Here we go again: US to suspend immigrant visa processing from 75 countries (including Tanzania) over public assistance concerns

Here we go again: US to suspend immigrant visa processing from 75 countries (including Tanzania) over public assistance concerns

Yes, waliiboresha kwa kuipanua.

Wenzetu hawa aisee.

Nashukuru mie pia nilipata nafasi ya kumalizia masters yangu (miaka ya 2000s) kwenye chuo (jina kapuni) wale watu wasije kunitafuta kwenye alumni), na sasa nimelowea hapa Brooklyn.
Vizuri sana.

Hapo Brooklyn nimepitia sana sehemu inaitwa Crown Heights kuna mrembo mmoja alikuwa ananileta sana hapo miaka hiyo hiyo.
 
Vizuri sana.

Hapo Brooklyn nimepitia sana sehemu inaitwa Crown Heights kuna mrembo mmoja alikuwa ananileta sana hapo miaka hiyo hiyo.
Daah totoz za hapa ziko poa zapenda mazoezi mwakutana kwenye jogging pale Brower Park.

Utakuwa ulichezea sana kituo cha train cha Utika.

Pana wayahudi wengi sana hapa na kiukweli New York ni political neutral city.

Yanikumbusha nilipokuwa nikipiga kazi UK pana kakitongoji chaitwa Stanford Hill (Kaskazini mwa London) pana wayahudi wengi sana pale.
 
Daah totoz za hapa ziko poa zapenda mazoezi mwakutana kwenye jogging pale Brower Park.

Utakuwa ulichezea sana kituo cha train cha Utika.

Pana wayahudi wengi sana hapa na kiukweli New York ni political neutral city.

Yanikumbusha nilipokuwa nikipiga kazi UK pana kakitongoji chaitwa Stanford Hill (Kaskazini mwa London) pana wayahudi wengi sana pale.
Utica ndiyo kilikuwa kituo changu pale.

West Indian Parade Day hapo never miss unakutana na kina Rihanna kibao wamepagawa woote nusu utupu 😂😂😂

all-jouvert-and-west-indian-day-parade-called-off-again-because-of-covid-2021-09-0301BCPRINT_W...jpg
 
Utica ndiyo kilikuwa kituo changu pale.

West Indian Parade Day hapo never miss unakutana na kina Rihanna kibao wamepagawa woote nusu utupu 😂😂😂

View attachment 3530063
Never Miss kila Jumatatu ya kwanza ya mwezi September.

Huwezi jutia maana ukipata "angle" nzuri waweza kusimama na kuchagua kwa utulivu binti mrembo wa kula nae nyama choma na kushushia na kinywaji.

Mwaka 2020/2021 wakati wa COVID-19 meya bwana Blasio alipiga marufuku hii event na kukawa kumepooza mnoo.

Ila hii ni kama ile Carnival ya UK lazima shaba au mtu apigwe kameme (lugha ya mitaani).

Uzuri wake weye waweka budget kiasi ya kula nyama choma na ingine ya kusindikizwa na totoz yoyote.

Huwa inakuwa easy sana.
 
15 January 2026

Trump akazia viza majirani wote wa Kenya​

trump-sera-1320x792.jpg

Rais wa Amerika Donald Trump ambaye nyingi ya sera zake zinakabiliwa na maswali ya ufanisi. Picha|Maktaba

Utawala wa Rais wa Ameria Donald Trump unasitisha uchakataji wa viza za uhamiaji kwa raia kutoka nchi 75, msemaji wa Wizara ya Masuala ya Kigeni alisema Jumatano, kama sehemu ya hatua kali zinazoendelea za kudhibiti uhamiaji.

Hatua hiyo inafanya Kenya kuwa nchi ya pekee kutoka Afrika Mashariki na upembe wa Afrika ambayo raia wake watapata viza kuingia Amerika.

Raia wa nchi za Amerika Kusini zikiwemo Brazil, Colombia na Uruguay, nchi za Balkan kama Bosnia na Albania, nchi za Asia Kusini, Pakistan na Bangladesh, pamoja na mataifa mengi barani Afrika, Mashariki ya Kati na Caribean, hawatapata viza za kuzuru Amerika Januari 21, alisema msemaji huyo.


Barua wa Wizara ya Masuala ya Kigeni uliotangaza hatua hiyo na kuonekana na Reuters ulisema idara hiyo inaendesha “mapitio kamili” ya sera, kanuni na miongozo yote ili kuhakikisha “kiwango cha juu zaidi cha uchunguzi na uhakiki” kwa waombaji wote wa viza za Amerika.

Barua hiyo, iliyotumwa kwa balozi za Amerika nje ya nchi, ulisema kuna viashiria kwamba raia kutoka nchi hizo wamekuwa wakitafuta msaada wa kijamii nchini Amerika.

“Waombaji kutoka nchi hizi wako katika hatari kubwa ya kuwa mzigo kwa umma na kutegemea rasilmali za serikali za mitaa, majimbo na serikali ya shirikisho nchini Amerika,” ilisema barua hiyo.


