Benjamini Netanyahu
JF-Expert Member
- Aug 7, 2014
- 102,675
- 126,903
Twende kazini
Ukweli mchungu,hapa kwenye haya mabadiliko lazima watu tutapiga kelele sana kwani kiukweli panauma,ila itafika mahali tutazowea,maisha ya kiujanja ujanja yametugharimu sana,sasa ifikie mahali tuseme basi tufanye mambo kiuhalisia.Habari wana jf.
Nawapongeza HESLB kwa kazi nzuri ambayo mmeifanya naamini sasa mikopo hiyo imewafikia walengwa kwa Asilimia 89%
Ifike mahala watanzania tuweke siasa pembeni na tuache kushabikia mambo kwa kufuata mkumbo.. Tusitake Kuona eti idadi kubwa ya watu wamepewa mikopo angali wazazi wao wanauwezo Wa kuwalipia...Mfano kwa uchungu Mkubwa kuna hadi watumishi Wa umma nao miaka ya nyuma walipewa mikopo ambao wana mishahara wanauwezo Wa kujisomesha unakuta ana 80% asilimia halafu mtoto wa masikini ana 60%....lakini watu wanakuja na blah blah et mbona idadi ya watu ambao wamepewa ni ndogo,..ni kweli lazima vigezo na masharti vizingatiwe.. Mmefanya kazi nzuri.
Natokeaga "Busega""....
Wanaoumia ni wale tyu waliozoea pesa za bure bure..ili uitumikie pesa ni lazima uipate kwa shiidaaaa.....Tunapokusanya sana mapato tunapodhibiti sana matumizi unapopunguza sana wafanyakazi hewa bila shaka tunaokoa pesa nyingi sana swali mbona huduma zinazorota kila siku badala ya kuboreka kwa mapato yanayoingia matokeo, dawa hospital hakuna tumepunguza idadi ya wanapewa mikopo, biashara zinazorota kila siku why?
Ujinga ni mzigo kama ulizoea vya bure pole ila nazungumzia huduma muhimu hapo vipi?Wanaoumia ni wale tyu waliozoea pesa za bure bure..ili uitumikie pesa ni lazima uipate kwa shiidaaaa.....
Mi nilijisomesha mwenyewe kwa mshahara wangu mwenyewe....nashangaa Kuona watu ni watumishi halafu bado wanaomba mkopo halafu manakuja kulalamika uku.....unafiki wa watanzania sijui utaisha lini! unashindwa kufanya utafiti wa kile unachoongea ila kwasababu umepata wewe basi unabaki kuona kilichofanywa ni kizuri!
Mi niliweza tambua maisha ni kuchagua....Watu wanadhan gharama za chuo ni sawa na za secondary!!! Kule ni pagumu especially ktk accommodation, kwa hiyo kuyamudu hayo na wakati mwingine mzazi hata km mtumishi anao watoto wengine wanasoma na kimshahara chake chenye makato kibao, after all hiyo ni mikopo watailipa so wapewe tu
Nitakuwa kiongozi Mkubwa tyu ila si katika taasisi za mikonge....muache kila MTU apambane na maisha yake mwenyewe usimfanye MTU aone maisha mazuri kupitia wewe..Wabongo ni wabinafsi ndio maana Nchi ngumu mtoa mada umeonesha ubinafsi wako wewe ndio baadae usome uwe kiongozi sijui kama atasoma mtu kwa mkopo..
Wamepiga sana ma deal hawa jamaa....hiyo ya watumishi wa uma ni kweli, mtu anamkopo ana mshahara na bado kuna fungu halmashauri zilikua zina wapa, walio fanyia la maana kila la kheri ila wale wenzangu wa bata na totoz hiro era isha pita