Hatimaye Mbowe apewa dhamana

Hatimaye Mbowe apewa dhamana

Kiwango cha upumbavu wa Magesa (kama anao) hakiwezi kuzidi chako wewe unayedhani kwamba mtu akiwa kiongozi wa CDM basi ana kinga dhidi ya hatua zinazotokana na ukiukaji wa sheria. Yeye alikataa kwenda kwa hiari yake na sasa amelitia hasara Taifa. Huyu aliyelazimisha hazina ya Taifa kutumika kumsafirisha kwenda kuitikia wito halali ndiye wa kulipa fidia!

Unachanganyikiwa nini?, wakati kuna wezi na mafisadi hata kuwataja hawatajwi. lakini wanawaibia wananchi. Swala si mtu kuwa juu ya sheria, issue ni kwa nini viongozi wa CDM/ Chama cha wanyonge wanakamatwa hovyo? na baada ya kuona nguvu ya umma wanaachiwa au na sisi tuwe na jeshi letu la kuwakamata mafisadi wa CCM?
 
Dondoo za yaliyojiri kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi, Charles Magesa Arusha leo:

  1. Hakimu Magesa alisema ni kweli mahakama iliruhusu washitakiwa wabunge wahudhurie kikao cha bunge la bajeti na hivyo hawana tatizo na Mh. Mbowe, ila kutokana na kukosekana kwa mdhamini wake, ndiyo sababu walitoa amri ya kukamatwa kwake.
  2. Hakimu amesema mahakama inaendelea kuwapa ruhusa washitakiwa wote ambao ni wabunge kutohudhuria mahakamani hapo hadi pale ambapo kikoa cha bunge kitamalizika ila aliwasisitiza wadhamini wa washitakiwa kuhudhuria mahakamani kila siku ambapo tarehe ya kesi imepangwa
  3. Wakili upande wa Utetezi, Method Kimomogoro, aliiomba Mahakama kuondoa amri ya kukamatwa kwa Mbowe na kutaka apewe dhamana yake ya awali, ili aweze kuhudhuria vikao vya bunge la bajeti ambalo yeye ni kiongozi wa kambi ya Upinzani na kwamba mdhamini wa Mbowe hakufika mahakamani kwa kuwa alisahau, na hiyo ipo kwa kila mtu na hata wao kama mawakili wanasahahu tarehe za mahakamani.
  4. Mdhamini wa Mbowe bwana Julius Margwe alizitaja sababu za kutofika mahakamani Mei 27, 2011 ni kutokana na kuwa na kesi Mahakama ya Mwanzo Maromboso. Pia, hakufika Mahakamani Mei 30, 2011 kwa sababu mahakama haikumpa nafasi kusema lolote.
  5. Wakili wa Serikali Juma Ramadhani, aliiomba mahakama hiyo itoe onyo kali kwa mshitakiwa kwa kutofika mahakamani hapo na pia kumtaka mshitakiwa huyo na wenzake wawe na mawasiliano ya karibu na wadhamini wao, ili wasikosekane wanapotakiwa mahakamani hapo, pia, mdhamini wa Mbowe hana uhakika na hajui nini anafanya, hivyo hafai kuwa amdhamini.
  6. Hakimu Magesa akasema Julius ana makosa mengine yanayomkabili na hata hawezi kujieleza, hivyo Mahakama haina sababu kuwa naye sababu tayari ana kesi ya jinai ambayo hatma yake haifahamiki.
  7. Mahakama imemkubali mdhamini mwingine ambaye ni John Bayo, Diwani wa kata ya Elerai (CHADEMA).
  8. Baada ya Freeman Mbowe, kuachiwa huru na aliwashukuru wananchi na kusema anasikitishwa sana na kutumia nguvu kubwa kumlinda yeye na kumsafirisha usiku akiwa chini ya ulinzi mkubwa kama kwamba yeye alikuwa ni gaidi ambaye alikuwa na silaha, “Mimi nilijipeleka mwenyewe polisi sasa kama kweli ningekuwa wa kukimbia ningejipeleka? Sasa wao hawajaona hayo yote haitoshi wameamua kutumia nguvu kubwa sana maana wakati wakinipeleka uwanja wa ndege walikuwa na polisi wengi sana zaidi ya 50 yaani utadhani ni gaidi anapelekwa alafu ndege ya kubeba watu mia ndo wameniweka mimi, wakati hayo mafuta wangeyaweka ata kwenye kutengeneza vitanda vya hospitali. Wanatumia vibaya kodi za wananchi “alisema Mbowe. Alisema kuwa Serikali ilitumia ndege ya jeshi, ambayo ina uwezo wa kubeba watu 100, ambayo ilichukua watu watatu yaani yeye, Kamishina wa Polisi kanda kanda ya Ilala na Kamishna wa Polisi wa kikosi cha kuzuia ghasia wa Tanzania hadi KIA usiku wa majira ya saa 9.00. Pia alisema mbali na kusafirishwa kwa ndege hiyo kubwa, pia kulikuwa na magari nane ya FFU ambao walikuwa na mabomu na silaha kama wanasindikiza mhalifu. Akashukuru Polisi kutomfanyia unyama wowote, walikaa naye vizuri, isipokuwa alinyimwa haki yake ya msingi ya kuwa na uhuru wa kuwasiliana na watu. Mara baada ya kesi hiyo kumalizika wananchi walimbeba kiongozi waho kwa juu huku wakiimba.
Kesi ilihudhuriwa na wabunge 13 wa CHADEMA ambao ni Zitto Kabwe, Halima Mdee, Godbless Lema, Suzan Kiwanga, Ezekia Wenje, Christina Lissu, Paulina Gekulu, Israel Natse, Suzana Lyimo, Joseph Mbilinyi, Rahya Ibrahimu ( Mbunge toka Pemba), Joyce Mukya na Joseph Selasini.


