Hatimaye makazi ya baadhi ya wakazi wa Kijijini Mbezi Beach B (Dar es Salaam) yavunjwa

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,460
1.JPG

IMG_2995.jpg
Serikali imetekeleza agizo la kubomoa makazi yasiyo halali katika eneo maarufu la Kijijini katika Kata ya Kawe, Mtaa wa Mbezi Beach B, Wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Mkuu wa Wilaya baada ya siku 14 za kuwataka kuhama kwa hiari kupita muda mrefu, huku wakazi wa eneo hilo wakiendelea kukaidi agizo hilo.

Utekelezaji wa zoezi la ubomoaji ulianza mapema alfajiri ya Desemba 9, 2023 bila kujali mvua kubwa iliyokuwa ikinyesha, huku likitekelezwa chini ya ulinzi mkali wa Jeshi la Polisi pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mtaa.

Wakati zoezi hilo likiendelea wakazi wa eneo hilo walisikika wakilia huku kukiwa kwenye hekaheka ya kujaribu kuokoa kinachowezekana bila kujali mvua kubwa iliyokuwa ikiendelea kunyesha alfajiri.
1111.JPG

11.JPG
Mmoja wa wakazi wa eneo hilo ambaye jina lake halikupatikana, alisikika akisema; “Wenyewe wanaitaka barabara yao, bora tungefanya wenyewe maana tuliambiwa ila ndio ubishi umetufiikisha hapa.

“Tumeponzwa na hawa viongozi uchwara, waliotuambia hatutaondoka sababu wao ndo “wenye duka (CCM)” Mkuu wa Wilaya ni msimamizi tu wa duka, sasa leo msimamizi wa duka ndio kasimamia duka, sasa hapo nani zaidi?” aliongea kwa hasira mwanaume huyo.

TimesMajira online ilishuhudia zoezi la ubomoaji likiendelea huku kukiwa na hekaheka za kuokoa vitu mbalimbali.

Katika ubomoaji huo, walikuwepo Wafanyakazi wa Halmashauri wakisimamia na kukusanya mabati na mbao na kupakia katika moja ya lori lenye namba za usajili SM12739.

Nao askari wa Jeshi la Polisi waliokuwa wakisimamia zoezi hilo walipoulizwa kuhusu mwenendo wa zoezi hilo, walisema hapakuwa na upinzani wowote, wala kizuizi chochote na kwamba wakazi hao walitoa ushirikiano kwa kukusanya wenyewe vitu vyao.

“Hakuna vurugu yoyote, hakuna upinzani wala aliyekaidi, sisi kama polisi tuko hapa kuhakikisha kuna amani na zoezi hili linakamilika bila ubishi wala kikwazo chochote” alisema mmoja wa askari ambaye hakutaka kutajwa jina lake kwa madai kuwa sio msemaji wa jeshi hilo.

Chanzo: Times Majira

Pia soma >

= Dar es Salaam: Wakazi wa Kijijini Mbezi Beach B wapewa Siku 14 Wahame
= Kijijini, Mbezi Beach eneo hatari Jijini Dar es Salaam
= Dar es Salaam: Wakazi Kijijini Mbezi Beach B waigomea Serikali kuhusu kuhama eneo hilo
 
Tumeponzwa na hawa viongozi uchwara, waliotuambia hatutaondoka sababu wao ndo “wenye duka (CCM)” Mkuu wa Wilaya ni msimamizi tu wa duka, sasa leo msimamizi wa duka ndio kasimamia duka, sasa hapo nani zaidi?” aliongea kwa hasira mwanaume huyo.

Sent using Jamii Forums mobile app
Alisikika Genta wa Jf akilia kwa uchungu 😂
 
Kwani si walisema wanaleta mganga wao awafanyie zindiko wasibomolewe!
Vipi naye kachomoa betri?
 
Waanzilishi wa eneo hilo ni wamakonde....
Huwezi ukazungukwa na mashuwa alafu katika kukawa uswazi
Nlisema humu wale lazima wataondoka

Ova
 
Hongera sana mkuu wa wilaya ya Kinondoni kwa kuipa heshima serikali kwa kusimamia sheria! Walisema huwezi sasa wamelipata somo kuwa “ Simba hachezewi sharubu”
Wakati huu karibu na uchaguzi wa serikali za mitaa, walinzi wa viwanja hasa huko Mbezi beach wanakuwa na miradi ya kuwarusu watu wajenge mabanda kando kando ya mto Ndumbwi na kuwatoza fedha nyingi; ambako hawana vyoo hivyo sio tu kuharibu Mazingira bali kueneza magonjwa kwani wanakunya hovyo mtoni!!
Mlinzi wa kiwanja cha Mama Maria Nyerere sehemu inaitwa “Rungwe” anatumia jina la huyu mama akishirikiana na Diwani wa Kawe kufanya uhalifu huu!
Hii sehemu inajulikana sana kuwa ni kijiwe cha uhalifu wa kila aina ikiwemo kuuza madawa ya kulevya ambayo Diwani wa Kawe ana husika!!
Ni vyema kama mkuu wa wilaya ya Kinondoni atalitupia macho eneo hili kwani limekuwa kero kwa majirani wakiwemo viongozi wakuu wa serikali!
Polisi wa Kawe wanafumbia macho uhalifu kwenye eneo hili kwani ni wanufaika na uhalifu huu.
 
Back
Top Bottom