Hatua hiyo, iliyoripotiwa kwa mara ya kwanza na Fox News, haiathiri viza za wageni, ambazo zimekuwa zikivutia uangalizi mkubwa hasa ikizingatiwa kuwa Amerika itaandaa Kombe la Dunia la 2026 na Olimpiki za 2028.

Uamuzi huo unafuatia agizo la Novemba lililowaelekeza mabalozi wa Amerika kuhakikisha kuwa waombaji wa viza wana uwezo wa kujitegemea kifedha na hawako katika hatari ya kutegemea ruzuku za serikali wakati wa kukaa kwao Amerika, kulingana na barua ya Wizara ya Masuala ya Kigeni.

“Wizara itatumia mamlaka yake ya muda mrefu kutangaza wasio na sifa wahamiaji wanaoweza kuwa mzigo kwa umma kwa Amerika na kutumia vibaya ukarimu wa wananchi wa Amerika,” alisema Tommy Pigott, Naibu Msemaji Mkuu wa Wizara ya Masuala ya Kigeni.

“Uchakataji wa viza za uhamiaji kutoka nchi hizi 75 utasitishwa wakati Wizara ya Masuala ya Kigeni inapopitia upya taratibu za uhamiaji ili kuzuia kuingia kwa raia wa kigeni watakaotegemea ustawi na manufaa ya umma,” aliongeza..
 
15 January 2026

Trump akazia viza majirani wote wa Kenya​

trump-sera-1320x792.jpg

Rais wa Amerika Donald Trump ambaye nyingi ya sera zake zinakabiliwa na maswali ya ufanisi. Picha|Maktaba

Utawala wa Rais wa Ameria Donald Trump unasitisha uchakataji wa viza za uhamiaji kwa raia kutoka nchi 75, msemaji wa Wizara ya Masuala ya Kigeni alisema Jumatano, kama sehemu ya hatua kali zinazoendelea za kudhibiti uhamiaji.

Hatua hiyo inafanya Kenya kuwa nchi ya pekee kutoka Afrika Mashariki na upembe wa Afrika ambayo raia wake watapata viza kuingia Amerika.

Raia wa nchi za Amerika Kusini zikiwemo Brazil, Colombia na Uruguay, nchi za Balkan kama Bosnia na Albania, nchi za Asia Kusini, Pakistan na Bangladesh, pamoja na mataifa mengi barani Afrika, Mashariki ya Kati na Caribean, hawatapata viza za kuzuru Amerika Januari 21, alisema msemaji huyo.


Barua wa Wizara ya Masuala ya Kigeni uliotangaza hatua hiyo na kuonekana na Reuters ulisema idara hiyo inaendesha “mapitio kamili” ya sera, kanuni na miongozo yote ili kuhakikisha “kiwango cha juu zaidi cha uchunguzi na uhakiki” kwa waombaji wote wa viza za Amerika.

Barua hiyo, iliyotumwa kwa balozi za Amerika nje ya nchi, ulisema kuna viashiria kwamba raia kutoka nchi hizo wamekuwa wakitafuta msaada wa kijamii nchini Amerika.

“Waombaji kutoka nchi hizi wako katika hatari kubwa ya kuwa mzigo kwa umma na kutegemea rasilmali za serikali za mitaa, majimbo na serikali ya shirikisho nchini Amerika,” ilisema barua hiyo.


Hatua hiyo, iliyoripotiwa kwa mara ya kwanza na Fox News, haiathiri viza za wageni, ambazo zimekuwa zikivutia uangalizi mkubwa hasa ikizingatiwa kuwa Amerika itaandaa Kombe la Dunia la 2026 na Olimpiki za 2028.

Uamuzi huo unafuatia agizo la Novemba lililowaelekeza mabalozi wa Amerika kuhakikisha kuwa waombaji wa viza wana uwezo wa kujitegemea kifedha na hawako katika hatari ya kutegemea ruzuku za serikali wakati wa kukaa kwao Amerika, kulingana na barua ya Wizara ya Masuala ya Kigeni.

“Wizara itatumia mamlaka yake ya muda mrefu kutangaza wasio na sifa wahamiaji wanaoweza kuwa mzigo kwa umma kwa Amerika na kutumia vibaya ukarimu wa wananchi wa Amerika,” alisema Tommy Pigott, Naibu Msemaji Mkuu wa Wizara ya Masuala ya Kigeni.

“Uchakataji wa viza za uhamiaji kutoka nchi hizi 75 utasitishwa wakati Wizara ya Masuala ya Kigeni inapopitia upya taratibu za uhamiaji ili kuzuia kuingia kwa raia wa kigeni watakaotegemea ustawi na manufaa ya umma,” aliongeza..
There’s ulterior motive behind every move that Trump makes. Just like Kenya, DRC and Burundi aren’t affected by this suspension!
 
utashangaa watu wanaumia wakati China, Korea kaskazini na Russia bado wapo
 
Racist Trump kishasema anataka immigrants from Norway,Denmark or somewhere Europe sio third world shithole countries,in short only whites no blacks
 