SOURCE:Wavuti - Home
Ahasante Mkuu Kibakwe kwa hii taarifa, ni sawa kama tulivyo predict gharama kubwa bila sababu yoyote!!!!!!!!!! Maghamba tumia busara kidogo tafadhari tuepushieni hasara zisizo na msingi Watanzania!!!!!!!!!!
 
wee unapimaje umaarufu,mbona alikua rumande sasa amepiganiaje hiyo haki,na kama ni hivyo kuwekwa rumande ndio umaarufu basi mch. mtikila ndie jembe zaidi kuliko yoyote tanzani.

Amepigania haki kwa kulazwa rumande kwa ajili ya kupinga vitendo vya Jeshi la Polisi kutumiwa na CCm kuwabana wapinzani ambao wanatetea masahi ya umma na haki za wanyonge. Mbowe anachopinga ni vitendo vya Jeshi la Polisi kuwa na ubuguzi wa dhahiri ambao wabunge wa CCM wakifanya makosa ya jinai makubwa zaidi huombewa viabli kwa Spika ili anagalau kuhojiwa tu, lakini wabnge wa upinzani wakituhumiwa tu hukamatwa na kurundikwa ndani ii kukwamisha uamshaji wa wananchi.
 
Wanadanganywa, wanadanganyika. ndio maana mara mgogoro uvccm na imara wanatumiwa na cdm kuvuruga amani.
kwani kabila kubwa la wakazi wa Arusha ni wafugaji. kabila hili ni wazi limekosa elimu kwa miaka mingi sasa. lkn siasa za tz sasa zimehamia huko. CDM yenye ngome kwa sasa. nadhani imefika wakati cdm wawe na mkakati imara wa kuwasomesha ndugu zetu waondokane na sisasa hizi

Nadhani unafikiria zaidi kupitia ******, nxt time tumia ubongo.
FYI wakaazi wengi wa Arusha ni wakuja na ama wameamia kikazi au kutafuta maisha na pia elimu siyo vidato tu kama unavyodhania
 
Pia nadhani kuna tatizo la ufahamu wa taratibu ndani ya jeshi la polisi. RPC wa Mwanza labda ndiye anayefaa kuwa IGP.

