Hatimaye Mbowe apewa dhamana

Hatimaye Mbowe apewa dhamana

Sidhani kama katika jeshi la polisi la ccm kuna mtu wa kuyafikiria hayo wala katika mahakama hakuna mtu wa maana wa kutoa constructive ideas kama hzo. Tunashukuru kwa wanataasisi kma hawa kwa michango yao ya kimawazo ya kuwaamsha ipo siku watakumbuka shuka wakati kumekucha.
Uwezo wa hawa waheshimiwa wa kufikiri ni finyu saana, kwa nchi masikini yetu kama hii Tanzania utumie gharama zote hizo kubebana na mtu ambaye si jambazi sugu labda anaweza kutoroka. Kweli inaingia hakirini kweli hiyo??????????? Magari kwenda Air Port Ukonga, ndege Dar to KIA or Ars Aport, magari mahakamani yote hiyo ni gharama kwa mwananchi wa Tanzania!!!!!!!!! Hivi Watanzania wamekosa nini kwa Mungu wapewe adhabu za aina hii. Si busara zitumike ingawa kiasi jamani????????
 
Dondoo za yaliyojiri kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi, Charles Magesa Arusha leo

Hakimu Magesa alisema ni kweli mahakama iliruhusu washitakiwa wabunge wahudhurie kikao cha bunge la bajeti na hivyo hawana tatizo na Mh. Mbowe, ila kutokana na kukosekana kwa mdhamini wake, ndiyo sababu walitoa amri ya kukamatwa kwake.

1.Hakimu amesema mahakama inaendelea kuwapa ruhusa washitakiwa wote ambao ni wabunge kutohudhuria mahakamani hapo hadi pale ambapo kikoa cha bunge kitamalizika ila aliwasisitiza wadhamini wa washitakiwa kuhudhuria mahakamani kila siku ambapo tarehe ya kesi imepangwa


2.Wakili upande wa Utetezi, Method Kimomogoro, aliiomba Mahakama kuondoa amri ya kukamatwa kwa Mbowe na kutaka apewe dhamana yake ya awali, ili aweze kuhudhuria vikao vya bunge la bajeti ambalo yeye ni kiongozi wa kambi ya Upinzani na kwamba mdhamini wa Mbowe hakufika mahakamani kwa kuwa alisahau, na hiyo ipo kwa kila mtu na hata wao kama mawakili wanasahahu tarehe za mahakamani.


3.Mdhamini wa Mbowe bwana Julius Margwe alizitaja sababu za kutofika mahakamani Mei 27, 2011 ni kutokana na kuwa na kesi Mahakama ya Mwanzo Maromboso. Pia, hakufika Mahakamani Mei 30, 2011 kwa sababu mahakama haikumpa nafasi kusema lolote.


4.Wakili wa Serikali Juma Ramadhani, aliiomba mahakama hiyo itoe onyo kali kwa mshitakiwa kwa kutofika mahakamani hapo na pia kumtaka mshitakiwa huyo na wenzake wawe na mawasiliano ya karibu na wadhamini wao, ili wasikosekane wanapotakiwa mahakamani hapo, pia, mdhamini wa Mbowe hana uhakika na hajui nini anafanya, hivyo hafai kuwa amdhamini.


5.Hakimu Magesa akasema Julius ana makosa mengine yanayomkabili na hata hawezi kujieleza, hivyo Mahakama haina sababu kuwa naye sababu tayari ana kesi ya jinai ambayo hatma yake haifahamiki.


Mahakama imemkubali mdhamini mwingine ambaye ni John Bayo, Diwani wa kata ya Elerai (CHADEMA).


Baada ya Freeman Mbowe, kuachiwa huru na aliwashukuru wananchi na kusema anasikitishwa sana na kutumia nguvu kubwa kumlinda yeye na kumsafirisha usiku akiwa chini ya ulinzi mkubwa kama kwamba yeye alikuwa ni gaidi ambaye alikuwa na silaha, "Mimi nilijipeleka mwenyewe polisi sasa kama kweli ningekuwa wa kukimbia ningejipeleka?

Sasa wao hawajaona hayo yote haitoshi wameamua kutumia nguvu kubwa sana maana wakati wakinipeleka uwanja wa ndege walikuwa na polisi wengi sana zaidi ya 50 yaani utadhani ni gaidi anapelekwa alafu ndege ya kubeba watu mia ndo wameniweka mimi, wakati hayo mafuta wangeyaweka ata kwenye kutengeneza vitanda vya hospitali.

