Hebu tujiulize undani wa hili ‘Tishio la UGAIDI’

Wengi wetu humu Tumeona, tunesikia na tumesoma tamko la Ubalozi wa Marekani kuhusu uwezekano wa kutokea shambulio la ugaidi hapa nchini.
View attachment 2497876

Tumesikia mwitikio wa jeshi la polisi kuhusu hatua wanazochukua dhidi ya tahadhari hiyo huku wakituhakikishia usalama na ulinzi. Lakini mimi nineona hapo kuna jambo la kutafakari kuhusu uwezo wetu katika usalama wa ndani ya nchi yetu sambamba na uhusiano wa dola na wananchi.

Iwapo taifa la nje linaweza kuchunguza na kupata uthibitisho wa kuwepo na tishio la usalama nchini na wakatoa tahadhari maana yake kuna kulegalega na kuzembea kwa vyombo vyetu vya ulinzi hususani espionage ya ndani ya nchi.

Serikali ya Tanzania imeeza kupitia viongozi waandamizi kuhusu uwekezaji mkubwa walioufanya katika kununua mitambo ya kudukua mawasiliano ya mitandaoni hususani ikiwalenga wahalifu wa mitandaoni. Hapo awali nilisema kuwa tambo za serikali zinathibitisha kuhusu kuingilia uhuru wa wananchi wake binafsi kwa sababu mifano ya waliochukuliwa hatua hata kufikishwa mahakamani ni wale waliotuhumiwa kutoa kauli ama maneno ya kuudhi dhidi ya watawala. Hatujawahi kuona ama kusikia wahalifu ambao wanafanikisha matukio ya kihalifu ama wanaotoa matishio ya usalama wetu wa ndani waking'amuliwa ama kuchukuliwa hatua.

Marekani kupitia taasisi zake za nje wamejijengea uwezo wa kuwez kupenya vihunzi vya usalama vya makundi ya kiuhalifu dhidi ya binadamu na wakaweza kutambua mipango yao na kwa nia njema kabisa wametoa tahadhari.

Watanzania wenzangu nyie ni mashahidi wa namna ambavyo serikali yetu chini ya mkoloni mweusi CCM inavyotushughulikia raia wake huku ikivunja katiba inayotoa uhuru wa maoni. Ushshidi wa hili ni namna ambavyo asilimia kubwa ya members wa JamiiForums tunatumia pen names au majina bandia ili kuficha utambulisho wetu kwa sababu ya kuhofia vyombo vya dola ambavyo vimekuwa vikitumia kodi zetu kutufanyia uhalifu badala ya kutimiza wajibu wake muhimu wa kikatiba na kisheria.

Wachache wetu tunafahamu kinachoendelea maeneo ya mpakani mwa Tanzania na Msumbiji pamoja na juhudi kubwa sa serikali kudhibiti utoaji wa taarifa kwa umma. Ndugu zetu wanauawa na magaidi ambao wamejikita kaskazini mwa Msumbiji. Wahalifu hao inasemekana ni wale magaidi waliofurushwa Kibiti na Rufiji hivyo wameamua kuweka base eneo ambalo wanaamini watajiimarisha na kurudi nchini kuleta tafrani.

Tishio la ugaidi kama lilivyotolewa na ubalozi wa Marekani ni wazi kwamba hatupo salama kwa sababu taarifa ya awali ilipaswa kutolewa na vyombo vyetu na kuchukua tahadhari zote.

Tunahitaji kuona vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vikitimiza wajibu wao muhimu kisheria na kikatiba kwa kutuhakikishia usalama wetu wa ndani kwa sababu uwepo wao ni muhimu kwetu na si kwa viongozi pekee.

