Nilianza kumsikia kwa mbali alipochaguliwa kuwa mbunge Hai mwaka 2000
Alipata umaarufu zaidi alipochaguliwa kuwa mwenyekiti wa CHADEMA (2004?)
Alipata umaarufu sana alipogombea uraisi mwaka 2005, zaidi kwa kuanzisha styles za helkopta na magwanda, ambazo ni maarufu hadi leo
Alikuja kuvuma tena sana wakati wa operesheni sangara.
Katika uchaguzi uliopita, hakuvuma sana (kwa sababu ya kuwepo Slaa katika uraisi?)
Alikuja kuvuma zaidi wakati wa kuundwa kwa kambi ya upinzani
Aliendelea kuwa midomoni mwa watanzania katika matukio tofauti kwa kiwango tofauti hadi Ijumaa tarehe 3 June 2011
Kwa siku tatu mfululizo Kuanzia Ijumaa jioni, hadi leo asubuhi, Freeman Aikaeli Mbowe amengeza mstari mwingine katika historia yake ya kupigania wanyonge Tanzania. Mstari ambao kwa wanaofuatilia vyombo vya habari na kusikiliza maoni ya watu ya kisiasa, bila shaka unastahili kuandikwa bolded zaidi, na kwa font kubwa zaidi, angalau kuliko mistari yote iliyowahi kuandikwa siku ya nyuma...