Ms Judith
JF-Expert Member
- Dec 24, 2010
- 2,563
- 918
leo nimepata furaha kubwa sana. kuna mkaka mmoja aliwahi kuniapproach miaka ya nyuma akitaka kunichumbia na aliniambia ukweli kuwa alishadivorce na alipata mtoto mmoja kabla ya hiyo talaka. siku moja nikampa mtihani kuwa ampigie mtalaka wake simu mbele yangu amwambie kuwa licha ya talaka yao, anaomba wazae mtoto mmoja zaidi kwani hapendi kuwa na watoto na wanawake tofauti. alisita sana kwani alisema mtalaka wake ana maneno makali sana tena saa nyingine ya kashfa na angeweza kumtukana. baada ya kumhakikishia kuwa kama atamtukana nitamkubalia ombi lake palepale, alikubali.
alipompigia, mkewe alikuwa tofauti na alivyomtarajia. alicheka kwanza kwa mzaha, baadaye akamuuliza "leo una nini wewe, kitu gani kimekupata hadi unafikiria hivyo? natamani nikuone leo nijue kilichokupata!" walipokata simu alishangaa sana kwa maongezi yale, nilimwambia kuwa Mungu akishaunganisha watu huwa hawawezi kutengana, nikamwambia aendelee kumpigia simu kama hizo na amtafute ila akimkataa, tutakubaliana kuoana. sasa leo kanipigia simu anasema kuwa kakubali kuzaa naye! wow. God is at work! i am soooooo happy wapendwa.
jamani ALICHOKIUNGANISHA MUNGU, MWANDAMU ASIKITENGANISHE please!!!!!!!!!!!!!
alipompigia, mkewe alikuwa tofauti na alivyomtarajia. alicheka kwanza kwa mzaha, baadaye akamuuliza "leo una nini wewe, kitu gani kimekupata hadi unafikiria hivyo? natamani nikuone leo nijue kilichokupata!" walipokata simu alishangaa sana kwa maongezi yale, nilimwambia kuwa Mungu akishaunganisha watu huwa hawawezi kutengana, nikamwambia aendelee kumpigia simu kama hizo na amtafute ila akimkataa, tutakubaliana kuoana. sasa leo kanipigia simu anasema kuwa kakubali kuzaa naye! wow. God is at work! i am soooooo happy wapendwa.
jamani ALICHOKIUNGANISHA MUNGU, MWANDAMU ASIKITENGANISHE please!!!!!!!!!!!!!