Hiki kichwa achana nacho, shule imelala hapo na haikupata cheo kwa kubana miguu kama wengine bali ni elimu na uelewa wa (Mbayuwayu) kuchanganya na za kwake
 
Jamani kila wakati nawaza sana kuhusu jeshi la polisi la tanzania. Mbona watumia zaidi nguvu kuliko hekima, akili, na busara. Kushika kwao silaha ndo washindwe hata kufikiri basics. Kama mh. mbowe aliripoti mwenyewe, polisi, walimshikilia ili nini? Je mbowe ni mtu anayeweza kukimbia? Je walishindwaje kumwamuru jumatatu ariport mahakamani badala ya wao kumshikilia na kumsafirisha na ndege binafsi ya kukodi? Ili jeshi limejaa watu ambao hawana shule, na failures wengi, wengi waliopata sifuri (0) form IV na form VII. Hili jeshi linafanya faulu sana katika mambo mengi ikiwa ni pamoja na mauaji ya Arusha, tarime, nk.

Nchi nzima watu walikua kwenye tension kwa sababu ya ujinga wa Kova. Hatuna jeshi bali kikundi cha wahuni na wezi

Jazba uliyonayo imesababisha uchanganye mambo. Katika sakata hii Mahakama iliwaamuru Polisi wamkamate Mbowe, hawakujiamulia wao na hawana shida naye kwa sasa kwani shauri lililowakutanisha liko Mahakamani siku nyingi Huu mjadala umeuanzia mkiani, pole sana.
 
Pia nadhani kuna tatizo la ufahamu wa taratibu ndani ya jeshi la polisi. RPC wa Mwanza labda ndiye anayefaa kuwa IGP.

Inaenda bila kusema; said Mwema anafaa kuwa askari wa kawaida kwa vile inaonekana kazi za kuagizwa anazitekeleza kwa umakini wa kupita kiasi. Kazi na maamuzi yanayohitaji busara na hekima ni zero kabisa.
Baba akiwa mlevi, watoto watavuta hata bange kama tunavyoona sasa hapa Tanzania.
 
HIVI NGOJA NIULIZE, mbona Slaa alipoitwa mahakamani alienda bila tatizo? Kwa nini Mbowe hakwenda as required? Na kama alikuwa na jambo muhimu la kufanya,kwa nini mwanasheria wake hakutoa taarifa mapema?
Mkuu kama nimesoma ile taarifa ya Hakimu Magesa aliyotoa mahakamani vizuri, yeye anasema alikua hana shida na Mbowe i.e. alisharuhusu Mbowe ahudhurie vikao that means Mbowe alishaomba dharura akaruhusiwa. Sasa ninachojiuliza mimi ni hiki " Nani basi alitoa kibali cha Mbowe kukamatwa?? Naona bado kuna majibu yanahitajika. Na kama umesikiliza/soma maelezo ya Slaa, inaonyesha palikua na mabishano kule mahakamani siku walipohudhuria kina Slaa kuhusu vifungu vya sheria vinasemaje (Soma hiyo thread ya maelezo ya Slaa na Magesa) unaweza pata picha pana zaidi.
 
Heshima kwako WildCard.

Mkuu tuko pamoja haswa, CHADEMA na viongozi wake hasa mwenyekiti Mheshimiwa A F Mbowe lazima wajue Tanzania [Wananchi] wanawahitaji sana hasa kwenye masuala muhimu eg katiba mpya,vita vya ufisadi,matumizi sahihi ya kodi zetu na nk.CHADEMA lazima wawe makini sana wasije kuwaangusha kama ilivyotokea kwa NCCR Mageuzi wengi wanadhani mageuzi ni lelemama.Mageuzi yanahitaji mikakati makini matatizo madogo madogo kama hili la Mheshimiwa Mbowe yalitakiwa kuepukwa mapema hapakuwepo na sababu za msingi Mwenyekiti wa chama cha upinzani kuswekwa ndani, ni jambo linaloweza kuepukwa.

