Heshima kitu cha bure! Kwanini Rais Samia, japo sio lazima apendwe na wote lakini ni lazima aheshimiwe na wote? Akosolewe kwa staha na asitukanwe!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,499
113,610
Wanabodi,
Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na makala zangu za kwa maslahi ya taifa, makala ya leo ni makala elimishi ikielimisha kuhusu heshima ni kitu cha bure, hivyo kuwaelimisha wana jf na mitandao ya kijamii, kwanini Rais Samia, japo sio lazima apendwe na wote, lakini ni lazima aheshimiwe na wote kwasababu mtu akiishakuwa rais wa nchi, hapo hapo ana assume dual personality, yaani wanakuwa ni watu wawili in one!, hivyo rais wa nchi ni lazima aheshimiwe kwa heshima ya lazima ya kimamlaka, akosolewe kwa lugha ya staha, asitukanwe wala asitusiwe!.

Hoja hii ni kufuatia mjadala mingi kwenye mitandao ya jamii kwenye issue ya Bandari yetu na DPW, kuna watu wamevuka mipaka na kumkosea heshima Rais Samia na kumkosoa kwa lugha kali, kumtweza, kumkashifu na wengine kuvuka mipaka kwa kumtukana hadi matusi ya nguoni!, this is not right!.

Angalizo la Uzalendo Uchawa Vs Uzalendo Halisi!.

Kufuatia kuibuka kwa dhana ya uchawa, kuna watu wanajiita kabisa chawa wa Mama, hivyo mtu kama mimi nikijitokeza kutaka Rais Samia aheshimiwe wote, watu wenye akili fupi hawachelewi kuniona chawa!. Mimi sio chawa na hili sio bandiko la uchawa! ni bandiko la kukumbushana heshima ya kiasili ya Kiafrika ya heshima kitu cha bure, mkubwa kumheshimu mdogo, na mdogo kumheshimu mkubwa, heshima kwa wote.

Declaration ya Kutosaka Uteuzi.
Kumezuka mtindo wa sisi waandishi wa habari na watu wa media, tukiusifu utawala kwa mazuri au tukisifu viongozi, tunaonekana kuwa tunasaka uteuzi, naomba niwahakikishie tena Paskali hasaki uteuzi wowote na hili Paskali aliisha mueleza mteuzi mwenyewe face to face Pongezi Zangu ni Bonafide-Genuine! Sisaki Teuzi, Sitaki Teuzi, Niko Naye Mbeya, Nitamweza!

The Duality of President. heshima ya lazima ya kimamlaka!, Akosolewe kwa Staha na Asitukanwe!.
Duality ni kanuni ya mtu mmoja ku na personalities mbili kwa wakati mmoja.
Rais wa nchi ni dual personality ana personalities mbili ambazo ni duality but they exist in one!. Yaani ni mtu mmoja mwenye two personalities ambazo zina exist in one and at the same time.

Kanuni hii ya double personalities au dual personality imezungumzwa vizuri na Mwana Saikolojia mahiri wa Marekani, Dr. Segmund Freud katika kukichambua kitabu cha Dr. Jekyll and Mr. Hyde, kilichoandikwa na Dr. Robert Luis Stevenson aliyeandika pia kitabu cha Kisiwa chenye Hazina, Treasure Island, ambapo mtu mmoja mwenye double personality mchana yuko vingine na usiku yuko vingine kama watu wawili tofauti.

Hii duality ipo sana kwa binadamu wote, yaani nafsi na roho, au me & I. mambo kama ya de javu, third eye, physical body na astra body, mambo ya ying na yang, vyote hivi vinatumia kanuni ya duality.

Wanawake wengi wanalelewa kwa kuandaliwa kuwa wife materials, ili kupata mchumba hivyo katika kusaka ndoa anakuwa na one personality na akiisha pata ndoa na kuolewa, ana change na ku show her true colours!.

Jamii zetu nyingi za kiasili za Kiafrika kina watu wanaishi double life mfano mzuri ni wanga, wachawi na washirikina, ukiwaona mchana ni watu wa kawaida, lakini usiku ni watu wengine kabisa!.

Na kwenye siasa ndio usiseme!.

Persnality ya kwanza ya Rais wa nchi ni human personality, yaani rais ni binadamu, a human being kama binadamu mwingine yoyote wa kawaida anayestahili mahitaji tote ya kibinadamu, hivyo rais wetu Samia ni mtu anayeitwa Samia Suluhu Hassan, Huyu ni human being, she has all human needs including feelings, love and compassion na ana mahitaji mengine yote ya kibinaadamu ikiwemo kupenda, kupendwa na heshima, love and dignity and can make mistakes just like any other human beings. Hivyo huyu Samia ambaye she is only a human, unaweza kumpenda au usimpende, unaweza usimkubali, unaweza kumbeza, unaweza kumtukana na kumdhalilisha au kusema chochote kumhusu mtu anayeitwa Samia Suluhu Hassan na hakuna tatizo!. Mfano mzuri wa hili ni huyu mtu niliyemzungumzia hapa Ikitokea kuna Kiongozi ana Macho mazuri, na umeyapenda, je, kuna ubaya kumsifia macho yake? Ni ukosefu wa heshima na adabu? bandiko kama hili liliwezekana kupandishwa kwasababu she is just a human na enzi hizo alikuwa na single personality, sasa with dual personality bandiko kama hili haliwezi kupanda.