Wanatumia vibaya kodi za wananchi "alisema Mbowe. Alisema kuwa Serikali ilitumia ndege ya jeshi, ambayo ina uwezo wa kubeba watu 100, ambayo ilichukua watu watatu yaani yeye, Kamishina wa Polisi kanda kanda ya Ilala na Kamishna wa Polisi wa kikosi cha kuzuia ghasia wa Tanzania hadi KIA usiku wa majira ya saa 9.00.

Pia alisema mbali na kusafirishwa kwa ndege hiyo kubwa, pia kulikuwa na magari nane ya FFU ambao walikuwa na mabomu na silaha kama wanasindikiza mhalifu. Akashukuru Polisi kutomfanyia unyama wowote, walikaa naye vizuri, isipokuwa alinyimwa haki yake ya msingi ya kuwa na uhuru wa kuwasiliana na watu.

Mara baada ya kesi hiyo kumalizika wananchi walimbeba kiongozi waho kwa juu huku wakiimba.
Kesi ilihudhuriwa na wabunge 13 wa CHADEMA ambao ni Zitto Kabwe, Halima Mdee, Godbless Lema, Suzan Kiwanga, Ezekia Wenje, Christina Lissu, Paulina Gekulu, Israel Natse, Suzana Lyimo, Joseph Mbilinyi, Rahya Ibrahimu ( Mbunge toka Pemba), Joyce Mukya na Joseph Selasini.


SOURCE:
Wavuti - Home
 
Amesafirishwa usiku usiku

Kwa gharama za watanzania unatumia ndege inayochukua watu 100 kumpeleka mtuhumiwa 1 polisi 2 wanao msindikiza hd Arusha ThinkTwice :becky:unachekelea angalia ni hasara kiasi gani imepatikana kwa kuingiza siasa kwenye issue zisizo stahili?

Magamba magamba magamba magambaaaaaaaaaaaaaaa!
 
Limbukeni mkubwa wewe dhuruma ya CCM ndiyo imewafanya kuwa hivyo ndugu zetu wengi
 
Wanadhani wanamkomoa Mbowe, wanadhani wanafifisha umaarufu wa Cdm, wrong calculation. . . . . Wanaishi kwa mbinu na mitazamo ya kale sana.
 
At least Kimomogoro amekuwa muungwana kukiri kwamba mteja wake alisahau, which means kwamba kulikuwa na kosa ambalo mteja wake amelifanya na kwamba huo ni utetezi. Sasa uropokaji wa kudai kwamba mara ooh kuna udini, eti ooh kuna mkono wa jaji mkuu na mchanyato mwingine wa kijinga ulitokana na ushabiki tu! I pity them!
 
Chama cha wanasheria Tanzania (Tanganyika Law Socitiety - TLS) kimesema mahakama haikutumia busara kwenye suala la Mh. Freeman Aikael Mbowe. Rais wa Chama hicho Francis Stolla akizungumza na Radio Sauti ya Ujerumani (Deutsche Welle) alisema katika kipindi hiki ambocho bunge la bajeti linakaribia mahakama ingeweza kusubiri mpaka shughuli ya bunge iishe kwani Mbowe ni mtu anayeweza kupatikana.

Aidha amesema hata polisi hawakutumia busara kutomwachia mapema na kumtaka aende mahakamani yeye mwenyewe, kwani ni mtu anayejulikana na si mhalifu sugu.

kweli bana big up tls
 
Duh, hii ni nchi ya kijeshi na yenye vipaumbele vyenye kuleta maendeleo kwelikweli kwa wananchi. Hii ndio TANZANIA YENYE NEEMA ambayo tuliahidiwa wakati wa kampeni!!!!
 
mAGESA NI MPUMBAVU

Kiwango cha upumbavu wa Magesa (kama anao) hakiwezi kuzidi chako wewe unayedhani kwamba mtu akiwa kiongozi wa CDM basi ana kinga dhidi ya hatua zinazotokana na ukiukaji wa sheria. Yeye alikataa kwenda kwa hiari yake na sasa amelitia hasara Taifa. Huyu aliyelazimisha hazina ya Taifa kutumika kumsafirisha kwenda kuitikia wito halali ndiye wa kulipa fidia!
 