CHADEMA kama cha kikuu cha upinzani lazima kikae chini kitafakari kwa kina nini kilijiri hadi mwenyekiti wake afikie hatua ya kukamatwa.Je CHADEMA hakuna wanasheria wakutosha ?,Je wasaidizi wa mwenyekiti walifanyakazi yao vyema ?,Je viongozi wa CHADEMA wafuate mkondo wa Mchg Mtikila.

Najua hapakuwa na sababu za msingi kwa kiongozi kama Mbowe kufanyiwa aliyofanyiwa.hakika mahakama na polisi wanajua dhahiri Mbowe hawezi kutoroka lakini Mbowe alitakiwa kujua kabla kwamba wakuu wa hivi vyombo wanategemea fadhila za CCM kupanda vyeo [IGP Mahita na A L Mrema] hivyo alitakiwa kuchukua tahadhari mapema.

Hapo kwenye red tuko pamoja kabisa Mkuu.
 
Mungu ashukuriwe! kaongeza umaarufu balaaa, kila redio inamjadili.
 

Jazba uliyonayo imesababisha uchanganye mambo. Katika sakata hii Mahakama iliwaamuru Polisi wamkamate Mbowe, hawakujiamulia wao na hawana shida naye kwa sasa kwani shauri lililowakutanisha liko Mahakamani siku nyingi Huu mjadala umeuanzia mkiani, pole sana.

Ukiona hivyo ujue na yeye ni O au 0 teh teh teh
 
"Cogito ergo sum" i.e. I think and therefore I am... Kuna mtu ananiambia hapa nilipo kwamba wapinzani wanaleta vita.
:majani7: Sijui anataka tucheze rege?

:confused2: Watawala tulionao sasa hivi wamechoka kazi yao ndo maana wanaamua kuanzisha mitafaruku katika jamii wakidhani kwamba inaweza kusaidia kufanya watu wasahau. ki-ukweli ni kwamba DOWNS and SYMBIASIS ni dhana halisi ya kujivua gamba na si kutema wale watatu!!!! simple...kamata Wembo kisha changanya watu ili SYMBIASIS itimize lengo...

I :mwaaah: CDM na hakika ametoka kama alivyosema, kweli katoka!!!

Mara walitoa msimamo wao...duh nisingependa kuona Nyamongo nyingine...HAKIKA AMETOKA KWELI KAMA ALIVYOSEMA

Hongera sana wana CDM kwa kupigania haki zetu sisi wanyonge --- "NIHIL NIHIL FIT"

people's power!!!
 
Je AMRI YA MAHAKAMA YA KUKAMATA WASIMAMIZI WA DOWANS KWA KUZA MITAMBO HALI KKESI IKIWA MAHAKAMANI NI HALALI AU SIO HALALI KWA NI MBONA HAKUNA ALIYEKAMATWA KWA KUWA WAHUSIKA NI CCM
 
Waberoya punguza woga wa kusema ukweli-tupe mtazamo wako basi credibilty ya chadema imepanda au imeshuka?usitafune maneno maana tuna criminals nchi hii ambao tungetamani nguvu kubwa kama hii itumike but chama unachoamini huwaita na kujadiliana nao gizani!!!!
 
Waweza tu kumuapisha akawa rais wa familia yenu ubaya upo wapi kwani , ila yule wa watanzania aliisha apishwa !

kweli mkuu. Angeapishwa kuwa rais wa familia yetu,yan familia ya watanzania. Nyie wakuja si hamuhusiki ktk familia ya Watanzania,ndo maana hata uchungu hauna! Ipo siku tutawaexport kwenye makontena kuwarudisha huko kwenu na akina RA wenu!
 
Back
Top Bottom