Mheshimiwa waziri mama
Dkt. Gwajima D tafadhali sana, naomba mfikishie hili Mh. Rais kwenye vikao vya baraza lenu la mawaziri kaliongee. Ama kama kuna namna nyingine nzuri ya kuongea naye ongea naye, kuhusu suala la umeme.
Kwenye umeme mama Samia binafsi sioni juhudi zake. Kama nakosea naomba mnisamehe na mnikumbushe. Kiangazi mabwawa yanakauka, haya sasa mvua kila siku mbona hakuna nafuu?
Viongozi wa serikali mnatuambia tujiajiri, sawa, lakini mbona umeme wenyewe haupo?
Mnataka tukalime?
Hatuwezi sote kuwa wakulima. Kila mtu anazitazama fursa katika angle yake. Mimi nikitazama mabango sehemu za biashara, magari, nguo, na vifaa vingine naona fursa ya kufanya print works. Naamua kuwekeza nguvu huko, nakaa na mashine zangu masaa 7 hakuna power. What a shameful country?
Vipi kijana wa salon
Vipi kijana wa welding
Vipi kijana wa wooden furniture?
Vipi kuhusu mshonaji? Hata yule aliyeomba cherehani, pengine mtaleletea ya umeme. Mtakuwa mmemsaidia?
Huko mama Samia nchi za watu anakokwenda mara kwa mara hajifunzi? Haulizi, haoni? Wenzetu wanafanyaje kupata reliable sources of energy?
Noneteheless, naomba mfikishie mh Rais alivunje shirika la umeme Tanzania. Tuwe na mamlaka za umeme kila mkoa kama ambavyo inafanyika kwenye maji. Kila mkoa utarithi mali za Tanesco mkoani kwake. Na kila mkoa utafute vyanzo vya uhakika vya umeme. Shida ya umeme ya Mwanza haitakuwepo Dar. Na ya Dar haitakuwepo Dodoma. Nchi nzima tatizo ni moja. Kwanini?
Pengine shirika la umeme Dar es Salaam lingefikiria kuzalisha umeme toka baharini, kuna upepo na mawimbi mengi, Pwani, Lindi, Mtwara wangetumia mto kama Rufiji na Ruvuma na bahari pia.
Wenye umeme wa ziada watauza kwa mikoa yenye uhitaji, bei nzuri ili nao wauze kwa watumiaji wake.
REA iachwe kama ilivyo RUWASA iendelee kushughulikia vijijini huko.
RAIS SAMIA TAFADHALI IVUNJE TANESCO