Hayati Mwinyi alivyomgomea Mwalimu Nyerere kuondoa jina lake ili Salim awe Rais 1985, ikawa ukombozi kwa Watanzania

mdukuzi

JF-Expert Member
Jan 4, 2014
16,053
35,955
Kama kuna kitu kizuri mzee wetu Ruksa alikifanya ilikuwa kumgomea mwalimu Nyerere kuondoa jina lake kwenye mchakato wa Urais 1985.

Ilikuwa hivi:
Mwalimu alikuwa na marafiki watatu kule zanzibar, Thabit Kombo, Salim A. Salim na Aboud Jumbe ambaye alikuja kulikoroga wakawa maadui kisa kutaka kuvunja muungano,

Ikapigwa figisu Aboud Jumbe akapokwa kadi yake ya CCM na kupoteza Urais,akarithiwa na Ali Hassan Mwinyi.
Sasa mwaka 1985 Nyerere alitaka kumrithisha nchi kijana wake Salim, alichofanya ni kupandikiza wagombea namluki wawili, Rashid Kawawa na Ali Hassan Mwinyi wachuane na Salim.

Mchakato ulipokaribia mwisho akamwambia Kawawa ajitoe,yule mzee wa watu alikuwa mtiifu sana kwa Mwalimu,akatii akajitoa.

Akamwendea Ali Hassan Mwinyi ili ajitoe,Mwinyi akagoma,majina yakabaki Mawili, Salim na Mwinyi,wazanzibar wakamwambia Mwalimu kuwa hawamtaki Salim yeye ni Hizbu na anajiona mwarabu zaidi, hajawahi kuyapongeza mapinduzi ya 1964 na inasemekana alishiriki mauaji ya Karume, wakasena chaguo lao ni Mwinyi,

Mwinyi akapita uchaguzi mkuu akapata ailimia 92.
Kwa nini nasema alifanya kitu kizuri, Salim na Nyerere akili zao zilikuwa moja wanasiasa wazuri lakini wajamaa sana, wanachukua ubeparu na matajiri ni kama akili za JPM.

Kipindi mwinyi anachukua nchi,ilikuwa kawaida kuona tako la mti mzima kutokana na suruali kuchanika kwa ukosefu wa nguo, sabuni sigara,sukari,bia,kiberiti,mafuta ya taa, ilikuwa ni anasa,na ungekutwa navyo kuliko kiwango kilichowekwa ni jela na ungepewa kesi ya kuhujumu uchumi.

Ukitaka kununua gari lazima uombe kibali,hata petrol lazima ununue kwa kibali, uchaguzi wa 1985 kampeni zake zilianza october 14 badala ya october 7 kutokana na uhaba wa mafuta nchini. Mwinyi baada ya kushika nchi alibadili kila kitu cha Nyerere, nchi ikafunguka mabilionea wapya wakazaliwa bidhaa zikajaa madukani,... kwa mara ya kwanza kombe la dunia tukaliona live tukiwa sebuleni kwetu, kuvaa viraka ikawa ni ulofa,wasanii wa njw wakaanza kumiminika nchini, Bongoman na chakachaka walipikuja nchini kiingilio ilikuwa laki moja .laki moja ndio, nilikuwa mdogo ila mengi nayakumbuka na mengine niliambiwa na wazee wangu

Itaendelea...
 
Kama kuna kitu kizuri mzee wetu Ruksa alikifanya ilikuwa kumgomea mwalimu Nyerere kuondoa jina lake kwenye mchakato wa Urais 1985.
Ilikuwa hivi:
Mwalimu alikuwa na marafiki watatu kule zanzibar,Thabit Kombo,Salim A. Salim na Aboud Jumbe ambaye alikuja kulikoroga wakawa maadui kisa kutaka kuvunja muungano,
Ikapigwa figisu Aboud Jumbe akapokwa kadi yake ya CCM na kupoteza Urais,akarithiwa na Ali Hassan Mwinyi.
Sasa mwaka 1985 Nyerere alitaka kumrithisha nchi kijana wake Salim,alichofanya ni kupandikiza wagombea namluki wawili,Rashid Kawawa na Ali Hassan Mwinyi wachuane na Salim .
Mchakato ulipokaribia mwisho akamwambia Kawawa ajitoe,yule mzee wa watu alikuwa mtiifu sana kwa Mwalimu,akatii akajitoa,
Akamwendea Ali Hassan Mwinyi ili ajitoe,Mwinyi akagoma,majina yakabaki Mawili,Salim na Mwinyi,wazanzibar wakamwambia Mwalimu kuwa hawamtaki Salim yeye ni Hizbu na anajiona mwarabu zaidi,hajawahi kuyapongeza mapinduzi ya 1964 na inasemekana alishiriki mauaji ya Karume ,wakasena chaguo lao ni Mwinyi,

