The Palm Beach
JF-Expert Member
- Dec 30, 2015
- 3,611
- 9,269
Makamu wa Rais wa Tanzania, Dkt. Emmanuel Nchimbi amewaomba viongozi wa dini kuendelea kumwombea Rais Samia Suluhu dhidi ya watu wabaya ili wasipate nafasi ya kumsogelea yeye mwenyewe na Ikulu.
Dkt. Nchimbi amesema hayo jana Ijumaa, Februari 6, 2026 wakati wa hafla ya Usimikaji na Uzinduzi wa Uongozi wa Awamu ya Tano wa The Council Of Pentecostal Churches Of Tanzania (CPCT) iliyofanyika Ukumbi wa Agape Life Church Mbezi Jogoo, jijini Dar es Salaam.
Dkt. Nchimbi amesema hayo jana Ijumaa, Februari 6, 2026 wakati wa hafla ya Usimikaji na Uzinduzi wa Uongozi wa Awamu ya Tano wa The Council Of Pentecostal Churches Of Tanzania (CPCT) iliyofanyika Ukumbi wa Agape Life Church Mbezi Jogoo, jijini Dar es Salaam.
- Waufukweni
- damu dini ikulu nchimbi viongozi viongozi wa dini
- Replies: 88
- Forum: Jukwaa la Siasa
Hiki ni kipande kidogo cha video clip cha hotuba ya VP Dr Emmanuel Nchimbi alipohudhuria mkutano wa CPCT jana tarehe 7/2/2026.
Ujumbe wa hotuba hii unasisitiza mambo kadhaa kwa ufupi:
1. Ametuomba watu wote kuiombea nchi na taifa letu
2. Kwamba, watu wengi hatujui nafasi ya Rais katika taifa/nchi yoyote. Kwamba, Rais (kiongozi mkuu wa taifa/nchi) akitikiswa, taifa na nchi yote inatikisika. (Kwa hili, binafsi nakubaliana na Vice President Dr. Emmanuel Nchimbi bila kujali Rais ameingia au kaupata huo uRais kwa njia gani, ya HAKI au HARAMU)
3. Amesisitiza tumwombee Rais Samia Suluhu Hassan ili Mungu ampe hekima, busara na roho ya ufahamu ili imwezeshe kutambua lipi jema analipoaswa kufanya na lipi baya asilopaswa kulifanya (Hili pia, binafsi nakubaliana VP Dr. Emmanuel Nchimbi).
4. Kipekee sana, amesisitiza kuwa tumwombee Rais Samia ili Mungu ampe roho ya kuwatambua na kuchagua wasaidizi wenye kumshauri mema na sio mabaya.
MAONI YANGU BINAFSI KWA WITO HUU WA VP DR. EMMANUEL NCHIMBI
👉🏻MOSI: Binafsi simpendi na nisingependa kumuona huyu mwanamke akiendelea kuwa Rais wa nchi na taifa letu kwa sababu kila mtu akiwemo yeye mwenyewe anajua na kutambua kwa hakika kabisa kuwa HAKUUPATA URAIS HUU KWA KURA ZA WANANCHI. AMEUPATA KWA ULAGHAI NA 'KUUA' MAELFU YA WATU ANAODAI KUWA ANAWAONGOZA!
👉🏻Lakini kwa kuwa kaupata Urais kwa njia zisizo halali, za ulaghai ndio maana yanampata yanayompata. Na honestly, Mungu amemruhusu ajiite na Rais wa Tanzania kwa malengo na makusudi maalumu. Kwa hiyo, hata kama mimi simpendi na sitaki awe Rais, ili mradi Mungu Yehova atawalaye mbingu na dunia ameruhusu hili, mimi ni nani nipinge?
👉🏻Ninachoweza kusema kwa sasa ni hili: KWAMBA, MAKUSUDI NA MAPENZI YA MUNGU WA MBINGUNI YATIMIZWE KTK NCHI NA TAIFA LETU KAMA VILE YATIMIZAVYO HUKO JUU MBINGUNI..!
👉🏻Naitikia wito wa Dr Emmanuel Nchimbi na haya ndiyo maombi yanvu nikisema maneno haya👇🏻👇🏻:
"......Mungu Jehovah muumba wa mbingu na nchi, wewe uwatawalaye wanadamu hapa katika nchi na mataifa kwa kuweka viongozi wanadamu kwa niaba yako namleta mbele zako Rais Samia Suluhu Hassan, japo ameupata utawala wa nchi na taifa letu hili la Tanganyika kwa njia ya ulaghai, udanganyifu kwa kuumiza na 'kuua' na kumwaga damu za watu wako mamia kwa maelfu, lakini ni wewe Mungu ndiye umemruhusu awe Rais wa nchi na taifa la Tanganyika ili malengo na makusudi yako yapate kutimizwa. Mimi sitapinga kamwe mipango yako eeh Baba na Mungu wangu wa mbinguni. Lililo ndani ya uwezo wangu ni kuleta maombi haya kwako juu ya Bi Samia Suluhu Hassan (Rais wa Tanganyika) kwamba, mpe hekima, busara na ufahamu wa kufanya maamuzi sahihi juu ya nchi na taifa hili. Mpe roho wa ufahamu apate kutambua lipi ni jema apaswalo kulitenda na kulifanyia maamuzi sahihi na lipi baya asiplopaswa kulitenda wala kulifanyia maamuzi yoyote. Ninafunga milango ya pande zote za nchi (kusini, kaskazini, mashariki na magharibi) ambayo roho za adui wabaya wa taifa hili wanapitia kwa watu wakiwa na sura za "washauri wa Rais" lakini lengo lao likiwa ni kuleta uangamivu na uharibifu kwa nchi na taifa letu. Baba na Mungu wangu wa mbinguni narudia tena kusema mbele zako na kuomba kuwa, umemruhusu Bi Samia Suluhu Hassan awe kiongozi mkuu wa taifa na nchi yetu kwa njia hiyo hiyo ovu aliyoitumia kujipatia Urais wa nchi. Natambua kuwa una kusudi jema kwa nchi na taifa letu. Mimi nasema kuwa MAPENZI NA MAKUSUDI YAKO NA YATIMIZWE SASA KATIKA NCHI NA TAIFA LETU KAMA YATIMIZAVYO HUKO MBINGUNI. Naomba haya kwa Jina la YESU KRISTO aliye hai. Amina🙏🏻🙏🏻..."