Hatimaye Mbowe apewa dhamana

Hatimaye Mbowe apewa dhamana

Inasikitisha! inashangaza! Hekaheka zote zilikuwa za nini? Mambo ya nchi hii ni ya ajabu kweli, mtu anaandamwa na vyombo vya dora kwa nguvu nyingi zaidi utafikiri marehemu Osama!! Inatia aibu kwa Hakimu Magesa na watawala kwa vitendo vya kudumaza demokrasia."They are often thinking in the box only" Hatutafika kama tabia hii itaendelea. Vyama vyote ni vyetu,vipo kwa ajili ya watanzania.Kama mmezidiwa kwa sera endeleeni kujipanga zaidi.Mmeshajivua Magamba! na bado tatizo lipo! basi fanyeni kujichuna magamba ili mbaki na nyama tu!!!!!!!! muone tena kuna tija au la mwendele na hatua nyingine.Nakutakia maisha marefu Freman Mbowe katika hekaheka na misukosuko unayoipata.Ni wachache wanaoweza kuthubutu.Umethubutu!!!!!!!!!!:majani7:
 
HTML:

Hivi yale magari ya washawasha yako mangapi nchi nzima? maana ukiyalipua hayo, polisi hawana nguvu tena (just thinking twice)[/QUOT

Wanapoteza pesa nyingi kununua magari ya maji ya kuwasha badala ya kununa magari ya zimamoto!
 
Elewa topic kwanza mkuu...
Sijamfananisha na Mtikila, wala sijasema yeye ni maarufu kuliko mtu yeyote Tanzania
Unaelewa maana ya umaarufu?
Kuna watanzania wangapi leo wako rumande? au wanasafirishwa kwenda mahakamani? au wamesomewa mashitaka?
Naomba utumia kamusi yako kuangalia maana ya neno 'umaarufu'...

ningekuwa mimi nisingemjibu huyo jamaa maana kichwa chake kina uzito wa ubongo usiotumika, laiti kama angejua wamarekani wananunua unused brain angejaribu japo kidogo tu kuutumia ubongo wake kabla hajajibu.
 
Nilianza kumsikia kwa mbali alipochaguliwa kuwa mbunge Hai mwaka 2000

Alipata umaarufu zaidi alipochaguliwa kuwa mwenyekiti wa CHADEMA (2004?)

Alipata umaarufu sana alipogombea uraisi mwaka 2005, zaidi kwa kuanzisha styles za helkopta na magwanda, ambazo ni maarufu hadi leo

Alikuja kuvuma tena sana wakati wa operesheni sangara.

Katika uchaguzi uliopita, hakuvuma sana (kwa sababu ya kuwepo Slaa katika uraisi?)

Alikuja kuvuma zaidi wakati wa kuundwa kwa kambi ya upinzani

Aliendelea kuwa midomoni mwa watanzania katika matukio tofauti kwa kiwango tofauti hadi Ijumaa tarehe 3 June 2011

Kwa siku tatu mfululizo Kuanzia Ijumaa jioni, hadi leo asubuhi, Freeman Aikaeli Mbowe amengeza mstari mwingine katika historia yake ya kupigania wanyonge Tanzania. Mstari ambao kwa wanaofuatilia vyombo vya habari na kusikiliza maoni ya watu ya kisiasa, bila shaka unastahili kuandikwa bolded zaidi, na kwa font kubwa zaidi, angalau kuliko mistari yote iliyowahi kuandikwa siku ya nyuma...


Mzee naona umepost,na inasomeka!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! vipi unatizama tumechangia wangapi huu upupu?
 
Wengine tuko kwenye vita ya kuikomboa nchi yetu. Kulala sakafuni ni jambo la kawaida sana, tunalitegemea na tumeshalizoea. Heshima unaipata kwa watu wanaokuheshimu. Kuna tofauti kubwa sana kati ya kukocholewa na kichaa na kukocholewa na mtu mwenye akili timamu analujua analolifanya. Na kwa taarifa yako CCM inahusika sana na hili jambo kwa kuingilia kazi za mahakama. Order ya kukamatwa Mbowe imetoka Lumumba.

