Hatimaye Masauni - UvCCM Ang'atuka

Hatimaye Masauni - UvCCM Ang'atuka

Kama kijana ameweza kung'atuka atakuwa amemdhalilisha sana Mkulu kwa kushindwa kuchukua uamuzi ambao kijana mdogo amechukua, kwa hali ilivyo sasa ndani ya CCM, ni dhahiri JK alitakiwa awe tayari amejiudhuru nyazifa zake zote katika chama
 
Kama Masauni alighushi vyeti hapa kuna kosa la jinai.

Pia UVCCM inaonekana ni dhaifu,does it mean kwamba hawakujua hilo muda wote huu?

Kitu kingine,nadhani UVCCM inatumika vibaya.ridhiwani ana historia ya kutaka kuburuza watu since akiwa UDSM.

Nadhani udhaifu wa UVCCM unaweza kuwa adavantage kwa vyama vya upinzani.BAVICHA wajipange vizuri,wawe na ushawishi ndani ya chama.BAVICHA ikiweza kuwa na ushawishi na nguvu kuliko UVCCM,basi CHADEMA watakua na nguvu kubwa sana,na hata kunufaika na Migogoro mikubwa ndani ya UVCCM.

Kwa kweli UVCCM wanajimaliza wenyewe,wanajua kutumia mbinu chafu tu katika siasa zao.Hawatafika mbali
 
Mkuu FEMS uko wapi?tunahitaji dataz za jikoni maanke huwa nakuaminia sana mwanawane.Plz jitokeze,kipindi muhimu sana hiki!

Let me hope uko poa wherever you are!
 
Lazima mjue kuwa UVCCM ni daraja na ni kituo. Ni daraja la kuvukia kule ambako mtu anataka kwenda kisiasa ndani ya CCM. NI mahali ambapo viongozi wapya wa CCM hutengenezwa, hujaribiwa na hatimaye huvutwa ndani. Hili limetumika tangu zamani na hivyo vijana wengi wa CCM wanajua kabisa ili waweze kupata nafasi huko mbeleni ni lazima siyo tu wapitie UVCCM lakini wapate nafasi za uongozi... inawakumbusha juu ya EN.

Lakini vile vile ni kituo cha mapumziko. Hapa ni mahali pa kusubiria ili muda ukifika mtu aende kwenye kile anachokitaka hasa. Tatizo ni kuwa UVCCM inaanza kuhusiana sana moja kwa moja na establishment ya CCM kuu kiasi kwamba kuna influence ya ajabu kutoka kwa 'wazee' kwenye UVCCM. UVCCM siyo huru tena na haiwezi kufanya mambo yake kwa uhuru kama ilivyokuwa zamani. Hivyo mgongano ni lazima.

Njia pekee ni kwa UVCCM kuwa kweli taasisi ya vijana wa CCM nje ya kucha za wakubwa. Waweze kufanya maamuzi yao hadi ya mwisho bila kuingiliwa na Kamati Kuu wala nini. Hapo ndipo vijana wa CCM wanaweza kweli kufanya mambo yao bila mizengwe.
 
Lazima mjue kuwa UVCCM ni daraja na ni kituo. Ni daraja la kuvukia kule ambako mtu anataka kwenda kisiasa ndani ya CCM. NI mahali ambapo viongozi wapya wa CCM hutengenezwa, hujaribiwa na hatimaye huvutwa ndani. Hili limetumika tangu zamani na hivyo vijana wengi wa CCM wanajua kabisa ili waweze kupata nafasi huko mbeleni ni lazima siyo tu wapitie UVCCM lakini wapate nafasi za uongozi... inawakumbusha juu ya EN.

Lakini vile vile ni kituo cha mapumziko. Hapa ni mahali pa kusubiria ili muda ukifika mtu aende kwenye kile anachokitaka hasa. Tatizo ni kuwa UVCCM inaanza kuhusiana sana moja kwa moja na establishment ya CCM kuu kiasi kwamba kuna influence ya ajabu kutoka kwa 'wazee' kwenye UVCCM. UVCCM siyo huru tena na haiwezi kufanya mambo yake kwa uhuru kama ilivyokuwa zamani. Hivyo mgongano ni lazima.

Njia pekee ni kwa UVCCM kuwa kweli taasisi ya vijana wa CCM nje ya kucha za wakubwa. Waweze kufanya maamuzi yao hadi ya mwisho bila kuingiliwa na Kamati Kuu wala nini. Hapo ndipo vijana wa CCM wanaweza kweli kufanya mambo yao bila mizengwe.

Nadhani hiki ndicho alichokua anajaribu kufanya huyu jamaa,masauni .Ingawa pia naona na yeye hafai kama kweli alifoji miaka.

Pia UVCCM imepoteza mwelekeo kutokana na watu wazima wanaotaka kugombea nafasi za juu,hao wanajua nguvu ya UVCCM.