Jee ni lazima kumpenda Rais?.
Kumpenda mtu yoyote ni person preferences, mtu yoyote anaweza kumpenda mtu mwingine yeyote, kwa sababu zozote au bila sababu, au unaweza usimpende kwa sababu zozote, au bila sababu, na hakuna kosa lolote kutompenda yeyote lakini hata ikitokea mtu fulani humpendi, bado una wajibu wa kumheshimu na kuulinda utu wake.

Hivyo watu wako huru kumpenda Rais Samia ama kutompenda, it's an option lakini kumheshimu is not an option ni wajibu ndio maana kumtukana mtu ni kosa.

Personality ya pili ya Rais Samia, ni rais wa nchi, hivyo huyu binadamu anaitwa Samia Suluhu Hassan, baada ya kuwa ni rais wa nchi ana, assume kitu kinachoitwa presidential personality, huyu sasa sio mtu binadamu, ni mtu taasisi yenye mamlaka ya juu kabisa ndani ya JMT, hivyo rais wa nchi kwa personality yake ya urais, ni lazima aheshimiwe, utii kwa mamlaka, huwezi kumtukana, huwezi kumdhalilisha, itakuwa ni kuitukana taasisi ya urais. Dini zote zinafundisha utii kwa mamlaka, iwe ni mamlaka halali au haramu, una wajibu wa kutii mamlaka, ndio maana hata enzi za yule Blaza wangu, kabla hajagombea urais, toka ile 2014 nilipoambiwa ni yeye, nilileta angalizo humu Elections 2015 - Mgombea wa Urais Kwa tiketi ya CCM, 2015 "Could Be" John Pombe Magufuli baada tuu ya kushinda nikatoa ushauri huu Elections 2015 - If you can't beat them, join them! He is the worst dictator. Let's pray for him! na pia nikatoa angalizo hili Elections 2015 - Kama Hii ni Kweli, Then, Serikali Yetu ni Serikali Dhalimu?, Haramu?. Hukumu ya Karma ii Juu Yake!
Hivyo despite all the odds heshima na utii kwa mamlaka ni jambo la wajibu!.

Rais Samia kama taasisi ya urais, huhitaji kumpenda lakini ni lazima kumheshimu!. Rais Samia kama taasisi ya urais, she is not human, hawezi kufanya makosa ndio maana hawezi kushitakiwa!.

Wito kama huu niliwahi kuutoa enzi za utawala wa JK, Mapungufu ya Kikwete: Constructive Criticisim! na wakati wa Magufuli pia nilishauri Wito Kwa wana JamiiForums kuhusu ukosoaji wa Rais Magufuli
Hivyo sasa tuko na Samia, tunaweza tusimpende lakini lazima tumuheshimu na ukitokea ukosoaji, tumkosoe kwa lugha ya staha na sio kumtukana na kumdhalilisha.

Niliwahi kushauri humu kuwa Rais Samia, sio malaika ni binadamu anaweza kukosea. Tusimlaumu, kumshutumu na kumponda kwa makosa ya kukoseshwa. Tumvumilie tumpe muda unaweza usimpende lakini ni lazima kumheshimu.

Hitimisho
Rais Samia ni rais wetu, tumpende, tumheshimu, tumsuport, na hata ikitokea, kuna sehemu anakosea tumkosoe kwa heshima na staha.
Kwa sisi wengine ambao tunamkubali Samia kama Mama, mzazi wako, hata akukosee vipi, kamwe huwezi kumtukana!. Samia ni Mama wa Taifa, tumheshimu.

Namalizia kwa msisitizo huu

Heshima Kitu cha Bure, Rais Samia, ni lazima aheshimiwe na wote, akosolewe kwa staha na asitukanwe!.​

Paskali
 
Me naona kama anajitusi yeye mwenyewe.. na wewe ndio naona kama unaendeleza kumtusisha Mayalla umekuwa kama Nabii tito unapinga ushoga kwa mababgo yaliyoandikwa matusi...

Ujumbe kwa raisi.. Mtu mzima nguo ikikuvuka chutama la sivyo watu watashawishika vibaya.. so unakuwa wewe ndiye mkosaji...

