Hatua za kuchukuliwa baada ya watu 20 kufa Moshi

Hatua za kuchukuliwa baada ya watu 20 kufa Moshi

Tabutupu

JF-Expert Member
Joined
Nov 26, 2010
Posts
13,262
Reaction score
18,711
Kwanza nimpongeze waziri wa mambo ya ndani kwa hekima aliyo tumia kuweka vizuri jambo hili hadi likaeleweka vizuri kwa jamii juu ya makosa yaliyofanyika na huyu mtu anaye jiita nabii.


Pili hili liwe fundisho kwa hawa wasaka utajiri kwa udanganyifu kupitia dini, sijui Mungu wa nyakati hizi ameounguza hasira lakini ipo siku watalipwa sawaswa na matendo yao.


Naomba serikali ifanye mambo haya.


1. Kufunga mojamoja kwa moja kibanda hiki cha mwamposa.

2. Asiruhusiwe kufanya mamho yake haya ndani ya Tanzania.

3. Yeye mwamposa na kundi lake wawajibike na kesi hii ya mauaji kama kesi nyingine.

4. Achunguzwe Utajiri wake na kundi lake lote waeleze wamepata wapi.

Hili liwe fundisho kwa wengine wenye roho mbaya kama mwamposa. Ameacha watu wamekufa na kujeruhiwa anekimbilia dar kwenye kibanda chake kawe. Roho mbaya sana hii.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe haupo sahihi! Mwenye makosa hapa siyo mwamposa bali ni polisi waliotakiwa kutoa ulinzi ila hawakuwajibika! Polisi wako tayari kulinda mikutano ya CCM lakini hawapo tayari kulinda mikutano mingine ya wananchi.Polisi wapo tayari kutokutoa vibali vya mikutano ya vyama vya upinzani kwa kisingizio kuwa hakuna usalama ila ukitaka kufanya mkutano wa dini wala hutakiwa kuomba kibali na wala hawana haja ya kuja kuhakikisha usalama wa mkutano huo.

Mwamposa yeye ana jukumu la kukusanya watu na kuwapiga neno la mungu ila suala la crowd risk management strategy ni la polisi. Polisi hawakutimiza wajibu wao kwa hiyo wao ndiyo watuhumiwa namba moja!
 
Pamoja na machungu yote sion kosa la mwamposa kisheria
USSR
Sent from my SM-J110H using JamiiForums mobile app
Kuna kitu kinaitwa criminal negligence, hasa iwapo hiyo neglicence itasababisha kifo. Mwamposa lazima awe liable kwa negligence. Alitakiwa in the first place kutafakari kabla hajaruhusu watu zaidi ya elfu 10 kupita kwenye geti moja kwa wakati mmoja. Hilo la kwanza.

Namba mbili, Mwamposa aliomba kibali cha mikutano kuanzia sa 6 mchana hadi sa 12, maafa yametokea sa 2 usiku, hivyo alivunja sheria, akawa na unlawful assembly nje ya kibali.

Tatu, Mwamposa amekosa ubinadamu na ustaarabu, amesababisha watu kufa halafu akakimbia eneo la tukio, yeye ndie aliomba kibali hivyo alipaswa kurudi polisi kutoa taarifa nini kimeendelea na hata kama mkutano ungeisha salama alitakiwa kwenda polisi kutoa taarifa na kushukuru. Hakufanya hivyo, akakimbia, tena kwa kukwepa mamlaka, alikua arudi na ndege akashtuka atakamatwa akatumia gari, huu ni uhayawani.

Mwamposa amekosa hata huruma ya kuwa eneo la tukio kuwafariji waumini wake, kuwapa pole kwayaliyotokea.

Hili la Mwamposa ni wazi alikua na nia mbaya-ill motive hasa baada ya kukimbia eneo la tukio. Apigwe marder case atulie kwanza lupango.

Mpumbavu sana.
 