Mwinyi akapita uchaguzi mkuu akapata ailimia 92.
Kwa nini nasema alifanya kitu kizuri,Salim na Nyerere akili zao zilikuwa moja wanasiasa wazuri lakini wajamaa sana ,wanachukua ubeparu na matajiri ni kama akili za JPM.
Kipindi mwinyi anachukua nchi,ilikuwa kawaida kuona tako la mti mzima kutokana na suruali kuchanika kwa ukosefu wa nguo,sabuni sigara,sukari,bia,kiberiti,mafuta ya taa,ilikuwa ni anasa,na ungekutwa navyo kuliko kiwango kilichowekwa ni jela na ungepewa kesi ya kuhujumu uchumi.
Ukitaka kununua gari lazima uombe kibali,hata petrol lazima ununue kwa kibali,uchaguzi wa 1985 kampeni zake zilianza october 14 badala ya october 7 kutokana na uhaba wa mafuta nchini.Mwinyi baada ya kushika nchi alibadili kila kitu cha Nyerere,nchi ikafunguka mabilionea wapya wakazaliwa bidhaa zikajaa madukani,...kwa mara ya kwanza kombe la dunia tukaliona live tukiwa sebuleni kwetu,kuvaa viraka ikawa ni ulofa,wasanii wa njw wakaanza kumiminika nchini,Bongoman na chakachaka walipikuja nchini kiingilio ilikuwa laki moja .laki moja ndio,nilikuwa mdogo ila mengi nayakumbuka na mengine niliambiwa na wazee wangu

Itaendelea...
JPM hajawahi kuchukia matajiri,bali alichukia wezi wa mali ya umma hasa watumishi wa umma waliojilimbikizia mali kwa njia ya udanganyifu,wakwepa kodi
 
Upo sahihi lakini umeongeza chumvi sana. umelemewa na upendo kwa marehemu kiasi kwamba una adjust fact ili ziendane na kile unachokitamani adhira waamini.
Ni kweli Salim ndiye lilikuwa chaguo la Nyerere
Pengine neno sahihi ni kuwa Mwinyi alimgeuka nyerere.
Alimgeukaje! Ilikuwaje Nyerere mwenyewe akapendekeza jina la mwinyi kwenye Kikao, Why Nyerere alitaka Dr Salimu awe mgombea? Kawawa ilikuaje hakuwa mrithi! hapo sasa ndio pana story ambayo wanao ijua ni wachahache na hawataki kuileza au wanaipotosha. Sasa kama wewe unaijua ilivyo na una utayari wa kutu elimisha please tupe facts pasipo kuweka hisia zako wala kuwa biase.
Tafadhari niwie radhi kama comment yangu itakukwaza
 
JPM hajawahi kuchukia matajiri,bali alichukia wezi wa mali ya umma hasa watumishi wa umma waliojilimbikizia mali kwa njia ya udanganyifu,wakwepa kodi
Mwizi anachukia wez wenzie? Umesahau habari ya kivuko cha bagamoyo? Umesahau zile nyumba ziligawiwa mahawara? Umesahau yule jamaa alikuwa Tanroads Ars akapelekwa bandari? Umesahau Mayanga construction? Umesahau CAG aliyebainisha 1.5T alivotimuliwa? Etc etc.
 
Nyerere ndie aliyempeleka Mwinyi Zanzibar na Nyerere huyo huyo ndie aliyemfanya Mwinyi Rais wa JMT na wala sio SAS kuwa Rais wa JMT
Uko sahihi mara mia moja. mdukuzi ametoa story ya vijiweni ambayo nimeshaisikia sana lakini hai-make sense. Mwinyi angewezeja kumgomea Nyerere kipindi kile chama kimeshika hatamu? Ukweli ni kwamba Mwinyi alikuwa chaguo la Nyerere.
 
Back
Top Bottom