Tufike mahala tuangalie kwa uwiano bajeti ya ulinzi wa viongozi na bajeti ya ulinzi wa umma ili kutenda yatupasayo na si kuelemea eneo moja pekee huku nchi ikiwa ktk hekaheka na matishio ya usalama

TUSIJEKUPUUZA HILI TISHIO..
Mkuu juzi tu tunaskia mzee kaua watu zaidi ya kumi huko US.
Ni kweli Tanzania tuko ovyo lakin taarifa za intelligence polisi, jw au tiss sio za kuweka public hata kama wanajua tena za ugaidi.
Kama wametangaza kwanini wasipambane kuzuia waje wakutangazie wewe kuna tishio?
US anachofanya ni kwa ajili ya raia wake hapa Ila sio kuisaidia tz
 
Mkuu juzi tu tunaskia mzee kaua watu zaidi ya kumi huko US.
Ni kweli Tanzania tuko ovyo lakin taarifa za intelligence polisi, jw au tiss sio za kuweka public hata kama wanajua tena za ugaidi.
Kama wametangaza kwanini wasipambane kuzuia waje wakutangazie wewe kuna tishio?
US anachofanya ni kwa ajili ya raia wake hapa Ila sio kuisaidia tz
Wajuzi wa masuala ya usalama wakikusoma hapa hawatoondoa shaka yao kwamba vyombo vyetu vya dola vinawatumia raia kama ngao.

Elewa nilichoandika lakini
 
Wajuzi wa masuala ya usalama wakikusoma hapa hawatoondoa shaka yao kwamba vyombo vyetu vya dola vinawatumia raia kama ngao.

Elewa nilichoandika lakini
Hakuna ulicho andika...
Ujuaji tu mimi nimekaa na hao ma MI naelewa sana kuhusu haya mamb o ya ugaidi.
Lengo la ugaidi ni kutengeneza hofu, kui-sabotage serikali na kupata publicity unapotanganza kwa raia kunatishio umeshafanikisha lengo lao la kwanza hofu, kama umefuatilia huko marekani na ulaya wasomi wengi akiwemo prof Jordan Peterson wa chuo cha canada wanataka hizo taarifa za watu kuwashambulia watu wengine zisiwe zinatangazwa kwa sababu hyo ni moja ya motive ya hao watu.
Unless kama wewe ni mtu wa intelligence unajua zaidi
 
Wengi wetu humu Tumeona, tunesikia na tumesoma tamko la Ubalozi wa Marekani kuhusu uwezekano wa kutokea shambulio la ugaidi hapa nchini.
View attachment 2497876

Tumesikia mwitikio wa jeshi la polisi kuhusu hatua wanazochukua dhidi ya tahadhari hiyo huku wakituhakikishia usalama na ulinzi. Lakini mimi nineona hapo kuna jambo la kutafakari kuhusu uwezo wetu katika usalama wa ndani ya nchi yetu sambamba na uhusiano wa dola na wananchi.

Iwapo taifa la nje linaweza kuchunguza na kupata uthibitisho wa kuwepo na tishio la usalama nchini na wakatoa tahadhari maana yake kuna kulegalega na kuzembea kwa vyombo vyetu vya ulinzi hususani espionage ya ndani ya nchi.

Serikali ya Tanzania imeeza kupitia viongozi waandamizi kuhusu uwekezaji mkubwa walioufanya katika kununua mitambo ya kudukua mawasiliano ya mitandaoni hususani ikiwalenga wahalifu wa mitandaoni. Hapo awali nilisema kuwa tambo za serikali zinathibitisha kuhusu kuingilia uhuru wa wananchi wake binafsi kwa sababu mifano ya waliochukuliwa hatua hata kufikishwa mahakamani ni wale waliotuhumiwa kutoa kauli ama maneno ya kuudhi dhidi ya watawala. Hatujawahi kuona ama kusikia wahalifu ambao wanafanikisha matukio ya kihalifu ama wanaotoa matishio ya usalama wetu wa ndani waking'amuliwa ama kuchukuliwa hatua.

Marekani kupitia taasisi zake za nje wamejijengea uwezo wa kuwez kupenya vihunzi vya usalama vya makundi ya kiuhalifu dhidi ya binadamu na wakaweza kutambua mipango yao na kwa nia njema kabisa wametoa tahadhari.

Watanzania wenzangu nyie ni mashahidi wa namna ambavyo serikali yetu chini ya mkoloni mweusi CCM inavyotushughulikia raia wake huku ikivunja katiba inayotoa uhuru wa maoni. Ushshidi wa hili ni namna ambavyo asilimia kubwa ya members wa JamiiForums tunatumia pen names au majina bandia ili kuficha utambulisho wetu kwa sababu ya kuhofia vyombo vya dola ambavyo vimekuwa vikitumia kodi zetu kutufanyia uhalifu badala ya kutimiza wajibu wake muhimu wa kikatiba na kisheria.

