Hebu tujiulize undani wa hili ‘Tishio la UGAIDI’

Hakuna chochote Cha maaana kaona isipokuwa makomandoo wa Marekani wamemuua kiongozi wa IS hapo Somalia. Wanachofanya ni kujihami maana wanajua Islamic state Wana wafuasi sehemu nyingi na hapa ni karibu Sana na Somalia lolote linaweza kutokea.

Sent from my CPH1923 using JamiiForums mobile app
Inawezekana wewe umeweza kuweka kidole sahihi kwenye hili jambo.

Ni kama Mmarekani anajihami, kutokana na aliyotenda karibuni. Ni mbinu ya kuwaogopesha hata waliofikiri wanaweza kulipa kisasi kwa tendo lililofanyika Somalia.
 
Inawezekana wewe umeweza kuweka kidole sahihi kwenye hili jambo.

Ni kama Mmarekani anajihami, kutokana na aliyotenda karibuni. Ni mbinu ya kuwaogopesha hata waliofikiri wanaweza kulipa kisasi kwa tendo lililofanyika Somalia.
Na ndiyo hiko hivyo mkuu. Marekani anajihami kwa alichofanya hapo Somalia.

Wale jamaa Wana wafuasi karibia kila sehemu hapa Africa na Tz ikiwemo. Lolote laweza kutokea.
 
Wengi wetu humu Tumeona, tunesikia na tumesoma tamko la Ubalozi wa Marekani kuhusu uwezekano wa kutokea shambulio la ugaidi hapa nchini.
View attachment 2497876

Tumesikia mwitikio wa jeshi la polisi kuhusu hatua wanazochukua dhidi ya tahadhari hiyo huku wakituhakikishia usalama na ulinzi. Lakini mimi nineona hapo kuna jambo la kutafakari kuhusu uwezo wetu katika usalama wa ndani ya nchi yetu sambamba na uhusiano wa dola na wananchi.

Iwapo taifa la nje linaweza kuchunguza na kupata uthibitisho wa kuwepo na tishio la usalama nchini na wakatoa tahadhari maana yake kuna kulegalega na kuzembea kwa vyombo vyetu vya ulinzi hususani espionage ya ndani ya nchi.

Serikali ya Tanzania imeeza kupitia viongozi waandamizi kuhusu uwekezaji mkubwa walioufanya katika kununua mitambo ya kudukua mawasiliano ya mitandaoni hususani ikiwalenga wahalifu wa mitandaoni. Hapo awali nilisema kuwa tambo za serikali zinathibitisha kuhusu kuingilia uhuru wa wananchi wake binafsi kwa sababu mifano ya waliochukuliwa hatua hata kufikishwa mahakamani ni wale waliotuhumiwa kutoa kauli ama maneno ya kuudhi dhidi ya watawala. Hatujawahi kuona ama kusikia wahalifu ambao wanafanikisha matukio ya kihalifu ama wanaotoa matishio ya usalama wetu wa ndani waking'amuliwa ama kuchukuliwa hatua.

Marekani kupitia taasisi zake za nje wamejijengea uwezo wa kuwez kupenya vihunzi vya usalama vya makundi ya kiuhalifu dhidi ya binadamu na wakaweza kutambua mipango yao na kwa nia njema kabisa wametoa tahadhari.

Watanzania wenzangu nyie ni mashahidi wa namna ambavyo serikali yetu chini ya mkoloni mweusi CCM inavyotushughulikia raia wake huku ikivunja katiba inayotoa uhuru wa maoni. Ushshidi wa hili ni namna ambavyo asilimia kubwa ya members wa JamiiForums tunatumia pen names au majina bandia ili kuficha utambulisho wetu kwa sababu ya kuhofia vyombo vya dola ambavyo vimekuwa vikitumia kodi zetu kutufanyia uhalifu badala ya kutimiza wajibu wake muhimu wa kikatiba na kisheria.

Wachache wetu tunafahamu kinachoendelea maeneo ya mpakani mwa Tanzania na Msumbiji pamoja na juhudi kubwa sa serikali kudhibiti utoaji wa taarifa kwa umma. Ndugu zetu wanauawa na magaidi ambao wamejikita kaskazini mwa Msumbiji. Wahalifu hao inasemekana ni wale magaidi waliofurushwa Kibiti na Rufiji hivyo wameamua kuweka base eneo ambalo wanaamini watajiimarisha na kurudi nchini kuleta tafrani.

Tishio la ugaidi kama lilivyotolewa na ubalozi wa Marekani ni wazi kwamba hatupo salama kwa sababu taarifa ya awali ilipaswa kutolewa na vyombo vyetu na kuchukua tahadhari zote.

Tunahitaji kuona vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vikitimiza wajibu wao muhimu kisheria na kikatiba kwa kutuhakikishia usalama wetu wa ndani kwa sababu uwepo wao ni muhimu kwetu na si kwa viongozi pekee.