Pia ukitaka kuingamiza CCM anza na UVCCM....................
 
HUYU kIJANA MASAUNI NI MJEURI SANA,MAJIVUNO,MBINAFSI EBU MUULIZENI YULE DEREVA WAKE ANAYESIHI KAWE NAMANA ANAVYONYANYASIKA NA MASAUNI, WANAPOKUWA DAR INAFIKIA WANAZUNGUUKA NA GARI MPAKA SAA NANE ZA USIKU, DEREVA ANAMRUDISHA HOTELINI MASAUNI ANAMWAMBIA DEREVA, OK ACHA GARI HAPA, UWAHI KESHO USUBUHI BILA KUMPA SENTI KA KUPANDA TAX,KUMBUKA DEREVA WAKE ANAISHI KAWE .. HUYO NDIE MASAUNI AHHH!!! ANAKERA KINOMA DOGO HUYU MWENYE UMRI TOFAUTI.

dogojk%5B1%5D.jpg

Mwenyekiti wa CCM Taifa Rais Jakaya Kikwete

DSC09219.JPG

Wajumbe wa baraza wakisikiliza kwa makini kikao cha baraza ambacho kinadaiwa kuwa moto kwa mwenyekiti wa UV-CCM Hamad Yusuph Masaun ambae ametangaza kujiuzulu usiku huu

DSC09227.JPG


DSC09220.JPG

Wajumbe wa baraza wapigwa na butwaa ukumbini

Mpenzi mdau wa mtandao huu habari hii ni kutoka ndani ya kikao hicho ambapo inadaiwa kuwa mwenyekiti wa UV-CCM taifa na makamu katibu wa UV-CCM Bw.Moyo wamejiuzulu nafasi zao ,hizo ndizo tetesi za uhakika kutoka ndani ya kikao hicho japo ukweli halisi utaupata mapema asubuhi ili kujua sababu hasa na maelezo yao kabla ya kujiuzulu kwao japo Masauni ni juu ya sakata la kudaiwa kufoji veti huku Moyo ni hatua yake ya kuendeleza makundi Visiwani

DSC09235.JPG


Habari hizi ni kwa msaada wa Blog ya Francis Godwin[/QUOTE]
 
Kama hakushinikizwa kujiuzuru kafanya uamuzi wa busara kwa kutambua umuhimu wa UWAJIBIKAJI...lakini hiki chama kinashangaza sana!!! kuna viongozi wameliingizia taifa hasara ya mabilioni lakini wanaangaliwa tu...inasikitisha sana
 
Kama UVCCM ndio inategemewa kuandaa viongozi wajao wa Taifa, basi tujiangalie vizuri. Naona kama waliojaa kule sio viongozi, bali ni opportunist ambao wanasubiri wakati muafaka ufike ili neema zianze kuwafunukia. Taifa hili liko kwenye mgogoro mkubwa wa kupata viongozi wa uhakika.
 
hili ni doa kubwa kwa mkuu wa kaya yetu- tatizo mbishi sana.na sio makini kuchumba issues,yeye ukurupuka tu.basi na ampe mwanae tuone.
 
SIKU moja baada ya Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM), Hamad Masauni Yussuf kuachia ngazi wadhifa huo, baadhi ya vijana wa jimbo la Kikwajuni warejesha kadi za CCM kutokana na kutoridhishwa na suala hilo.

Viongozi wa CCM Jimbo la Kikwajuni jana walikataa kusema lolote kwa madai kuwa wao hawajui kinachoendelea zaidi ya kupata taarifa hizo kwenye magazeti na walipotakiwa kuelezea uamuzi wa Vijana kurejesha kadi walisema "hatujawaona, lakini kwa vijana hilo linawezekana" Alisema Kiongozi Mmoja wa Jimbo hilo ambayer hakutaka kutajwa hata cheo chake.

Baadhi ya viongozi hao walionekana wakisoma gazeti la Mwananchi na kusema kwamba ndio kwanza wamepata gazeti hivyo hawezi kutoa ufafanuzi wowote kuhusiana na suala hilo lakini wanachokijua huo ni uamuzi kutoka ngazi ya juu ya vijana.


"Sasa hivi ndio nilikuwa na gazeti hapa lakini sijawahi hata kulisoma nimenyanganywa kuna vijana wanalisoma huko kwa hivyo hatujajua chochote hadi sasa lakini hata kama ndio amejiuzulu huo uamuzi ni wa vijana sisi kama chama hatujaletewa taarifa zozote zinazomhusu yeye ni mambo yao vijana" alisema Katibu wa jimbo hilo la kikwajuni.


Mbali na suala hilo, pia imebainika kuwa mabadiliko mbali mbali yaliyofanywa na Masauni ikiwemo uhamisho wa mke wa Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Shara Saleh Ferouz uliwachukiza baadhi ya vigogo wa CCM Visiwani humo.


