti za kijamii.

Changamoto yetu ya kuitengeneza Tanzania tunayoitaka si kushindwa kukabiliana na kundi la vijana lisilokuwa na ajira,changamoto kubwa ni kutokuwa na taasisi za kutosha,viwanda na kupuuza kilimo.

Mwisho

Kama kweli tunataka kuwa na Taifa imara lazima tuache kucheza na na sekta za elimu, kilimo pamoja na nishati na madini. Taifa likipuuza elimu haliwezi kujiamlia mambo yake leo na kesho, lazima tusimame na tuitetee elimu yetu. Elimu ikiwa imara itatusaidia kuwa na uelewa mpana kwenye sekta zingine zote.

Lazima tuwe na dira nzuri,tuijue historia yetu vizuri na tuwajibike kwa pamoja. Kelele nyingi haziwezi kututoa hapa tulipo. Tanzania imara inatusubiri,ili kuiona lazima tujitoe kweli kweli na tukumbuke kuwa tukiwa tunajitoa tujue wazi kuwa maendeleo yetu yatapatikana tu tukiwa na juhudi, maarifa na ujasiri
 
TANZANIA TUNAYOITAKA IPO

Kama kweli tunataka Tanzania imara huko tuendako naamini ipo Tanzania hiyo na inatusubiri kwa hamu kwa sababu Mungu ni mwema kwa watu wote. Ni sisi kuamua kwa pamoja.

Je,kuna Mtanzania leo hataki Tanzania yenye elimu bora?,kilimo bora?, barabara safi?, maji safi na salama?,huduma bora za afya?, na miundombinu iliyo imara?

Bila shaka kila mtanzania anataka kuliona Taifa linakuwa kwa nguvu kubwa kiuchumi huku masuala ya umasikini yakipungua kwa kasi kubwa sana. Je,tuko tayari kuitengeneza Tanzania kwa pamoja?, au wengine ni kupiga kelele wakati huo tumejiweka pembeni?.

Tuko tayari kukabiliana na changamoto zinazotukabili leo ili kuitengeneza nchi yetu kuwa imara?. Kama tuko tayari lazima tuanze kupanua bongo zetu na si kupanua midomo yetu tu. Juhudi,maarifa na ujasiri ndiyo siraha ya kuleta maendeleo.

Changamoto yetu ya kuitengeneza Tanzania tunayoitaka si kukosa mawazo ya kuifanya nchi yetu kuwa imara. Changamoto tuliyo nayo ni kukosa uwajibikaji imara uliyo na sura ya kitaifa ili kukabiliana na umasikini wa watanzania.

Changamoto yetu ya kuitengeneza Tanzania tunayoitaka si kutokuwa na ardhi yenye rutuba. Changamoto tuliyo nayo ni kupuuza kilimo na kuwapuuza wakulima wetu vijijini huku tukihubiri mijini asilimia kubwa ya watanzania wanategemea kilimo na kuja na maneno tu bila kudhamiria kuwasaidia wakulima.

Changamoto yetu ya kuitengeneza Tanzania tunayoitaka si kukosa wanasiasa wa rika mbalimbali. Changamoto tuliyo nayo ni kuwa na wanasiasa wanaosimama kuwawakilisha wananchi wakati huo huo wanaonyesha kama wanajiwakilisha wao na familia zao. Pili,kuwa na wanasiasa wanaowaza kujilimbikizia mali kwa kutumia ofisi za umma.

Changamoto yetu ya kuitengeneza Tanzania tunayoitaka si kukosa njia ya kuifanya elimu yetu iwe imara na ya ushindani. Changamoto tuliyo nayo ni kuwa na viongozi wanaopeleka watoto wao kusoma nje na kusomesha watoto wao kwenye shule bora hapa nchini na kujifanya kuzipenda na kuzisifia shule za umma. Pili,changamoto yetu kubwa ni kuwapuuza walimu wetu wanaojitolea kwa nguvu na akili nyingi kila siku.

Changamoto yetu ya kuitengeneza Tanzania tunayoitaka si kukosa njia ya kutengeneza reli yetu iwe imara na ya kuleta matumaini kwa masikini. Changamoto tuliyo nayo ni kuwa na viongozi wenye ama ubia na makampuni makubwa ya malori,ama kupata chochote au baadhi kumliki kabisa na kutokuwa na moyo dhabiti wa kukabiliana na changamoto hii.

Changamoto yetu ya kuitengeneza Tanzania tunayoitaka si kukosa njia za kupunguza umasikini. Changamoto tuliyo nayo leo ni kutoumizwa na hali ya Taifa letu na kujaa ubinafsi wa kijinga kabisa. Pili,kuwa na akili finyu kuwa wawekezaji ndiyo watapunguza umasikini wetu.

Changamoto yetu ya kuitengeneza Tanzania tunayoitaka si kushindwa kupambana na rushwa. Changamoto tuliyo nayo leo ni kupinga rushwa na wakati na sisi tunaitekeleza ipasavyo yaani tunatoa na kupokea rushwa.

Changamoto yetu ya kuitengeneza Tanzania tunayoitaka si kutokuwa na wanasayansi. Changamoto tuliyo nayo leo ni kutowasaidia watu wenye upeo wa juu kisayansi na kutegemea sayansi za kigeni. Pili,kuwakamata na ama kuwafunga wale wanaovumbua sayansi. Tatu,kukosa walimu wa sayansi kuanzia elimu ya awali,na hata wakiwepo uwezo wao wa kuwafundisha vijana wetu kuwa mdogo.

