Eli Cohen
JF-Expert Member
- Jun 19, 2023
- 1,309
- 4,017
■AHADI
Mungu alimbariki mzaliwa wa Ibrahim, Isaac, ambaye ndie mtoto halisi wa familia ya Ibrahim na Sarah iliotambulika kama ndio familia asilia ya agano la nchi ya ahadi dhidi ya mzaliwa wake wa kwanza aitwae Ismael aliezaa na mjakazi wake kutokana na utasa wa Sarah kabla ya kuambia atajifungua na malaika.
So, kiimani tutambue walibarikiwa. Ingawa bado walimkosea Mungu mara nyingi na akaruhusu adhabu juu yao ila bado asili ya baraka ilibaki juu yao.
■KUTAPAKAA KWA WAYAHUDI NA KUJITAFUTA KIUCHUMI
Baada ya uvamizi wa mara kwa mara pale Israel ilipelekea wayahudi kutapakaa sehemu tofauti duniani. Mostly Europe na baadae Marekani. Wayahudi waliendelea na shughuli tofauti za kimaisha na kibiashara. Katika harakati hizi Wayahudi walijijengea utamaduni wa kuinuana kiuchumi kwa kupeana fursa na connecrions na kurithishana mali na biashara kifamilia.
Kwa mfano kwa miaka hii Kuna agencies nyingi zilianzishwa ya jamii ya kiyahudi ili kusapoti wayahudi wenzao katika maeneo na nyanja tofauti za maisha.
Pia Wayahudi walijetengenezea utamaduni wa ustaarabu juu ya pesa. Hakika hata nyie mnaona wayahudi wengi matajiri sio watu wa kujionesha kwa misifa mingi kama jamii zetu zilizo tajiri
Wayahudi pia waliwekeza katika elimu. Yani wayahudi walipeleka watoto wao shule ili kurudi kuendesha biashara zao za familia na wengine kuajiriwa katika sector kubwa. Ndio maana leo mnaona Israel iko vizuri katika teknolojia, yani hadi wanatufundidha sisi kilimo cha kisasa ingawa hawana ardhi kubwa na yenye rotuba kama ya kwetu.
Ubaguzi dhidi ya Wayahudi katika nyanja za ajira ilipelekea biashara kuwa the only option kwa wayahudi. Hii ilipelekea kujijenga vyema katika sekta ya biashara na fedha.
■CHUKI DHIDI YA WAYAHUDI
Tambueni kuwa muhamad, muarabu, na muasiisi wa Islam alisisitiza kuwa yeye ni zao la Ismael mtoto wa Ibrahim. Kumbuka Ismael akupewa baraka ya urithi wa nchi ya ahadi. Kwa namna nyingine ni kama chuki ilijengeka juu uyahudi kwa maana waliona wao ndio warithi asilia kwa maana ndio watoto wa kwanza. Leo mnajionea ni jinsi gani jamii ya kiarabu na kiislam wanavyowachukia Waisrael.
hitler aliwachukia wayahudi kutokana na mafanikio na influence waliyokuwa nayo ujerumani. Alisisitiza kuwa wayahudi ndio waliokuwa maadui kwa jamii asilia ya Ujerumani. Hii ilipelekea kuua wayahudi milioni 6 kutoka sehemu tofauti za ujerumani na ulaya.
Chuki dhidi ya Wayahudi ipo hadi leo katika nchi tofauti. Hii inaitwa Antisemitism. Vinyongo dhidi maendeleo makubwa ya wayahudi na pia kutokana na nafanikio yao kuwa makubwa na jamii nyingine kuwa chini basi wanawajengea nadharia kuwa wayahudi ni wapiga deal na wakujipendelea wenyewe.
■■■■som pia uzi wangu wa;
Tambua kuwa Wapalestina sio Wafilisti
■PHILISTINE: Wafilisti walifika kaanani miaka ya 1175 BC wakitokea maeneo yaliyopo pwani ya bahari ya meditaranean. Asili ya wafilisti ilikuwa watu wa asili ya ugiriki wakati wa bronze age. Waliendelea hadi kuwa na miji yao maarufu ya Gaza, Ashdod, Ashkelon, Ekron na Gath. Nabii Ezekiel...
www.jamiiforums.com
Tambua kuwa Wapalestina sio Wafilisti