Heche: Chadema Mwenyekiti wake ni Mbowe, akanusha kuwepo kambi ya Lissu na Mwenyekiti

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,447
7,830
1685606744251.png

John Heche

Akiwa kwenye mjadala wasafi fm, John Heche amekanusha uvumi aliolizwa na mwandishi kuhusu kuwepo kambi mbili ndani ya Chadema huku yeye Heche akiwa kambi ya Tundu Lissu.

Heche amesema mara ya kwanza kuingia kikao cha kamati kuu ilikuwa 2011 na alikuta mjadala wa fedha unajadiliwa, Heche anasema jinsi watu walivyokuwa wanavutana alijua ndio siku ya chama kupasuka ambapo Dk. Slaa alibananishwa na kina Mabere Marando na prof. Baregu.

Heche amesema hawawezi kuwa na uongozi ambao hauwezi kuhojiwa.

Kuhusu Mbowe kuwa mwenyekiti muda mrefu(miaka 19), amesema ni jambo zuri akiachia mtu mwingine lakini wanaoongea hivyo wachukue fomu, hawawezi kumuondoa mwenyekiti na chama kibaki bila mwenyekiti.
 
Uvumi hakuna kambi
Uzushi kambi zipo
Ukweli Mbowe aachie ngazi tu, na haya yote yatapotea
Piiiiipoz....Uvumi na Uzushi.


Ukweli utabakia...True Democracy
 
Hawa viongozi wa siasa wamekuwa wakifikiri kwamba bado kuna watz ambao ni mazuzu wa kuendelea kuwadanganya na kuwahadaa kama miaka ile.

Mwaka 2015, wakati mh Lowassa alipokatwa makusudi na CCM tetesi zilianza kuvuma kuwa mheshimiwa huyo anajiandaa kukimbilia katika chama kimoja wapo cha upinzani kati ya ACT Wazalendo au Chadema.

Ghafla viongozi wa Chadema hivi hivi mfano wa Heche wakajitokeza na kuanza kupinga kwa kuwatoa hofu wanachama wao kuwa Chama hicho hakiwezi kufanya kosa hilo la karne la kumkaribisha fisadi Lowassa ndani ya chama chao, na kwamba kama akihamia upinzani basi ataenda ACT Wazalendo ambacho ni chama alichokianzisha mwenyewe ili akikatwa akimbilie huko.

Muda ni mwl mzuri, baada ya muda mheshimiwa akamwaga mkwanja kupitia mlango wa uwani wa mwenyekiti na genge lake.

After that kila mtu anakumbuka kilichotokea na wale wote waliopinga tetesi hawakujitokeza kukanusha tena walichokipinga 🤣🤣🤣🤣

Siasa za Tanzania bila unafiki kwa kweli haziendi maana wajinga na wadanganyika ni wengi mno kuliko wajanja.
 
Hata ujio wa Lowasa kina Heche walikuwa hawajui lolote wakawa wanakenua meno tu kukanusha uvumi.

Kiufupi Heche ni kidagaa tu kama walivyo machadema wengi
 
Akiondoka Mbowe, Chama kitakuwa kama CUF,
CUF ikoje tena? 😇 Abakie ataona nnyewe
serikali ya CCM imejaribu sana ikiwemo kumbambika kesi ya ugaidi imeshindwa,
Kabrasha lipo, ni suala la muda tu? hatahivyo Mabakuli yalianza kukakuka tuu....ilikuwa mbinde!
njia rahisi ni kuwachochea wanachama Wadai uenyekiti.
Unafikiri anaitwa na kuonyesha ana Udikteta kwa kuchafuliwa tu? Wala sihitaji kutaja miaka yake tangu autwae/apewe Uenyekiti....Lissu akamatie hapo hapo, na wanaharakati wengine wa CHADEMA waendelee vivyohivyo, Wananchi wataamua na wanachama wao watashikwa na butwaa tuu.
 
Vyama vichanga hulelewa. Nyerere alikuwa mwenyekiti kwa miaka 23. Chadema isifange kosa kumuondoa mbowe kwenye uenyekiti kwa kusikiliza makelele ya ccm.
Kwa chama kinachotumia maharamia kuzima Legacy ya Nyerere, sidhani kama wana uhalali wa kumtaja taja kuhalalisha uwepo wa Mbowe madarakani, yaani hayo ni matusi kwa Baba wa Taifa.

Nyerere aliongoza Nchi.

Mbowe anaongoza Chama tu!

CHADEMA, kumbeza Nyerere kwa kuua siasa zake wako maradufu sana halafu wanageuka na kumuenzi kutafuta kutumia nguvu yake kwa manufaa ya kibinafsi, hio sio sawa.
 