Acheni Watanganyika wapiganie vyao.. urithi huu ulitunzwa vizuri kisha anakuja mtu hata hatumjui kwenye Marathi anauza mali ya yatima... mjalana ... Watanzania now wanahisi wamepata False President
 
Hayupo yeyote mwenye akili timamu, anayejiheshimu, aache kumheshimu mwingine, na mara zote, heshima ya mtu hulindwa na mtu mwenyewe, usijivunjie heshima yako mwenyewe, kwa matendo na maneno yako ya kijeuri kwangu, halafu utegemee niendelee kukulindia heshima yako, huo ni ujinga usiowezekana.

Na kwa wale chawa Pascal Mayalla ukiwemo, wanaotulazimisha kumheshimu mtu aliyeshindwa kujiheshimu mwenyewe, kuheshimu thamani ya utu wetu, thamani ya ardhi yetu na mipaka yake, nawashauri waendelee na mapenzi yao ya kijinga, ili mwisho wa siku kwasababu wamechagua kuongozwa na mjinga, basi wote wakatumbukie shimoni, lakini wasitarajie kututumbukiza werevu.
 
Wanabodi,
Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na makala zangu za kwa maslahi ya taifa, makala ya leo ni makala elimishi ikielimisha kuhusu heshima ni kitu cha bure, hivyo kuwaelimisha wana jf na mitandao ya kijamii, kwanini Rais Samia, japo sio lazima apendwe na wote, lakini ni lazima aheshimiwe na wote kwasababu mtu akiishakuwa rais wa nchi, hapo hapo ana assume dual personality, yaani wanakuwa ni watu wawili in one!, hivyo rais wa nchi ni lazima aheshimiwe kwa heshima ya lazima ya kimamlaka, akosolewe kwa lugha ya staha, asitukanwe wala asitusiwe!.
Mkuu paskali mafumbo ya nini mwambie Lissu aache kumtukana mama!
 
Wanabodi,
Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na makala zangu za kwa maslahi ya taifa, makala ya leo ni makala elimishi ikielimisha kuhusu heshima ni kitu cha bure, hivyo kuwaelimisha wana jf na mitandao ya kijamii, kwanini Rais Samia, japo sio lazima apendwe na wote, lakini ni lazima aheshimiwe na wote kwasababu mtu akiishakuwa rais wa nchi, hapo hapo ana assume dual personality, yaani wanakuwa ni watu wawili in one!, hivyo rais wa nchi ni lazima aheshimiwe kwa heshima ya lazima ya kimamlaka, akosolewe kwa lugha ya staha, asitukanwe wala asitusiwe!.
Pascal Mayalla hoja yako ni nzuri na ni ya msingi sana tena sana. Bahati mbaya sana maji yalishamwagika tangu siku ile Rais wetu Dkt Samia alipoanza kuonesha viashiria vya kudhihaki/kukebehi/kudharau/kubeza/kukaaa kimya pale kauli tata za kutweza utu wa Dkt Magufuli na yeye mwenyewe pia kutoa kauli tata kipindi cha maombolezo. Tena tuliandika hata wewe ni shahidi, tena tulimuomba mara kibao hata Maxence Melo waangalie utaratibu wa kufunga na kuzui posti zote zinazotweza utu wa aliyetumikia taifa kwa uzalendo ila hatukusikilizwa. Sisi wachambuzi hatushangai maana hii tabia alianza kuilea Dkt Kikwete kwa wapinzani mpaka wakamuita dhaifu, akaja Dkt Magufuli akahakikisha tunakuwa na staha ila kaja Rais Dkt Samia akasema eti kulikuwa na simba ya Yuda ….
 
Wanabodi,
Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na makala zangu za kwa maslahi ya taifa, makala ya leo ni makala elimishi ikielimisha kuhusu heshima ni kitu cha bure, hivyo kuwaelimisha wana jf na mitandao ya kijamii, kwanini Rais Samia, japo sio lazima apendwe na wote, lakini ni lazima aheshimiwe na wote kwasababu mtu akiishakuwa rais wa nchi, hapo hapo ana assume dual personality, yaani wanakuwa ni watu wawili in one!, hivyo rais wa nchi ni lazima aheshimiwe kwa heshima ya lazima ya kimamlaka, akosolewe kwa lugha ya staha, asitukanwe wala asitusiwe!.
Ni muhimu ucheki kalenda ujue upo mwaka gani nadhani unachanganya majira.
 
Hakuna uongozi mbaya kama huu wetu wa kiafrika unachukiza sana lakini swala la kumtukana kiongozi hilo halikubaliki .

Watanzania wengi wanapenda kuiga ,unakuta mtu mwengine anamtukana Rais halafu yupo nje ya nchi na uraia kabadilisha kabisa halafu na yeye yupo huku na ugali wa kwangu pakavu tia mchuzi anaiga mwisho wa siku wakiwekwa ndani wanaanza kusambaza hashtag .

