Abdul Said Naumanga
JF-Expert Member
- Jan 28, 2024
- 745
- 1,470
Disclaimer:
Uzi huu umeandaliwa kwa madhumuni ya kutoa elimu na kuibua mjadala wa kitaalamu na kiraia kuhusu uamuzi wa TCRA dhidi ya JamiiForums. Yalichopishwa hapa hayapaswi kutafsiriwa kama ushauri rasmi wa kisheria, bali ni uchambuzi wa kisheria na kikatiba kwa lengo la kuelimisha na kujadili kwa pamoja masuala yanayogusa haki, wajibu na utawala wa sheria.
Uzi huu umeandaliwa kwa madhumuni ya kutoa elimu na kuibua mjadala wa kitaalamu na kiraia kuhusu uamuzi wa TCRA dhidi ya JamiiForums. Yalichopishwa hapa hayapaswi kutafsiriwa kama ushauri rasmi wa kisheria, bali ni uchambuzi wa kisheria na kikatiba kwa lengo la kuelimisha na kujadili kwa pamoja masuala yanayogusa haki, wajibu na utawala wa sheria.
Habarini wanajamvi,
Nikiwa kama mmoja wa wanachama wa JF ambao hatujaridhishwa kabisa na uamuzi wa TCRA kulifungua jukwaa hili pendwa haswa kwa intelligent, smart and reasonable people, naona wazi haki yangu na mmeber wenzangu ya kutoa maoni ikibagazwa waziwazi. Sisemi JF wapo sahihi wala sisemi Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) wapo sahihi, ninachojaribu kusema ni kwamba haya mambo yanayogusa haki za watu moja kwa moja yanatakiwa kuangaliwa kwa jicho pana kuliko walilolitumia TCRA.
Kwa kuwa suala hili ni refu na linagusa sheria na katiba, nitaligawa katika sehemu nne: sehemu ya kwanza hii itaeleza msingi wa kisheria wa TCRA, sehemu ya pili madai yao dhidi ya JF, sehemu ya tatu mapungufu ya kisheria na taratibu, na ya nne itakuwa mapendekezo ya nini JF na sisi wananchi tunaweza kufanya.
Okay, nadhani wote tumeshuhudia siku za hivi karibuni TCRA ikitoa uamuzi wa kusimamisha leseni ya maudhui mtandaoni ya JF (Vapper Tech Ltd) kwa muda wa siku tisini. Uamuzi huu umeibua mjadala mkubwa miongoni mwa wananchi na wadau wa habari kuhusu uhalali wake, taratibu zilizofuatwa, na athari zake kwa haki za kikatiba za uhuru wa kujieleza na kupata habari. Ila kabla ya yote ni muhimu kwanza kufahamu msingi wa kisheria wa mamlaka ya TCRA, taratibu zinazopaswa kufuatwa, na hatimaye kutathmini hoja za TCRA dhidi ya JF.
Kiufupi Mamlaka ya TCRA kufanya walichoifanyia JF yametokana kwa mujibu wa sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Post, yaani Electronic and Postal Communications Act, Cap.306. Sheria hii inawapa nguvu ya kusimamia sekta ya mawasiliano na hasa kutoa na kusimamia leseni za huduma za maudhui mtandaoni. Kwa mujibu wa kifungu cha 103 cha sheria hiyo, Waziri wa Mawasiliano anayo mamlaka ya kutunga kanuni ndogo (subsidiary legislation) za kusimamia maudhui. Ndipo ilipozaliwa Electronic and Postal Communications (Online Content) Regulations, 2020 (GN No. 538/2020) na marekebisho yake ya mwaka 2022 (GN No. 136/2022) pamoja na ya mwaka 2025 (GN No. 57/2025). Kanuni hizi ndizo zilizobainisha majukumu ya “online content service providers” kama JF, “internet service providers” na hata wamiliki wa mitandao ya kijamii.
Pia kwa mujibu wa Kanuni ya 8(1) ya kanuni za 2020, TCRA inaweza kusimamisha au kufuta leseni iwapo masharti yaliyotolewa kwaajili ya matumizi ya leseni hiyo yatakiukwa. Pia Kifungu cha 22 cha sheria ya Mawasiliano Cap. 306 TCRA inaweza kufungia ama kusimamisha leseni na hatua hiyo inapaswa kuchukuliwa tu endapo kuna material breach , na TCRA lazima imjulishe mtoa huduma kwa maandishi na kueleza sababu.
Nitaendelea 🚶🏿🚶🏿🚶🏿