Sijapenda ndoto niliyoota leo. Eti nimeota ndoto kwamba Polisi wakiwa wanamsafirisha Mbowe njiani walimpiga sumu ya Kumuua taratibu in some few years to come bila yeye kujijua. Kama kuna roho kama hii ishindwe

Watu wamechoka na mfumo uliopo, hivyo tatizo siyo Mbowe. Wazo la kumuondoa duniani mbowe halitamaliza mchakato wa mabadiliko uliokwisha anza. Ni vema vibaraka wa wagandamizaji wa watanzania waelewe kuwa, It is just a matter of time. Wahenga wanasema: KARIBU NA MAPAMBAZUKO GIZA HUWA LINAKUWA NENE!

Mtu asipoiunga mkono CDM, akumbuke kuwa penye haki, Bwana aweza kuinua hata mawe yafanye hivyo.

peopleees Power!!!!!!
 
Mungu ibariki Chadema,Mungu ibariki tanzanIA MUNGU IBARIKI AFRICA.
 
Wajameni huyu malaria sugu ni kichaa anayejua kuandika kwa kutumia computer mazeee!!!shauri yenu nyie hamuoni ni akili za makalioni hizo??
 
Duh, wewe kweli hujui ku analyse mambo, hiyo ni kinyume chake sasa ! Jamaa wamemdhalilisha sana na hata wabunge wenyewe wamesema. N aelewa kuwa suala la bajeti ni suala la bunge sio la mbowe, sasa hapo pipoz powa inahusika vp?. Jamaa wamemkamata kama ndege, wameenda kumlaza sakafuni, wamemsafirisha usiku hakupata usingizi huoni heshima imepungua?. Na isitoshe hili ni suala la kisheria wala CCM haihusiki hata chembe, wenzake wao walienda mahakamani wakamdanganya mwenzao amedhalilika sana .

Tanzania bado tunaendekeza mambo ya "uchekbob/sista" sana. sasa utakuwaje kiongozi unayependa mabadiliko kama unaona kulala chini is a big thing. Hivi kuna mkombozi wa nchi yeyote ambaye hakulazwa chini/kuzalilishwa? Mkuu, we uko Dar nini? Huko ndio watu wanaendekeza usopu sopu badala ya uzalendo. If that is what cost kwamtu kupata haki yake why not???? Kwamtazamo mwingine hili tukio lilikua ni lazima litokee kwa kiongozi mmoja ili nchi ijidhihirishie how vyombo vya dola visivyojua Sheria. Nimesoma magazeti leo na kama yaliyoandikwa ni kweli basi hakimu Magesa amechemsha big time. Labda ni wakati pia wakujiuliza kuhusu tukio la Zitto. Inakuwaje sheria inamruhusu mtu kufanya mkutano mpaka 12.30, wewe unamkamata 12.20? Alafu bado kweli polisi wanahitaji kuheshimiwa? Utamuheshimu vipi mtu wakati unajua hajui na hataki kukubali kama hajui?
 
Walizoea sana kukandamiza vyama vya upinzani! Na kwa sababu kulikuwa hakuna watu wa kuwa challenge upinzani uliendelea kuwapigia magoti na kuwasujudia kama miungu. Zama hizo zimekwisha!!! Huu ni wakati wa ku-tweet, ku-facebook. Tunachota ni fair game! Mkienda kinyume na utaratibu uma utawa-hold reponsible. Mbowe, au Zitto au Dr Slaa sio individuals, ni CHADEMA na CHADEMA ina wenyewe!
 
wananchi wa Tanzania wanataka kuona MAPACHA watatu wanakamatwa, wanafikishwa mahakamani, ushahidi unatolewa(upo) na mapacha watatu wanahukumiwa.
wananchi hawako tayari kuona mtu anaye wapigania(Mbowe), anakamatwa huku mafisadi wakidunda vifua mbele na kuendelea kutoa maneno ya kashfa mbele ya wananchi waliowaibia. Hiyo si haki.
 
Kuna watu wanaongea tu nchi hii. Nadhani na Rais wetu sasa hili suala la kuongea kwa mazoea aliache. Mbona alituomba majina ya wafanyabiashara wa madawa ya kulevya tukampa halafu hajamtaja hata mmoja. Sasa inakuwaje anakwenda kwa maaskofu na kuwaambia wanauza unga.
Tena naomba viongozi wa dini watoe tamko kuhakikisha kuwa wao hawauzi unga. Otherwise, Rais awataje kwa majina hao wauza unga wao.
 
Back
Top Bottom