Hebu iweke jamvini hiyo order ya kukamatwa Mbowe iliyotoka Lumumba. Na huna sema huna hapa hapa !
 
naunga mkono hoja.maana hapa nilipo sina la kufanya labda nikapoteze muda kwenye maandamano, ingawa najua ni ya kijinga tu.ila ukweli ni kwamba wana cdm huwa tuna muda wa kupoteza na hatuna ubinadamu hata kidogo, tumetoka ktk uchaguzi juzi tu wananchi wametukataa kwa kishindo huu ni uzuzu ndugu zangu wana cdm.tuache wivu kikwete ndie rais wetu kwa miaka 5 ijayo, tujipange uchaguzi ujao sio mbali ndio demokrasia hiyo au sialaa anazeeka?...hahahahaaaaaaaaaaaa
 
Sipendi kuamini kwamba unauelewa finyu kiasi hiki kuhusu chaguzi zetu. Kuna mada nyingi sana hapa JF zimeongelea hili, ZISOME. Nina majibu yanayotosha kuandika kitabu lakini nitakujibu very briefly.

Napenda unijibu haya yafuatayo kwa ufasaha :
1. Kura zinaibwaje ?
Kada wa CCM kuwapigia kura wasiojua kuandika..., Mawakala kuhongwa kukubali matokeo feki, Maboksi ya majimbo yenye ushindi kusafirishwa kwenda kuhesabiwa kwenye majimbo mengine....

2. Kura zinachakachuliwaje ?
Msimazi wa uchaguzi kutangaza matokeo bila kuhesabu kura. Mfano Sumbawanga mjini, Shinyanga mjini, Vunjo etc. etc.

3. Kura zinalindwaje ?
Waulize watu wa Nyamagana, Ubungo, Kawe, Arusha mjini, etc watakuambia.
 
wee unapimaje umaarufu,mbona alikua rumande sasa amepiganiaje hiyo haki,na kama ni hivyo kuwekwa rumande ndio umaarufu basi mch. mtikila ndie jembe zaidi kuliko yoyote tanzani.

Yawezekana ukawa sahihi, katika mapambano ukishinda unaitwa shujaa, ukishindwa unaitwa mhalifu, Nelson Mandela alihukumiwa kufungwa na akatumikia miaka zaidi ya 20, akiwa kifungoni aliitwa ni haini, alipotoka na kufanikiwa alichokuwa akipigania akaitwa shujaa. Wanaopindua Serikali wakifanikiwa huitwa mashujaa, wakishindwa huitwa wahaini, lakini kwa sababu wale waliopo madarakani ni wakoloni weusi, wameacha kutekeleza katika kwa kuhakikisha ustawi wa wananchi bali ni ustawi wa wageni na kuweka maakaunti yao nje naamini kuna siku nchi hii itapata uhuru wa kweli. Si lazima awe Slaa au Mbowe hata ndani ya CCM imani yangu wanaweza kutokea. Namwomba MUNGU muumba wa mbingu na nchi atuwezeshe kumtambua huyo na kundi lake.
 
nani asingekaa?? msitume post hizi mkiwa kilwa, bado kama kufa wangekufa wananchi tu, in the name of politics, mtu kafanya uzembe wa kutoenda mahakamani, watu kama wewe wanarukaruka wakisema ni mpambanaji! you have to think twice!

muda umepotea bure na situation kama hizi two things may happen, credibility ya chama kupanda au kushuka vibaya mno!

guess what??

Weeee mtu wewe, kuna wazembe wangapi waliosababishia taifa hasara isiyoelezeka hawajachukuliwa hatua yoyote? au bado mnatafuta ushahidi?
 
nani asingekaa?? Msitume post hizi mkiwa kilwa, bado kama kufa wangekufa wananchi tu, in the name of politics, mtu kafanya uzembe wa kutoenda mahakamani, watu kama wewe wanarukaruka wakisema ni mpambanaji! You have to think twice!

Muda umepotea bure na situation kama hizi two things may happen, credibility ya chama kupanda au kushuka vibaya mno!

