mbezi beach

No Wikipedia entry exists for this tag
  1. Pdidy

    KERO DAWASA maji ya makazi mapya Mbezi Beach yana udongo mwezi sasa, nini shida?

    Nimejaribu kuwasiliana kiofisi nikahisi kuna marekebisho yanafanywa, sasa naona imekuwa kero. Wananchi wa makazi mapya Mbezi Beach wanateseka na maji ya udongo mwezi sasa. Kila bomba ukichota ndoo imejaa udongo, kutumia maji ni mpaka usubiri yatulie uchuje. Mnatupeleka wapi maana hatujui...
  2. A

    KERO Wakazi wa Mbezi Beach tunapata maji ya bomba machafu, na yana harufu mbaya. Mlipuko wa magonjwa unakuja

    Habari JF, Ni wiki na zaidi sasa maji yamekuwa yakitoka machafu hivi na wakati mwingine huwa machafu zaidi na yenye harufu mbaya. Niliuliza kwa mjumbe maana ni jirani yangu kama anakutana na tatizo hilo nikitaka kufahamu huenda ni mimi tu, naye akasema yapo hivyo na kwake pia (maji yalikatika...
  3. B

    KERO TANESCO na DAWASA mpaka mchukue roho zetu wakazi wa Mbezi Beach ndio mfurahi?

    Salaam kwenu wana JF, TANESCO na DAWASA mnatutaka nini wakazi wa Mbezi Beach? Umeme mnakata maji maji mmekata mnataka tuishije sisi? Mnaona raha watu tunavyosononeka na kutukana kila siku kwa hii dhulma mnatufanyia? Yaani hili fukuto ndani kukaa mateso nje huwezi kukaa mbu zikufanye chakula...
  4. 6 Pack

    Kwanini Mbezi beach imepoteza umaarufu wake iliyokuwa nao miaka ya nyuma?

    Habari wana jamii forum? Kuanzia miaka ya elfu mbili kushuka chini, eneo la Mbezi beach lilikuwa ni kati ya maeneo machache ya jiji la Dar es salaam ambayo yalikuwa na umaarufu mkubwa kama vile ilivyokuwa Masaki, Osterbay, Sinza nk. Hii ilipelekea watu wengi hasa wa mikoani wakisikia neno...
  5. JanguKamaJangu

    Hatimaye makazi ya baadhi ya wakazi wa Kijijini Mbezi Beach B (Dar es Salaam) yavunjwa

    Serikali imetekeleza agizo la kubomoa makazi yasiyo halali katika eneo maarufu la Kijijini katika Kata ya Kawe, Mtaa wa Mbezi Beach B, Wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Mkuu wa Wilaya baada ya siku 14 za kuwataka kuhama kwa hiari kupita muda mrefu, huku...
  6. JanguKamaJangu

    Dar es Salaam: Wakazi Kijijini Mbezi Beach B waigomea Serikali kuhusu kuhama eneo hilo

    Wakazi wa eneo la Kijijini lililopo katika Kata ya Kawe, Mtaa wa Mbezi Beach B, Wilaya ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam wamekahidi kuhama eneo hilo kama ilivyoamuliwa na Serikali. Wakazi hao walipewa siku 14 za kuhama eneo hilo kwa hiari na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Saad Matambule. Mkuu...
  7. JanguKamaJangu

    Dar es Salaam: Wakazi wa Kijijini Mbezi Beach B wapewa Siku 14 Wahame

    SERIKALI imetoa muda wa wiki mbili kwa wakazi wa eneo la Kijijini Kata ya Kawe, Mtaa wa Mbezi Beach B, Wilaya ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam kuwa ufikapo muda huo wawe wameondoka eneo hilo kwa hiari yao. Agizo hilo limetolewa mwishoni wiki iliyopita na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Saad...
  8. R

    Mbezi Beach eneo la wadosi na wakubwa lakini kipindi cha mvua ni kama kambale kwenye dimbwi la matope!

    Wakuu, Mbezi Beach inasifika kuwa kuwa na wadosi watu wazito na viongozi mbalimbali hasa upande wa chini. Lakini kipindi hiki cha mvua Mbezi haitamaniki, barabara za ndani ni mbovu kupita maelezo, yaani utafikiri uko pale urafiki wanapouza kwenye soko la ndizi. Kwa kwa jinsi Mbezi Beach...
  9. JanguKamaJangu

    Kijijini, Mbezi Beach eneo hatari Jijini Dar es Salaam

    Na Waandishi Wetu, TimesMajira Online, Dar es Salaam UKISTAAJABU ya Mussa Utayaona ya Firauni. Msemo huu unakamilisha picha halisi ya maisha ya wakazi wa eneo la Kijijini, lililopo katika Kata ya Kawe, Mtaa wa Mbezi Beach B, Wilaya ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam. Ukifika katika eneo hilo...
  10. JanguKamaJangu

    Bei ya kuzoa taka Mbezi Beach inapangwa kutokana na uhalisia wa mazingira na kipato

    Siku chache baada ya malalamiko kuripotiwa kuhusu gharama za uzoaji taka kwenye makazi ya watu kuwa juu katika baadhi ya mitaa ya Mbezi Beach B, ikidaiwa kuwa kuna kampuni inayotoza Tsh. 15,000 kwa mwezi kwa nyumba badala ya Tsh. 3,000 hadi 5,000 kwa mwezi, ufafanuzi umetolewa. Malalamiko yako...
  11. R