Wachache wetu tunafahamu kinachoendelea maeneo ya mpakani mwa Tanzania na Msumbiji pamoja na juhudi kubwa sa serikali kudhibiti utoaji wa taarifa kwa umma. Ndugu zetu wanauawa na magaidi ambao wamejikita kaskazini mwa Msumbiji. Wahalifu hao inasemekana ni wale magaidi waliofurushwa Kibiti na Rufiji hivyo wameamua kuweka base eneo ambalo wanaamini watajiimarisha na kurudi nchini kuleta tafrani.

Tishio la ugaidi kama lilivyotolewa na ubalozi wa Marekani ni wazi kwamba hatupo salama kwa sababu taarifa ya awali ilipaswa kutolewa na vyombo vyetu na kuchukua tahadhari zote.

Tunahitaji kuona vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vikitimiza wajibu wao muhimu kisheria na kikatiba kwa kutuhakikishia usalama wetu wa ndani kwa sababu uwepo wao ni muhimu kwetu na si kwa viongozi pekee.

Tufike mahala tuangalie kwa uwiano bajeti ya ulinzi wa viongozi na bajeti ya ulinzi wa umma ili kutenda yatupasayo na si kuelemea eneo moja pekee huku nchi ikiwa ktk hekaheka na matishio ya usalama

TUSIJEKUPUUZA HILI TISHIO..

Izingatiwe security alert ya beberu imetolewa siku Lissu alipowasili, Chadema wakiwa wamepanga mfululizo wa mikutano ya hadhara pamoja naye.

Ikumbukwe wale waliowahi kusema kama risasi 16 hazikumwua, basi watamchoma sindano za sumu wangalipo.

Bwana Musiba na wenziwe waliokuwa wakiyasema hadharani kuhusu kumdhuru Lissu nao wangalipo.

Wasiojulikana na genge zima lililolukuwa area D siku Ile ya tukio nao wangalipo.

Nk, nk.

Inahitaji nini zaidi kufahamu wenye roho za kumwua mtu wanaweza kuwa watu wa namna gani? Kwamba ghafla wanaweza kuwa waliacha na kustaafu sasa?

Kwani ni lini walitubu, kuokoka au hata kuslimu ili kuutafuta wokovu wa mbinguni sasa?

Ikumbukwe mikutanoni Chadema wamewahi kushambuliwa kigaidi Arusha, bila kusahau risasi za moto kinondoni zilizoondoka na yule binti asiyekuwa na hatia.

Tishio lipo, Chadema wengine kutoimarisha ulinzi msilalie mlango wazi.
 
Hakuna ulicho andika...
Ujuaji tu mimi nimekaa na hao ma MI naelewa sana kuhusu haya mamb o ya ugaidi.
Lengo la ugaidi ni kutengeneza hofu, kui-sabotage serikali na kupata publicity unapotanganza kwa raia kunatishio umeshafanikisha lengo lao la kwanza hofu, kama umefuatilia huko marekani na ulaya wasomi wengi akiwemo prof Jordan Peterson wa chuo cha canada wanataka hizo taarifa za watu kuwashambulia watu wengine zisiwe zinatangazwa kwa sababu hyo ni moja ya motive ya hao watu.
Unless kama wewe ni mtu wa intelligence unajua zaidi
Mkuu
Mnachokifanya ni kuwafanya raia ni mbumbumbu.

Suala la usalama kuna taarifa zinapaswa kutolewa public na zingine za kufanyiakazi.

Uhalifu unapovuja inapaswa ijulikane ili kuwajengea hofu ama kuvuruga stance ya wahalifu.

Kufichaficha mambo ndo mulemule kuwajengea hofu raia
 
Mkuu
Mnachokifanya ni kuwafanya raia ni mbumbumbu.

Suala la usalama kuna taarifa zinapaswa kutolewa public na zingine za kufanyiakazi.

Uhalifu unapovuja inapaswa ijulikane ili kuwajengea hofu ama kuvuruga stance ya wahalifu.