Changamoto yetu ya kuitengeneza Tanzania tunayoitaka si kukosa vijana wenye maadili mema. Changamoto tuliyo nayo leo ni kutowasaidia au kulegeza kamba ya kuwasaidia vijana wanaokosa maadili mema kuanzia ngazi ya kifamilia pamoja na taasisi zetu kama mashuleni.

Changamoto yetu ya kuitengeneza Tanzania tunayoitaka si kushindwa kupambana na wanaouza na kutumia madawa ya kulevya. Changamoto tuliyo nayo leo ni kupinga biashara na utumiaji wa madawa ya kulevya wakati wanaofanya biashara hiyo ni watu wetu wa karibu na sisi tunanufaika na biashara hiyo haramu kabisa.

Changamoto yetu ya kuitengeneza Tanzania tunayoitaka si kushindwa kuwa na wahitimu bora na walioiva kimafunzo,changamoto kubwa ni kuwa na na wahitimu wanaotegemea kuajiliwa tu kwa sababu ya mitaala ya elimu yetu. Pili, kuwa na vyuo vingi vinavyotegemea wahisani ndipo vifanye Tafiti za kijamii.

Changamoto yetu ya kuitengeneza Tanzania tunayoitaka si kushindwa kukabiliana na kundi la vijana lisilokuwa na ajira,changamoto kubwa ni kutokuwa na taasisi za kutosha,viwanda na kupuuza kilimo.

Mwisho

Kama kweli tunataka kuwa na Taifa imara lazima tuache kucheza na na sekta za elimu, kilimo pamoja na nishati na madini. Taifa likipuuza elimu haliwezi kujiamlia mambo yake leo na kesho, lazima tusimame na tuitetee elimu yetu. Elimu ikiwa imara itatusaidia kuwa na uelewa mpana kwenye sekta zingine zote.

Lazima tuwe na dira nzuri,tuijue historia yetu vizuri na tuwajibike kwa pamoja. Kelele nyingi haziwezi kututoa hapa tulipo. Tanzania imara inatusubiri,ili kuiona lazima tujitoe kweli kweli na tukumbuke kuwa tukiwa tunajitoa tujue wazi kuwa maendeleo yetu yatapatikana tu tukiwa na juhudi, maarifa na ujasiri

mkuu naunga mkono hoja.tuombe mungu atufikishe nchi ya ahadi
 
mkuu naunga mkono hoja.tuombe mungu atufikishe nchi ya ahadi

Inatakiwa tujitoe kweli na tubadilike sana. Lasima tubaeilike kuanzia kifikra mpaka kimatendo,lasivyo tutazidi kulalama kila siku bila hatua za kupigiwa mfano kimaendeleo. Tunaweza kabisa kuyafanya mataifa ya nje yawe yanakuja kuwekeza kwa adabu nchini kwetu.
 
TANZANIA TUNAYOITAKA IPO

Kama kweli tunataka Tanzania imara huko tuendako naamini ipo Tanzania hiyo na inatusubiri kwa hamu kwa sababu Mungu ni mwema kwa watu wote. Ni sisi kuamua kwa pamoja.

Lazima tuwe na dira nzuri,tuijue historia yetu vizuri na tuwajibike kwa pamoja. Kelele nyingi haziwezi kututoa hapa tulipo. Tanzania imara inatusubiri,ili kuiona lazima tujitoe kweli kweli na tukumbuke kuwa tukiwa tunajitoa tujue wazi kuwa maendeleo yetu yatapatikana tu tukiwa na juhudi, maarifa na ujasiri

Mkuu: mawazo yako mazuri, na hoja ni ya nguvu! Tafadhali tafakari haya:

1. Ujasiri - ujasiri wa kuwa na msimamo wa kutaka mabadiliko, hata kama itabidi kumwaga damu. Na kumwaga damu sina maana kuwaua wale wote wanaoliharibu taifa hili.. ni pamoja na wewe na mimi kujitoa kupinga ufidhuli na ufisadi wa walafi hata kama damu zetu zitamwagika, maana hao walio kwenye hizo nafasi hawatakubali kuondolewa kirahisi.

2. Ujasiri wa kuwakataa viongozi wasio na uzalendo, na kuwaweka wenye dira stahiki, hata kama itamaanisha wengi wetu kupotexa maslahi tunatogawiwa kutokana na ufisadi katika kila kona kuanzia kitongoji, kijiji, mtaa, kata, tarafa, wilaya, mkoa, ukanda hadi taifa.

3. Ujasiri wa kumfichua na kumnyooshea kidole jirani yako, ndugu yako wa karibu na hata wa ndani ya nyumba yako ambaye anaonyesha dhahiri kuwa ni mhujumu wa kimaadili, kiustawi wa jamii yetu, na kwa maendeleo tunayoyataka.

4. Ujasiri wa kukubali, kama kuna haja ya kujinyima ili tujenge kitu kizuri cha kudumu na kupunguza starehe , anasa na matanuzi yasiyo na maana tena ya kuiga tu, jambo ambalo WaTz tunaona shiiiiidah!

Mbadala: Kama ujasiri huu haupo na haupatikani kwa hiari, suluhishi ni moja tu.....fagia wahujumu woote!
 
Back
Top Bottom