Upumbavu na Ujinga wa Kilokole ndiyo Huu! Mambo ya kiroho haya au Ujinga? Sijaona one time Yesu apifanya miujiza vikatokea Vito vya Kijinga kama hivi!
Ukishaona Mtu anajiita mwenyewe Nabii badala ya kusubiri aitwe na wakati huohuo hajawai kutoa Unabii wowote mwogope sana huyo TAPELI.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jukwaa la kumuhubili Kristo lilitahadhalisha mapema sana juu ya hawa matapeli serekali na waziri Wa mambo ya ndani fungeni Huduma za hawa waganga Wa kienyeji kupitia dini

Sent using Jamii Forums mobile app
Msisitizo uwe usalama kwenye makanisa.Kuwa viongozI wa dini wahakikishe usalama upo na waumini wanakuwa salama

Sababu mtu kama mfano TB JOSHUA au Mzee mwasapile wa kikombe cha babu elimu hawana lakini maprofesa na ma doctor walienda kukinywa NA kWA TB JOSHUA NIGERIA HUFURIKA KIBAO.Imani ni kitu complicated

WASISITIZIWE tu usalama maeneo ya ibada kuwa viongozi wa dini wahahakikishe kuna usalama kwenye maeneo yao ya ibada.Hayo mengine ya wanaabudu nini Wawaachie wenyewe kama watakanyaga mafuta au mavi ya kiongozi wa dini yao shauri yao

NAMNA YA KUABUDU KILA MTU ANA YAKE
 
Jukwaa la kumuhubili Kristo lilitahadhalisha mapema sana juu ya hawa matapeli serekali na waziri Wa mambo ya ndani fungeni Huduma za hawa waganga Wa kienyeji kupitia dini

Sent using Jamii Forums mobile app
MIMI binafsi siendi kwa mashehe wala waganga wa kienyeji huwa naenda kwa waganga wakiristo wenye vilinge vya uganga wa kikiristo kama huyo Mwamposya, Nabii suguye,Ngurumo ya upako nk mwenyewe napenda na hunitoi huko
 
  • Thanks
Reactions: R.K
Jamani hili tatizo si dogo kama linavyofikiriwa ni tatizo kubwa sana. Ni tatizo lililojificha ndani ya Mabongo, hisia, mazoea na malezi yetu.

Wote ni mashuhuda hapa nchini jinsi kikombe cha Babu wa Loliondo kilivyowaumbua watu na Madigirii yao walipanga foleni kwenda pata kikombe

Haya yanayotokea kwa Mwamposya ni dalili ya tatizo kubwa lililopo kwa Watanzania/Waafrica. Hawa watu wanaoandika vibao vya Freemason kwenye nguzo za umeme, Waganga wa Jadi akina Sharrif Majini na hawa Wachungaji sio wajinga. Wameona opportunities(udhaifu ktk uwezo wa kuchanganua changamoto za kimaisha) wanazitumia hizo opportunities kujinufaisha

TATIZO KUBWA NI pale watu ambao tungefikiri wangeweza kusaidia kutatua tatizo hili nao wako mtegoni hawana tofauti na mwananchi wa kawaida wa Tandale(ashaakum si matusi)
Kwani sote ni mashuhuda jinsi wanavyohangaika nyakati hizi zinazokaribia uchaguzi.

Hapa ndipo panapoonekana umuhimu wa "Nation Think Tank"
Mtu kama Jenerali Ulimwengu, Prof Issa Shivji na Dr. Rakesh Rajan ni watu muhimu sana ktk mijadala kama hii

Ingewezekana ingewekwa topic hasa kwenye Civics/GS/DS ni jinsi gani kijana akikumbana na Matapeli wa aina hii ni jinsi gani ya kupambana nao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Behaviourist,
Kama mungu wenu ameshindwa kuwalinda dhidi ya majanga yaliyotokea,unaamini kuwa polisi wangeweza kuzuia hayo majanga yasitokee? au unamanisha kuwa polisi ni zaidi ya mungu wenu? au mlitaka polisi wawepo ili na wao wawe ni sehemu ya kafara?.
 
Mwamposa mwenyewe analindwa na mabausa
Kama mungu wenu ameshindwa kuwalinda dhidi ya majanga yaliyotokea,unaamini kuwa polisi wangeweza kuzuia hayo majanga yasitokee? au unamanisha kuwa polisi ni zaidi ya mungu wenu? au mlitaka polisi wawepo ili na wao wawe ni sehemu ya kafara?.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom