Haya maisha bhana!!

Haya maisha bhana!!

Kwa dunia ya sasa ukisoma kwa kukariri kwamba baada ya kumaliza shule utaajiriwa basi utakufa kwa stress mapema sana.
Wahenga walisema kua uyaone na kweli nimeyaona natamani hata nisingekuwepo duniani. Nimepiga kitabu kwa bidii diploma G.P.A ya 4 degree 4.0 na sioni muelekeo wowote.

Wakuu kitaa ni kugumu natamani hata niyeyuke nilisoma accounting and finance na sioni ikininufaisha kwa chochote, nawaza kwanini nilizaliwa
 
Nikarudi, na kuona chini ya jua, ya kwamba si wenye mbio washindao katika michezo, wala si walio hodari washindao vitani, wala si wenye hekima wapatao chakula, wala si watu wa ufahamu wapatao mali, wala wenye ustadi wapatao upendeleo; lakini wakati na bahati huwapata wote.

Wakati wako bado Mkuu. Usiwaze negatively sana ndio maisha yalivyo, Sometimes You have to be content the way you are.
Hakuna mtu ambae yuko perfect 100 asilimia. Na kumbuka kwamba hata Mti wa Machungwa au Maembe matunda yake huwa hayaIvi yote kwa wakati mmoja kila tunda huiva kwa wakati wake.
Au sio Misss Leejay49
Unapopata kukata tamaa unarudi kusoma hapa
 
Pole mkuu,
Mimi ni kati ya watu waliomaliza chuo wakiwa na gpa ndogo kweli. Nlisoma kozi siipendi kwa shinikizo la mzee plus nikafika chuo nikawa na mambo mengi. Sup za kutosha kila semister na course ilikuwa ngumu kweli watu kibao waka disco nashangaa hata nlitoboaje miaka 3.
Sasa kwakuwa nilijua gpa yangu ni ndogo sana nlijua siwezi compete na wenye ma gpa yao.
Niliamua kutafta njia zangu na kufanya vitu vingine. Luckily baada ya hapo nimewahi kuajiriwa sehemu 3 na kote huko sikuwahi kuulizwa cheti maana bali tu watu wananiajiri kwa experience au reference.
So, mkuu usikate tamaa maisha ni kupambana mlango huu ukizingua unacheki hata dirisha kama unaweza kupenya
Ulipata gpa ya ngapi mkuu
 
Wahenga walisema kua uyaone na kweli nimeyaona natamani hata nisingekuwepo duniani. Nimepiga kitabu kwa bidii diploma G.P.A ya 4 degree 4.0 na sioni muelekeo wowote.

Wakuu kitaa ni kugumu natamani hata niyeyuke nilisoma accounting and finance na sioni ikininufaisha kwa chochote, nawaza kwanini nilizaliwa
Kama upo dasalama na huna kazi nicheki nikupe mchongo ila ni nguvu 9 akili 1
 
Wahenga walisema kua uyaone na kweli nimeyaona natamani hata nisingekuwepo duniani. Nimepiga kitabu kwa bidii diploma G.P.A ya 4 degree 4.0 na sioni muelekeo wowote.

Wakuu kitaa ni kugumu natamani hata niyeyuke nilisoma accounting and finance na sioni ikininufaisha kwa chochote, nawaza kwanini nilizaliwa
Mkiambia nendeni VETA mnaona ushamba Sasa una GPA ndo Nini hata kibara saidia fundi nashindwa kukuita najua skills za handyman huna.
 
Kwani nani alikuambia ukasome hakuna , ulijiendea ,mwenyewe , jingine ungesema awali miezi kuanzia january hadi june ungepata kazi ndugu yangu alikuwa anatafuta muhasibu mshara 1. 2ml sasa kapata na kuna matangazo yalikuwa yanatokea ya watu waliosomea uhasibu mengi saivi unasema funga mwaka nani akuajiri
Daaaah mkuu umempa ukweli wote naona😀
 
Back
Top Bottom