Mke wa Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar ni Afisa Mwandamizi wa UVCCM Afisi Kuu Visiwani hapa ambaye hata hivyo amerudishwa Afisi Kuu, ingawa si kwa nafasi yake ya awali.


Habari zaidi zilizopatikana jana Mjini hapa zinaeleza kwamba jambo kubwa lililomponza Masauni ni pamoja na kutajwa kwake kuwania Jimbo la Kikwajuni sanjari na hasimu wake, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Saleh Ramadhan Ferouz ambaye ni mtu wa karibu na Naibu Katibu Mkuu wa UVCCM aliyeachia ngazi, Mohammed Nassor Moyo.


Imeelezwa pia baadhi ya vigogo wa CCM Visiwani wanatajwa kuhusika na vuguvugu la kumwondosha Masauni, ingawa wao walikaa kando wakiwachochea na kuwasukia mkakati ‘vibaraka' wao ndani ya Umoja huo ambao wameathirika na uongozi wa Masauni.


Jana katika maeneo mbalimbali ya Jimbo la Kikwajuni vijana walionekana wakiwa kwenye vikundi vikundi wakitafakari hali iliyotokea ambapo katika Afisi za CCM hali ilikuwa ni tofauti na siku nyengine viongozi walikuwa katika wakati mgumu wa kutoa ufafanuzi.


"Tatizo hapa ni Ubunge Kikwajuni…huyu Masauni anachuana na Ferouz (Saleh Ramadhan Ferouz), lakini hata kama Masauni ameacha Uenyekiti haitofanya mabadiliko yoyote Jimboni" Kilisema chanzo kimoja Jimboni humo.


Katika hatua nyengine, zipo taarifa kwamba Vijana wa Zanzibar wameandaa mapokezi makubwa kwa Mwenyekiti aliyejiuzulu atakapowasili Visiwani hapa akitokea Iringa kwenye mkutano wa Baraza Kuu.


"Huu ni msiba wa Zanzibar nzima kwa kweli ni pigo hawa vijana alikuwa ni hodari kwenye kazi za Chama na nje ya Chama, lakini kwa kila aliyefanya fitina hii Mungu atamlipa" Alisema Kada mmoja wa CCM.


Katika mitaa mbalimbali ya Unguja, wengi walisikika kusikitishwa na hali iliyotokea ndani ya Umoja wa Vijana wa CCM ambapo waliwashambulia wale wanaotajwa kuchochea vurugu katika Umoja huo.


Masauni alikuwa Mwenyekiti wa pili Mzanzibari kukalia kiti cha UVCCM, mtangulizi wake Mzanzibari mwengine ni Muhammed Seif Khatib ambaye kwa wakati mmoja alikuwa Mwenyekiti na Katibu Mkuu.


Taarifa zaidi zilizoenea hapa zinadai kwamba makundi ya wagombea Urais Zanzibar nao wanatajwa huenda wamehusika katika mbinu za kumwondoa Masauni ambaye walimuona kuwa na msimamo usiotabirika kwao.


Source: Zanzibar yetu web blog
 
Tulipokwambieni mnatumiwa tu na manya'nganyi kwa faida ya matumbo yao mlituona maadui wa nchi na watafuta vyeo, haya sasa mmeona mlipofikishwa CCM si chama chenu vijana wa Zanzibar, hasa Unguja, ni chama cha manyan'ganyi na majizi yanayotumia vibaraka wao Zanzibar kuifisidi nchi, hamjachelewa rudini kundini tuendeleze mapambano.
 
Hizi ndio siasa za bongo,fitna tupu hakuna lolote.Sasa wekeni mpiga kampeni wa Bn,hili awe mwenyekiti.Wakazi wa znz dawa sio kurudisha kadi halafu kuwapa kura,kaa na kadi usiwape kura.
naogopa cctv.
 
Mpaka sasa hivi hakuna habari ya uhakika Masauni kajiuzulu kwa sababu gani.
Wengine kafoji umri, wengine fitna sijui tushike lipi!!
 
Hizi ndio siasa za bongo,fitna tupu hakuna lolote.Sasa wekeni mpiga kampeni wa Bn,hili awe mwenyekiti.Wakazi wa znz dawa sio kurudisha kadi halafu kuwapa kura,kaa na kadi usiwape kura.
naogopa cctv.
Tatizo ni kuba zaidi kwa sababu hata hii habari ya kurudisha kadi inaweza isiwe sahihi sana
 
Mungiki kenya ni vijana na makomandoo wa KANU baada ya kuwatelekeza wakageuka kuwa mungiki. Sioni sababu ya vijana naona nonsense wakati kiuhalisia umri wao ni uleule wa wazee, huku nikuongeza matatizo yasiyo na tija.

Pia yawezekana Masouni walimweka ili waje wamwoondoe kama ilivyotokea ili kuhakikisha mipango yao ya 2010.
 
Back
Top Bottom