Akiwa kwenye mjadala wasafi fm, John Heche amekanusha uvumi aliolizwa na mwandishi kuhusu kuwepo kambi mbili ndani ya Chadema huku yeye Heche akiwa kambi ya Tundu Lissu.

Heche amesema mara ya kwanza kuingia kikao cha kamati kuu ilikuwa 2011 na alikuta mjadala wa fedha unajadili, Heche anasema jinsi watu walivyokuwa wanavuta alijua ndio siku ya chama kupasuka ambapo Dk. Slaa alibananishwa na kina Mabere Marando na prof. Baregu.

Heche amesema hawawezi kuwa na uongozi ambao hauwezi kuhojiwa.

Kuhusu Mbowe kuwa mwenyekiti muda mrefu(miaka 19), amesema ni jambo zuri akiachia mtu mwingine lakini wanaoongea hivyo wachukue fomu, hawawezi kumuondoa mwenyekiti na chama kibaki bila mwenyekiti.
Wenye kuona mbali tulikuwa tunajua Lissu na Mbowe hawawezi kugombana wala kugombanishwa !!
 

Akiwa kwenye mjadala wasafi fm, John Heche amekanusha uvumi aliolizwa na mwandishi kuhusu kuwepo kambi mbili ndani ya Chadema huku yeye Heche akiwa kambi ya Tundu Lissu.

Heche amesema mara ya kwanza kuingia kikao cha kamati kuu ilikuwa 2011 na alikuta mjadala wa fedha unajadili, Heche anasema jinsi watu walivyokuwa wanavuta alijua ndio siku ya chama kupasuka ambapo Dk. Slaa alibananishwa na kina Mabere Marando na prof. Baregu.

Heche amesema hawawezi kuwa na uongozi ambao hauwezi kuhojiwa.

Kuhusu Mbowe kuwa mwenyekiti muda mrefu(miaka 19), amesema ni jambo zuri akiachia mtu mwingine lakini wanaoongea hivyo wachukue fomu, hawawezi kumuondoa mwenyekiti na chama kibaki bila mwenyekiti.
To be honest Mbowe bado anatakiwa kuongoza chama hili kubwa.
Ukubwa wa chama, mikakati ya chama, na mahali chama kilipo, bado tunamuitaji Mbowe.
 
Uvumi hakuna kambi
Uzushi kambi zipo
Ukweli Mbowe aachie ngazi tu, na haya yote yatapotea
Piiiiipoz....Uvumi na Uzushi.


Ukweli utabakia...True Democracy
Kama unautaka uenyeakiti wa CHADEMA, ukifika wakati wa uchaguzi, nenda ukajaze fomu. Lakini ufahamu uongozi kwenye vyama vya upinzani ni tiketi ya kwenda jela wakati wowote, kubambikiwa kesi, kufilisiwa, na wakati mwingine hata kuuawa.

Afadhali CHADEMA huwa wana uchaguzi wa kumchagua mwenyekiti, kuliko CCM ambako wanachama wamenyimwa haki ya kumchagua mwenyekiti, eti aliyetangazwa na tume kuwa Rais, ndiye automatically ni mwenyekiti wa CCM..
 
Hawa viongozi wa siasa wamekuwa wakifikiri kwamba bado kuna watz ambao ni mazuzu wa kuendelea kuwadanganya na kuwahadaa kama miaka ile.

Mwaka 2015, wakati mh Lowassa alipokatwa makusudi na CCM tetesi zilianza kuvuma kuwa mheshimiwa huyo anajiandaa kukimbilia katika chama kimoja wapo cha upinzani kati ya ACT Wazalendo au Chadema.

Ghafla viongozi wa Chadema hivi hivi mfano wa Heche wakajitokeza na kuanza kupinga kwa kuwatoa hofu wanachama wao kuwa Chama hicho hakiwezi kufanya kosa hilo la karne la kumkaribisha fisadi Lowassa ndani ya chama chao, na kwamba kama akihamia upinzani basi ataenda ACT Wazalendo ambacho ni chama alichokianzisha mwenyewe ili akikatwa akimbilie huko.

Muda ni mwl mzuri, baada ya muda mheshimiwa akamwaga mkwanja kupitia mlango wa uwani wa mwenyekiti na genge lake.

After that kila mtu anakumbuka kilichotokea na wale wote waliopinga tetesi hawakujitokeza kukanusha tena walichokipinga

Siasa za Tanzania bila unafiki kwa kweli haziendi maana wajinga na wadanganyika ni wengi mno kuliko wajanja.

Kwa hiyo kuna mgogoro CHADEMA? Tusubirie mpaka lini ili kuthibitisha kuna mgogoro?
 
Back
Top Bottom