Kiranga
Platinum Member
- Jan 29, 2009
- 87,489
- 151,694
Tusiishie kuangalia mtu mmoja na kuacha mifumo.Kwanza nimpongeze waziri wa mambo ya ndani kwa hekima aliyo tumia kuweka vizuri jambo hili hadi likaeleweka vizuri kwa jamii juu ya makosa yaliyofanyika na huyu mtu anaye jiita nabii.
Pili hili liwe fundisho kwa hawa wasaka utajiri kwa udanganyifu kupitia dini, sijui Mungu wa nyakati hizi ameounguza hasira lakini ipo siku watalipwa sawaswa na matendo yao.
Naomba serikali ifanye mambo haya.
1. Kufunga mojamoja kwa moja kibanda hiki cha mwamposa.
2. Asiruhusiwe kufanya mamho yake haya ndani ya Tanzania.
3. Yeye mwamposa na kundi lake wawajibike na kesi hii ya mauaji kama kesi nyingine.
4. Achunguzwe Utajiri wake na kundi lake lote waeleze wamepata wapi.
Hili liwe fundisho kwa wengine wenye roho mbaya kama mwamposa. Ameacha watu wamekufa na kujeruhiwa anekimbilia dar kwenye kibanda chake kawe. Roho mbaya sana hii.
Sent using Jamii Forums mobile app
Tuna tatizo la kujielewa na kuthamini maisha ya watu.
Kwa mfano, mara nyingi nikienda sehemu zenye mikusanyiko ya watu Marekani, vyumba huwa vimeandikiwa idadi ya watu, kwa mfano, chumba au ukumbi huu hautakiwi kuzidisha watu 300. Sikumbuki kuona hilo Tanzania.
Katika mikutano ya watu, hatuna mifumo ya crowd control. Hatuna watu wa kutosha wa kuongoza makundi ya watu, hatuna mifumo ya kuweka uzio wa wapi watu wanaruhusiwa kuranda, na wapi ni njia ziachwe wazi kwa watu kutumia wakati wa dharula. Hatuna watu wa kutosha walioajiriwa kuhakiki usalama wa watu.
Sasa hivi naona jitihada kubwa zipo kwenye kuelekeza lawama kwa mtu mmoja, Mwamposa. Mwamposa inawezekana ana lawama zake, sikatai hilo.
Lakini tujiulize. Kwa nini ni rahisi sana kwa polisi kukataza mikutano ya kisiasa ya vyama vya upinzani, kwa sababu zisizo za msingi, wakati polisi hawakatazi mikutano ya kidini isiyo hata na mipango ya usalama.
Bila ya kuangalia haya, hatuwezi kudhibiti matukio kama haya yaliyoua watu huko Moshi.
Sent using Jamii Forums mobile app