interegenciadick
JF-Expert Member
- Nov 26, 2016
- 698
- 1,111
Muda mwingine naona polisi tunawapa zigo sana... Kwanini?Tusiishie kuangalia mtu mmoja na kuacha mifumo.
Tuna tatizo la kujielewa na kuthamini maisha ya watu.
Kwa mfano, mara nyingi nikienda sehemu zenye mikusanyiko ya watu Marekani, vyumba huwa vimeandikiwa idadi ya watu, kwa mfano, chumba au ukumbi huu haukitakiwi kuzidisha watu 300. Sikumbuki kuona hilo Tanzania.
Katika mikutano ya watu, hatuna mifumo ya crowd control. Hatuna watu wa kutosha wa kuongoza makundi ya watu, hatuna mifumo ya kuweka uzio wa wapi watu wanaruhusiwa kuranda, na wapi ni njia ziachwe wazi kwa watu kutumia wakati wa dharula. Hatuna watu wa kutosha walioajiriwa kuhakiki usalama wa watu.
Sasa hivi naona jitihada kubwa zipo kwenye kuelekeza lawama kwa mtu mmoja, Mwamposa. Mwamposa inawezekana ana lawama zake, sikatai hilo.
Lakini tujiulize. Kwa nini ni rahisi sana kwa polisi kukataza mikutano ya kisiasa ya vyama vya upinzani, kwa sababu zisizo za msingi, wakati polisi hawakatazi mikutano ya kidini isiyo hata na mipango ya usalama.
Bila ya kuangalia haya, hatuwezi kudhibiti matukio kama haya yaliyoua watu huko Moshi.
Sent using Jamii Forums mobile app
Sababu wangeingilia haya mambo ya kidini kama hivo ungesikia mitanzania tunapiga kelele kuingilia uhuru wa mtu kuhudumu kumbe ile ni kuwekeana utaratibu wa nini kifanyike kwenye mikusanyiko.
Points zako kibao sina shida nazo maana umeongea ukweli kabisaa Tz hatuna watu au watalamu wa kuona mambo kwa umbali kwenye mikusanyiko kama hii.
doggystyle changeinarudi shehe[emoji527]