Guess what??


kwani mheshimiwa mboe angetoa taarifa angepungukiwa na nini? Anjisikia tu kuleta tension na watu kumbabaikia.watanzania tufikiri vizuri huyu jamaa ni mbinafsi !!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Hatufai
 
Ametusababishia walipa kodi hasara kubwa apelekewe Invoice ya gharama,
 
Jamani kila wakati nawaza sana kuhusu jeshi la polisi la tanzania. Mbona watumia zaidi nguvu kuliko hekima, akili, na busara. Kushika kwao silaha ndo washindwe hata kufikiri basics. Kama mh. mbowe aliripoti mwenyewe, polisi, walimshikilia ili nini? Je mbowe ni mtu anayeweza kukimbia? Je walishindwaje kumwamuru jumatatu ariport mahakamani badala ya wao kumshikilia na kumsafirisha na ndege binafsi ya kukodi? Ili jeshi limejaa watu ambao hawana shule, na failures wengi, wengi waliopata sifuri (0) form IV na form VII. Hili jeshi linafanya faulu sana katika mambo mengi ikiwa ni pamoja na mauaji ya Arusha, tarime, nk.

Nchi nzima watu walikua kwenye tension kwa sababu ya ujinga wa Kova. Hatuna jeshi bali kikundi cha wahuni na wezi
 
Ukijadili elimu ya wamasai (kama kweli hawajaelimishwa vya kutosha) usimsahau Olaigwanani Lowassa ambaye kwa miongo miwili sasa amekuwa akiwatumia kuvuna kura na kupata fursa ya kuja kufisidi mali za Taifa huku akiwaacha bila hata shule au malambo ya maji au malisho kwa mifugo yao. Kazi kuwaambia Tobiko, Tobiko huku wao wakizidi kuwa maskini wa kutupwa na yeye akinunua mitaa huko London!
 
Mzee naona umepost,na inasomeka!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! vipi unatizama tumechangia wangapi huu upupu?
Natumaini ukujua kama nawewe umeongeza title ya Mh mbowe kwa ulichopost.Ata Yuda alimtangaza Yesu kwa alilofanya .Hili andiko litimie Mh mbowe kafanyiwa vile .
 
Kwa kweli baada ya kukamatwa na kuanchiwa leo, nimemvulia kofia. He is the man and the government and police are ....
 
wee unapimaje umaarufu,mbona alikua rumande sasa amepiganiaje hiyo haki,na kama ni hivyo kuwekwa rumande ndio umaarufu basi mch. mtikila ndie jembe zaidi kuliko yoyote tanzani.

Mandela, mmoja wa watu maarufu sana duniani, amekaa gerezani miaka 27. alifungwa na utawala kandamizi. ni sifa ya tawala kandamizi kunyamazisha watu kwa kuwatia rumande, kuwatia mbaroni, na kuwanyanyasa kwa njia mbalimbali. kuwwekwa ndani au kutiwa rumande au hata kuhukumiwa kifungo, haina maana kwamba huyo mtu hafai. inategemea na mamlaka inayomhukumu, na inategemea kafanya nini. unaweza ukawa unaandika tu kwa ushabiki wa juu juu, bila kuchambua mambo. lakini cha msingi ni wale tu ambao sio waoga, hawaogopi hata maguvu ya serikali kandamizi, ndio wananchi wanawahitaji hasa wakati huu. kama wewe unaogopa sana na unaona unadhalilishwa sana kwa kutiwa mbaroni mpaka uogope kufanya au kusema unachoona kinasogeza mbele mapambano ya kudai haki, basi kaa pembeni
 
Nakubaliana na wewe Mkuu, CCM hawasomi alama za nyakati, wanatumia vyombo vya dola wakidhani wanammaliza kisiasa CDM kumbe wanapandisha chati........Peoples'........!!!

tatizo JK anadhani mtu akiwa na kipara basi ndo ana maarifa ndo maana kamchagua MUKAMA..sasa huyu mukama ndo anamdanganya na ma strategy ya kizamani matokeo yake wanaaibika bila kujijua ...yaani hovyo tupu
 
Back
Top Bottom