The Watchman
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 2,176
- 4,918
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) inapenda kuutaarifu umma na kuvikumbusha vyombo vyote vya habari nchini, ikiwemo televisheni, redio, machapisho, mitandao ya kijamii, tovuti na majukwaa ya kidijitali, juu ya wajibu wao wa kufuata sheria na kanuni za mawasiliano katika kutoa habari kwa umma.
Soma TCRA yakanusha kutoa onyo kwa vyombo vya habari kusambaza maudhui kutoka kwa watu wenye kesi za uhaini
TCRA imebaini mwenendo wa baadhi ya watoa huduma za habari kurusha au kusambaza maudhui kutoka kwa watu wenye kesi zinazoendelea mahakamani, ikijumuisha kesi za tuhuma za uhaini, maudhui ambayo kwa namna tofauti yanaweza:
Maelekezo kwa vyombo vya habari:
Mamlaka itaendelea kufuatilia kwa karibu mawasiliano yote ya kielektroniki ili kuhakikisha kuwa mtandao unatumika kwa manufaa ya jamii na nchi kwa ujumla.
Soma TCRA yakanusha kutoa onyo kwa vyombo vya habari kusambaza maudhui kutoka kwa watu wenye kesi za uhaini
TCRA imebaini mwenendo wa baadhi ya watoa huduma za habari kurusha au kusambaza maudhui kutoka kwa watu wenye kesi zinazoendelea mahakamani, ikijumuisha kesi za tuhuma za uhaini, maudhui ambayo kwa namna tofauti yanaweza:
- Kuhamasisha au kuchochea uvunjifu wa amani,
- Kuathiri mchakato wa haki mahakamani,
- Kusababisha upotoshaji na taharuki kwa jamii,
- Kuhatarisha usalama na utulivu wa taifa.
Maelekezo kwa vyombo vya habari:
- Msitoe, msirushe, wala kusambaza maudhui kutoka kwa watu wenye kesi zinazoendelea mahakamani bila kufuata taratibu zinazokubalika kisheria.
- Hakikisheni uhariri wa kina kabla ya kuchapisha au kutangaza taarifa zinazoweza kuathiri amani na usalama wa nchi.
- Epukeni kurusha maudhui yenye lugha ya uchochezi, upotoshaji au yanayoweza kujenga hofu na mgawanyiko katika jamii.
Mamlaka itaendelea kufuatilia kwa karibu mawasiliano yote ya kielektroniki ili kuhakikisha kuwa mtandao unatumika kwa manufaa ya jamii na nchi kwa ujumla.