Kufichaficha mambo ndo mulemule kuwajengea hofu raia
Mkuranga na Rufiji ulikuwa nchini!?
 
Izingatiwe security alert ya beberu imetolewa siku Lissu alipowasili Chadema wakiwa wamepanga mfululizo wa mikutano ya hadhara pamoja naye.

Ikumbukwe wale waliowahi kusema kama risasi 16 hazikumwua, basi watamchoma sindano ya sumu wangalipo.

Bwana Musiba na wenziwe waliokuwa wakiyasema hadharani kuhusu kumdhuru Lissu nao wangalipo.

Wasiojulikana na genge zima lililolukuwa area D siku Ile ya tukio nao wangalipo.

Nk, nk.

Inahitaji nini zaidi kufahamu wenye roho za kumwua mtu wanaweza kuwa watu wa namna gani au wanaweza kuacha au kustaafu lini?

Kwani wauwaji wale au hawa wengine ni lini walitubu, kuokoka au kuslimu kuutafuta wokovu wa mbinguni?

Ikumbukwe mikutanoni Chadema wamewahi kushambuliwa kigaidi Arusha bila kusahau risasi za moto kinondoni.

Tishio lipo Chadema hapana kulala mlango wazi.
At least umeweka point inayoleta tafakuri.
 
Itumie hiyo kama case study yako katika mambo ya ugaidi
Kupuuzwa kwa securiry alerts ndo msingi mkuu.

Siasa za kipuuzi ambazo zinawabebesha walinzi wetu majukumu yasiyo yao ni msingi mwingine.

Yapo mengi yaliyopelekea hali ile kwa sababu uvamizi wa vituo vya polisi na kuteka silaha ulifanyika mfululizo na hakukuwepo na hatua thabiti zaidi ya vitisho vya kuwachukulia hatua wahalifu....

Polisi baadhi wanashirikiana na wahalifu na hili lipo ndani yao lakini wanachukulia.kama diplomasia rafiki.

Mkuu kuna mambo tukiyasema hapa tutakumbusha machungu na madhila mengi
 
Marekani wakati mwingine ni kama abudu nondo, wanakualati kumbe wanafanya wenyewe.

October 2020 kuelekea uchaguzi mkuu alert zao kuhusu Zanzibar zilikuwapo hivi hivi. Pana watu waliuliwa na kujeruhiwa sana tu kule.

Una mashaka kuwa wali alert na kufanyiza wao wao pia ndugu?
 
Kupuuzwa kwa securiry alerts ndo msingi mkuu.

Siasa za kipuuzi ambazo zinawabebesha walinzi wetu majukumu yasiyo yao ni msingi mwingine.

Yapo mengi yaliyopelekea hali ile kwa sababu uvamizi wa vituo vya polisi na kuteka silaha ulifanyika mfululizo na hakukuwepo na hatua thabiti zaidi ya vitisho vya kuwachukulia hatua wahalifu....

Polisi baadhi wanashirikiana na wahalifu na hili lipo ndani yao lakini wanachukulia.kama diplomasia rafiki.

Mkuu kuna mambo tukiyasema hapa tutakumbusha machungu na madhila mengi
Mkuu kama haujui mambo ya intelligence bora usiyagusie.
Unajua jinsi gani wnakusanya hizo taarifa za intelligence, jinsi wanavyozichambua na jinsi wanavyozishughulikia!?
 
Ninakazia:

"Tishio lipo, Chadema wengine kutoimarisha ulinzi msilalie mlango wazi."
Inawezekana tamko limelenga kuzungumzia jambo kama hili maana kwa mwenendo wa wasaidizi wa Hangaya ni kama wana mpango wa kumharibia mama apoteze uungwaji mkono na raia wake.

Hivyo kulegalega kwa usalama inawezekana ni eneo la kimkakati pia.

CHADEMA wachukue tahadhari kwa sababu wahafidhina wa CCM wamechafukwa kuona siasa inaendeshwa kwa ufasaha sasa
 
Security alert sio ya kuipuuzia...

Pia ni lazima itolewe hata wapangaji wakiiona wanajua wameshang'amuliwa
 
Back
Top Bottom