I wish watu waache kuiona US is like heaven, bongo unaweza kutoboa pia na ukaishi high quality life kuliko US, nimekaa US more than 20 years
Ahhh si kila mmoja anaweza toboa, yes US wako mbele kiuchumi, kwa fursa, just tu kuvioata hivyo you wilk have to fight alot

Kuna sababu why mamilion ya watu kutoka nchi masikini bado mpaka leo wana attempt kuingia Us
 
Ahhh si kila mmoja anaweza toboa, yes US wako mbele kiuchumi, kwa fursa, just tu kuvioata hivyo you wilk have to fight alot

Kuna sababu why mamilion ya watu kutoka nchi masikini bado mpaka leo wana attempt kuingia Us
Boss US sio rahisi kama wengi wanavyofikiria, majumba makubwa na SUVs yanawadanganya wengi kwenye TV, reality ingia ground utaelewa, nakuhakikishia kwa bongo mwenye mshahara wa dollar 1000 ni tajiri kuliko mshahara wa dollar 10,000 marekani
 
Boss US sio rahisi kama wengi wanavyofikiria, majumba makubwa na SUVs yanawadanganya wengi kwenye TV, reality ingia ground utaelewa, nakuhakikishia kwa bongo mwenye mshahara wa dollar 1000 ni tajiri kuliko mshahara wa dollar 10,000 marekani
It depends on one’s lifestyle!
 
Kifupi huyo mwanafunzi kapata visa kwa sababu wanafunzi hawatumii immigrant visa (hii iliyositishwa), wanatumia Non-Immigrant visa, ambayo haijasitishwa.

Ukisoma hiyo taarifa kwenye link post ya kwanza hapo juu utaona wameandika hivi.

"The suspension, which will begin Jan. 21, will not apply to applicants seeking non-immigrant visas, or temporary tourist or business visas, who make up the vast majority of visa seekers. Demand for non-immigrant visas is expected to rise dramatically in the coming months and years due to the upcoming 2026 World Cup and 2028 Olympics both of which the U.S. will host or co-host."

Kirefu.

Visa ya US ina aina nyingi, lakini ina aina kubwa mbili. Immigrant Visa na Non Immigrant Visa.

Tuanze na Immigrant Visa.

Hii ni visa ya watu wanaohamia kabisa US, wanasema wanataka kwenda kuweka makazi kabisa huko bila ya kuwa na mpango wa kurudi kimoja nchi walikotoka. Mfano mtu anayepata Green Card kwa lottery na kuamua kuishi Marekani, au mtu anayeoa au kuolewa na Mmarekani na kuamua kufanya makazi Marekani kimoja.

Hiyo inaitwa Immigrant Visa.

Kwa kuelewa kirahisi, Immigrant Visa ni ile inayoitwa Green Card.

Halafu kuna aina kubwa ya visa nyingine. Non-Immigrant Visa.

Hii ni kwa mtu anayesema anataka kwenda Marekani kwa kipindi fulani halafu atarudi nchini mwake. Watu wengi wanaoenda Marekani ndiyo wanatumia hii Non Immigrant visa. Hii inajumuisha visa za wanafunzi, watalii, wafanyabiashara na watu wengine wote ambao wanapata visa ya kwenda Marekani, kufanya shughuli zao, na kisha kurudi kwao, kwa mfano Tanzania.

Sasa Marekani ilisema imesitisha utoaji wa Immigrant Visa (Green Card). Wanadai kuwa wahamiaji wengi wanapata hizi visa halafu wanakuwa tegemezi kwa serikali. Serikali ya Marekani ya sasa inataka kuondoa utegemezi huu.Na ukiipata hii visa kwa namna fulani serikali ina wajibu fulani kukusaidia.

Mtu anayeenda kusoma anatumia student visa ambayo ni Non-Immigrant visa, si Green Card, si Immigrant Visa.

Hiyo inamaanisha mtu anayeomba Non-Immigrant Visa kwenda kusoma Princeton, suala la serikali ya US kusitisha utoaji wa Immigrant Visa halitamhusu.

Hata wewe ukitaka kuja kusoma, kutalii, kufanya biashara, kinsingi Marekani visa ya Non-Immigrant bado wanatoa, ila masharti yao ni magumu kama unavyowajua kila siku.

Ndiyo maana aliyeenda kusoma Princeton kapata visa bila tatizo.

Kwa sababu yeye anaomba Non-Immigrant Visa, si Immigrant visa (Green Card).

Huyu anayeenda kusoma zake Princeton (bonge la shule by the way, nilikwenda kutembea hapo miaka mingi sana wakati naangalia vyuo vya kusoma, hongera zake) huyu mambo ya Immigrant Visa hayamhusu, yeye anatafuta Non Immigrant Visa, hususan student visa.
Ufafanuzi mzuri mkuu!
👍
 
10 grand sounds good until reality checks in ,Kwa West/east Coast hiyo ni pocket change money,rent alone humbles you
Lifestyle is a big factor. Kuna watu wanaishi NYC au LA lakini income yao ni nusu (au pungufu ya nusu) ya hiyo pocket change. Hata Dar, kuna maeneo $1,000 haotoshi hata kulipia monthly rent!
 
Back
Top Bottom