    Dar: Basi la shule la St. Florence Academy (hiace) lapata ajali maeneo ya Interchick Mbezi Beach

    Ajali hii imetokea asubuhi hii, basi hilo likionekana kutumbukia kwenye mtaro likiwa na wanafunzi kama 10 hivi. Kwa kuwaangilia watoto hawaonekani kuwa wameumia sana, zaidi ya michubuko na hofu kwa kilichotokea. Basi jingine kubwa la shue hiyolilipita eneo hilo na kuwachukua watoto hao...
  12. kamandawasua

    Natafuta Chumba master (100k) Mbezi Beach au Goba

    Habari JF, Natafuta chumba chakupangisha maeneo ya Mbezi Beach (Mbuyuni, Africana, Makonde, Shule, Kogoo, Tank Bovu, Massana) au isipite Goba Kayuni ukienda na njia ya Goba Chumba kiwe ni kikubwa na Master. Mwenye nyumba aisiwe kwenye nyumba moja. Wapangaji wasiwe wengi (8+). Kuwe na uzio/fensi...
  13. The Boss

    Mbezi Beach wamekosaje lami? Mbona Mbweni, Manzese na Yombo kuna lami?

    Kuna kitu kinanishangaza Sana...ukienda Manzese Hadi vichochoroni kuna lami...ukienda Yombo kuna lami mitaani tu huko Buza Hadi vibarazani kuna lami... Ukifika Mbezi Beach ukishatoka Bagamoyo road Tu ni vumbi juu ya vumbi...majumba makali ...eneo planned lakini barabara vumbi....wakati ukienda...
  14. Artifact Collector

    Hotel ipi dar nzuri iliyoko mbezi beach kwa kufanya tafrija ndogo

    Ni hotel ipi dar nzuri ambayo unaweza fanya tafrija ya watu kama 30 hivi ambayo ipo maeneo ya mbezi beach
  15. Chizi Maarifa

    Msaada: Anayejua gym maeneo ya Africana, Mbezi Beach

    Naombeni mnisaidie wapi nitapata GYM maeneo ya Mbezi Africana. Ndipo ninapoishi. Naona uzito unaongezeka na si nzuri sana kiafya. Pia sipendi kuwa na mwili mayai mayai. Sasa maeneo ya huku sijajua wapi naweza pata Gym nianze kufanya mazoezi. Na kama kuna Kampani pia si mbaya. Mimi naishi Mbezi...
  16. officialbryteskylinks

    Tunatoa huduma za kusajili Jina la biashara, Kampuni na Incorporated Trustees

    Tunatoa huduma zifwatazo 📍-> Web Designing. -> Logo, Banners, Posters (Graphic)Designs. -> Business name & Company Registration. (BRELA) -> Air Ticket 🎫Reservations and Bookings. -> Passport Applications. -> Visa Applications. -> Study Abroad Programs. (+ Scholarships included) -> Tin...
  17. Black Opal

    Natafuta nyumba ya kupanga vyumba viwili inayojitegemea (stand alone) maeneo ya Mbezi Beach

    Habari Wakuu, Kama kichwa kinavyosema, nahitaji nyumba ya kupanga inayojitegemea kwenye fensi yaani stand alone maeneo ya Mbezi Beach. ~ Nyumba ya vyumba viwili, sebule na jiko inayojitegemea. ~ Bajeti laki 5 (500,000). ~ Iwe maeneo tulivu Nikipata ambayo haina udalali nitashukuru. Najua...
  18. J

    Natoa siku 14 kwa viongozi wa Tanesco walioshiriki kuninyima umeme mbezi beach!

    Mimi kama "Jicho la Mganga" nafikisha ujumbe huu kutoka kwa Wilfred kwenda kwa viongozi wa Tanesco! Wilfred anasema! Takribani miezi miwili sasa Tanesco wananihangaisha! Uungwana wangu hauna maana kwao! Niliomba umeme pale tanesco tankibovu, kwa kufuata taratibu zote, wakaja kunipimia na...
  19. GENTAMYCINE

    Mbona hatujatangaziwa Tume ya Uchunguzi Kuungua kwa Al Moustafa Islamic Foundation Mbezi Beach Makonde?

    Endeleeni kudhani wenye Akili hatujui kwanini mmeuchuna wakati siyo Kawaida yenu Kuuchuna katika Matukio kama hata tena likihusisha Taasisi ya Kiimani. Halafu washaurini kama wataendelea kuwa hapo Makonde Wabadilike na kale 'Katabia Kero Kao' kwa Wanafunzi wa Kiume vinginevyo Moto wa Mwenyezi...
  20. Sildenafil Citrate

    Chuo cha Kiislamu cha Al Mustafa Mbezi Beach Chateketea kwa moto

    Chuo cha Kiislamu cha Al Mustafa kilichopo maeneo ya Mbezi Beach Makonde, Jijini Dar es Salaam kinateketea kwa moto. Chanzo cha Moto huo bado hakijajulikana. ===== UPDATE: Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Saad Mtambule amesema moto uliounguza Chuo cha AI Mustafa Mbezi Beach Dar es salaam usiku...
Back
Top Bottom