luckyline
JF-Expert Member
- Aug 29, 2014
- 15,153
- 21,798
wape chakula kama kipo kisipokuwepo acha.Mkuu mbwa wako 11 sisi hapa home tuko watatu.. Chakula kinachobaki ni kidogo sana ama kisibaki kabisaaa...
Hiyo kuwapa chakula naona haiwezekani...
Umenikumbusha mbwa wetu "sebeya"
jamani mbwa ni kama mtu kasoro kuongea, nyumbani tulifunga mbwa kiukweli tulimpenda na alitupenda sana
mama akimwagiza kulinda nyumba alikuwa hawezi kutoka.
Mgeni akija mlango wa mbele atazunguka nyumba abweke tukitoka tu lazima tukute mgeni.
Usiku hakuna mtu alopita kwetu labda aite huko barabarani na mchana alikuwa hawezi kumthuru mtu bila kumpa amri.
Mama alimpenda sana, akiona uvivu kwenda porini kuangalia ng'ombe atamwambia sebeya nenda uwaone atakimbia akifika atakaa mlangoni kwa wachungaji baadae atageuza nyumbani. Akifika atakaa karibu na mama tatabweka na kutulia. Tukiwauliza wachungaji kweli wanasema alifika na kugeuza.
Tukifunga shule, kushuka barabarani tu sebeya atatupokea kwa kurukaruka yaani unaona kafurahi kasoro kuongea anajaribu kusaidia mizigo anashindwa, Na alikuwa hawezi kutusahau hata tumalize mwaka bila kufika home.
Ukienda kutembea kwa jirani anakusindikiza analala mlangoni mpaka utoke anakusindikiza nyumbani labda umwambie sebeya nenda nyumbani anatii na kuondoka.
Sebeya alikuwa hawezi kula chakula bila kumwambia kula au kukiweka kwenye beseni lake.
Walimwengu walikuja kumuua kwa kumwekea sumu kwenye chakula chake.
Tulimuuguza bila mafanikio, waganga wa mifugo walitibu wakashindwa, alikuwa analia kama mtu, sebeya mpaka anakufa tulikuwa nae karibu mpaka pale alipoaga dunia kwenye kijumba chake. Tulilia sana siku hiyo,
Alizikwa kwa heshima na aliwekewa shuka.
Sebeya tulianza kuishi nae akiwa mdogo mwaka 1994 mpaka hapo alipoaga dunia 2004.7.16. Jioni
Daima tutamkumbuka sana tulimpenda ila mungu alimpenda zaidi. Ni miaka 13 sasa tangu atutoke. Rip sebeya