Tufike mahala tuangalie kwa uwiano bajeti ya ulinzi wa viongozi na bajeti ya ulinzi wa umma ili kutenda yatupasayo na si kuelemea eneo moja pekee huku nchi ikiwa ktk hekaheka na matishio ya usalama

TUSIJEKUPUUZA HILI TISHIO..
Yaani Jeshi linatumia magari chakavu huku kila siku viongozi wananunua magari ya bei mbaya ila hilo neno
BAJETI YA ULINZI WA VIONGOZI NA ULINZI WA UMMA OVER
 
Yaani Jeshi linatumia magari chakavu huku kila siku viongozi wananunua magari ya bei mbaya ila hilo neno
BAJETI YA ULINZI WA VIONGOZI NA ULINZI WA UMMA OVER
Polisi walipaswa kuwa na vishkwambi vyenye nyenzo muhimu za ulinzi. Unakuta polisi anatembea na bunduki na king'amuzi pekee alichonacho ni redio call.

Polisi wanapaswa kuwa na server yao pekee inayosimamia intranet zao.

Polisi wanapaswa kuwa na camcoder kwenye kofia zao ili kuratibu mwenendo wake n amatukio yanayoambatana na utendaji wake......
 
Polisi walipaswa kuwa na vishkwambi vyenye nyenzo muhimu za ulinzi. Unakuta polisi anatembea na bunduki na king'amuzi pekee alichonacho ni redio call.

Polisi wanapaswa kuwa na server yao pekee inayosimamia intranet zao.

Polisi wanapaswa kuwa na camcoder kwenye kofia zao ili kuratibu mwenendo wake n amatukio yanayoambatana na utendaji wake......
Kwa bajeti ipi na viongozi gani wa kuwaza vitu Kama hivyo?
 
CCM inakosa dira nzuri na ubunifu wa kimkakati hilo ni tatizo.
Lakini tatizo lingine hakuna chama kingine chenyewe uwezo wa kuongoza kwa Tanzania kila mtu anaangalia maslahi
 
Wengi wetu humu Tumeona, tunesikia na tumesoma tamko la Ubalozi wa Marekani kuhusu uwezekano wa kutokea shambulio la ugaidi hapa nchini.
View attachment 2497876

Tumesikia mwitikio wa jeshi la polisi kuhusu hatua wanazochukua dhidi ya tahadhari hiyo huku wakituhakikishia usalama na ulinzi. Lakini mimi nineona hapo kuna jambo la kutafakari kuhusu uwezo wetu katika usalama wa ndani ya nchi yetu sambamba na uhusiano wa dola na wananchi.

Iwapo taifa la nje linaweza kuchunguza na kupata uthibitisho wa kuwepo na tishio la usalama nchini na wakatoa tahadhari maana yake kuna kulegalega na kuzembea kwa vyombo vyetu vya ulinzi hususani espionage ya ndani ya nchi.

Serikali ya Tanzania imeeza kupitia viongozi waandamizi kuhusu uwekezaji mkubwa walioufanya katika kununua mitambo ya kudukua mawasiliano ya mitandaoni hususani ikiwalenga wahalifu wa mitandaoni. Hapo awali nilisema kuwa tambo za serikali zinathibitisha kuhusu kuingilia uhuru wa wananchi wake binafsi kwa sababu mifano ya waliochukuliwa hatua hata kufikishwa mahakamani ni wale waliotuhumiwa kutoa kauli ama maneno ya kuudhi dhidi ya watawala. Hatujawahi kuona ama kusikia wahalifu ambao wanafanikisha matukio ya kihalifu ama wanaotoa matishio ya usalama wetu wa ndani waking'amuliwa ama kuchukuliwa hatua.

Marekani kupitia taasisi zake za nje wamejijengea uwezo wa kuwez kupenya vihunzi vya usalama vya makundi ya kiuhalifu dhidi ya binadamu na wakaweza kutambua mipango yao na kwa nia njema kabisa wametoa tahadhari.

Watanzania wenzangu nyie ni mashahidi wa namna ambavyo serikali yetu chini ya mkoloni mweusi CCM inavyotushughulikia raia wake huku ikivunja katiba inayotoa uhuru wa maoni. Ushshidi wa hili ni namna ambavyo asilimia kubwa ya members wa JamiiForums tunatumia pen names au majina bandia ili kuficha utambulisho wetu kwa sababu ya kuhofia vyombo vya dola ambavyo vimekuwa vikitumia kodi zetu kutufanyia uhalifu badala ya kutimiza wajibu wake muhimu wa kikatiba na kisheria.