Viongozi wa CCM hawajawahi kuwa bora lakini kuwe na mstari kwenye kukosoa na kuwaheshimu
 
Wanabodi,
Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na makala zangu za kwa maslahi ya taifa, makala ya leo ni makala elimishi ikielimisha kuhusu heshima ni kitu cha bure, hivyo kuwaelimisha wana jf na mitandao ya kijamii, kwanini Rais Samia, japo sio lazima apendwe na wote, lakini ni lazima aheshimiwe na wote kwasababu mtu akiishakuwa rais wa nchi, hapo hapo ana assume dual personality, yaani wanakuwa ni watu wawili in one!, hivyo rais wa nchi ni lazima aheshimiwe kwa heshima ya lazima ya kimamlaka, akosolewe kwa lugha ya staha, asitukanwe wala asitusiwe!.
Haya ndo yana tugharim ,mtu ni fisadi wa kutisha ila anataka apewa uheshimiwa
 
Me naona kama anajitusi yeye mwenyewe.. na wewe ndio naona kama unaendeleza kumtusisha Mayalla umekuwa kama Nabii tito unapinga ushoga kwa mababgo yaliyoandikwa matusi...

Ujumbe kwa raisi.. Mtu mzima nguo ikikuvuka chutama la sivyo watu watashawishika vibaya.. so unakuwa wewe ndiye mkosaji...

Acheni Watanganyika wapiganie vyao.. urithi huu ulitunzwa vizuri kisha anakuja mtu hata hatumjui kwenye Marathi anauza mali ya yatima... mjalana ... Watanzania now wanahisi wamepata False President
Nimefikiria sana neno la mwisho eti FALSE president. Wezi ndo wanapenda raisi wa namna hii
 
Wanabodi,
Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na makala zangu za kwa maslahi ya taifa, makala ya leo ni makala elimishi ikielimisha kuhusu heshima ni kitu cha bure, hivyo kuwaelimisha wana jf na mitandao ya kijamii, kwanini Rais Samia, japo sio lazima apendwe na wote, lakini ni lazima aheshimiwe na wote kwasababu mtu akiishakuwa rais wa nchi, hapo hapo ana assume dual personality, yaani wanakuwa ni watu wawili in one!, hivyo rais wa nchi ni lazima aheshimiwe kwa heshima ya lazima ya kimamlaka, akosolewe kwa lugha ya staha, asitukanwe wala asitusiwe!.

Hoja hii ni kufuatia mjadala mingi kwenye mitandao ya jamii kwenye issue ya Bandari yetu na DPW, kuna watu wamevuka mipaka na kumkosea heshima Rais Samia na kumkosoa kwa lugha kali, kumtweza, kumkashifu na wengine kuvuka mipaka kwa kumtukana hadi matusi ya nguoni!, this is not right!.

Angalizo la Uzalendo Uchawa Vs Uzalendo Halisi!.

Kufuatia kuibuka kwa dhana ya uchawa, kuna watu wanajiita kabisa chawa wa Mama, hivyo mtu kama mimi nikijitokeza kutaka Rais Samia aheshimiwe, watu wenye akili fupi hawachelewi kuniona chawa!. Mimi sio chawa na hili sio bandiko la uchawa! ni bandiko la kukumbushana heshima ya Kiafrika ya heshima kitu cha bure, heshimu mkubwa, mdogo, heshimu wote.

Declaration ya Kutosaka Uteuzi.
Kumezuka mtindo wa sisi waandishi wa habari na watu wa media, tukiusifu utawala kwa mazuri au tukisifu viongozi, tunaonekana kuwa tunasaka uteuzi, naomba niwahakikishie tena Paskali hasaki uteuzi wowote na hili Paskali aliisha mueleza mteuzi mwenyewe face to face Pongezi Zangu ni Bonafide-Genuine! Sisaki Teuzi, Sitaki Teuzi, Niko Naye Mbeya, Nitamweza!

The Duality of President. heshima ya lazima ya kimamlaka!, Akosolewe kwa Staha na Asitukanwe!.
Duality ni kanuni ya mtu mmoja ku na personalities mbili kwa wakati mmoja.
Rais wa nchi ni dual personality ana exist in duali,

Naomba usichangie kwanza, inaendelea ...

P
Kaka Paskali,
Heshima ipo kwa namna mbili, ya kwanza ni heshima itokanayo na nafasi au cheo chako na ya pili i ile itokanayo na namna mtu anavyowaheshimu wengine. Heshima itokanayo na nafasi huwa haivunjwi, ila hii inayotoka na namna mtu anavyowaheshimu wengine ndiyo ambayo huvunjwa. Kwa bahati mbaya, zote mbili zipo kwa mtu mmoja na hili husababisha kushindwa kutofautisha ipi hasa iliyovunjwa.
 
Back
Top Bottom