Wachache wetu tunafahamu kinachoendelea maeneo ya mpakani mwa Tanzania na Msumbiji pamoja na juhudi kubwa sa serikali kudhibiti utoaji wa taarifa kwa umma. Ndugu zetu wanauawa na magaidi ambao wamejikita kaskazini mwa Msumbiji. Wahalifu hao inasemekana ni wale magaidi waliofurushwa Kibiti na Rufiji hivyo wameamua kuweka base eneo ambalo wanaamini watajiimarisha na kurudi nchini kuleta tafrani.

Tishio la ugaidi kama lilivyotolewa na ubalozi wa Marekani ni wazi kwamba hatupo salama kwa sababu taarifa ya awali ilipaswa kutolewa na vyombo vyetu na kuchukua tahadhari zote.

Tunahitaji kuona vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vikitimiza wajibu wao muhimu kisheria na kikatiba kwa kutuhakikishia usalama wetu wa ndani kwa sababu uwepo wao ni muhimu kwetu na si kwa viongozi pekee.

Tufike mahala tuangalie kwa uwiano bajeti ya ulinzi wa viongozi na bajeti ya ulinzi wa umma ili kutenda yatupasayo na si kuelemea eneo moja pekee huku nchi ikiwa ktk hekaheka na matishio ya usalama

TUSIJEKUPUUZA HILI TISHIO..
Vyombo vyetu vipo imara sana kupambana na vyama vya siasa.
 
Vyombo vyetu vipo imara sana kupambana na vyama vya siasa.
Mikakati na mbinu zote wameweka kupambana nanraia badala ya kupambana na uhalifu.

Magari ya washawasha yale hayajanunuliwa kwa ajili ya kukomesha uhalifu. Angalia wanawaambia vyama kuwa hawana polisi wa kutosha kulinda mikutano yao lakini wanapeleka full battalion ya polisi kuwatwanga hao wapinzani.

Double standards zinatufanya kuwa vulnerable
 
CCM inakosa dira nzuri na ubunifu wa kimkakati hilo ni tatizo.
Lakini tatizo lingine hakuna chama kingine chenyewe uwezo wa kuongoza kwa Tanzania kila mtu anaangalia maslahi
Mkuu
Kauli kusema kuwa hakuna chama kingine mbadala ni propaganda iliyoasisiwa na CCM ambapo tumekaririshwa kufananisha upinzani na CCM.

TANU haikuenda kusomea kuongoza nchi bali walidai uhuru ili tujitawale na kujiamulia hatima ya mambo yetu. Ni jukumu la CCM kuwawezesha watanzania kujitawala lakini badala yake imejimilikisha nchi. Imekuwa mkoloni mpya
 
Ubalozi kuna tishio la ugaidi, mkuu wa majeshi “Tanzania ni salama hakuna tishio la usalama “
So tushike lipi na tuache lipi??
Tumsikilize nani??
 
Mkuu
Kauli kusema kuwa hakuna chama kingine mbadala ni propaganda iliyoasisiwa na CCM ambapo tumekaririshwa kufananisha upinzani na CCM.

TANU haikuenda kusomea kuongoza nchi bali walidai uhuru ili tujitawale na kujiamulia hatima ya mambo yetu. Ni jukumu la CCM kuwawezesha watanzania kujitawala lakini badala yake imejimilikisha nchi. Imekuwa mkoloni mpya
Ok lakini kujitawala ni lazima kuwe na chama.
Ukiitoa CCM ambayo ni sahihi kabisa ina mapungufu unahisi chama gani kingine kina uwezo wa kuongoza nchi na kwanini?
 
Ok lakini kujitawala ni lazima kuwe na chama.
Ukiitoa CCM ambayo ni sahihi kabisa ina mapungufu unahisi chama gani kingine kina uwezo wa kuongoza nchi na kwanini?
Chama sahihi ni kile kitakacholeta ilani yenye mantiki na inayotoa muelekeo wa kulinasua taifa kutoka katika MNYONG'ONYO huu tulio nao sasa.

Watanzania wana uwezo wa kuunda serikali kupitia chama kitakachoshinda kihalali na siyo uzwazwa wa CCM
 
Chama sahihi ni kile kitakacholeta ilani yenye mantiki na inayotoa muelekeo wa kulinasua taifa kutoka katika MNYONG'ONYO huu tulio nao sasa.

Watanzania wana uwezo wa kuunda serikali kupitia chama kitakachoshinda kihalali na siyo uzwazwa wa CCM
Bado hujajibu swali
 
Chama sahihi ni kile kitakacholeta ilani yenye mantiki na inayotoa muelekeo wa kulinasua taifa kutoka katika MNYONG'ONYO huu tulio nao sasa.

Watanzania wana uwezo wa kuunda serikali kupitia chama kitakachoshinda kihalali na siyo uzwazwa wa CCM
Nadhani swali ungejibu kiutendaji na hoja zaidi kuliko siasa za porojo
 
Back
Top Bottom