Hatimaye JK akabidhiwa ripoti ya madini

Hatimaye JK akabidhiwa ripoti ya madini

wanandugu Leo Hii Mheshimiwa
raisi Wa Jamahuri Wa Muungani Wa Tanzania Anatarajia
kupokea Ile Ripoti Ya Madini Toka Kwa Kamati Madini ...
goodnews::
meremeta Si Kampuni Ya Serikali Wanakamati Wakubaliana Hili,,,jamani Bungeni June Kama Nakuona Kazi Kwelikweli

gazeti La Mwanahalisi::

mapesa Ya Ben Yajulikana ....ac/ Zinatokea Meremeta-nbc-geneva Jamani Mungu Wee Tufungulie Njia Wanao....
 
wanandugu Leo Hii Mheshimiwa
raisi Wa Jamahuri Wa Muungani Wa Tanzania Anatarajia
kupokea Ile Ripoti Ya Madini Toka Kwa Kamati Madini ...
goodnews::
meremeta Si Kampuni Ya Serikali Wanakamati Wakubaliana Hili,,,jamani Bungeni June Kama Nakuona Kazi Kwelikweli

gazeti La Mwanahalisi::

mapesa Ya Ben Yajulikana ....ac/ Zinatokea Meremeta-nbc-geneva Jamani Mungu Wee Tufungulie Njia Wanao....
Sijui bungeni itakuwaje hapo june naona wabunge wetu wanaweza wakang'oa viti vya nyumba ya sita kama kenya hebu tusubili!
 
Namshauri Sita Awe Na Bastola Nyuma Ya Kiti Chake Vinginevyo Watu Wanaweza Kumtafuna Kileta Ujinga Wake Wa Kutetea Mafisadi.....
 
Nadhani tusubiri ripoti ianikwe hadharani ndo tutakuwa na mda wa kuichambua kwa kina kama ina maslahi kwetu.Hatujakisikia kilichomo kwenye hiyo ripoti.Madini ni urithi wetu lakini yamekuwa hayatunufaishi
 
mwanahalisi mwaga yote unayoyasikia kuwaumiza mafisadi
vyote vilivyomo ni mali zetu
 
bei ya bure tu aiitaji kuingia mtandaoni!!!!1tukuwekee oda

Sasa si ungeandika kila kitu? Bei ya bure ni ngapi na delivery method itakuwa ipi?

Kama linafaa watu tutanunua ila inabidi kujua kwanza contents zake.
 
Baada ya miezi miwili tangu kukamilika kwa ripoti hiyo. Je, itawekwa hadharani ili Watanzania tujue kilichomo katika ripoti hiyo au itafanywa kuwa ni siri kali?

JK akabidhiwa ripoti ya madini

na Mwandishi Wetu
Tanzania Daima~Sauti ya Watu

RAIS Jakaya Kikwete, leo anakabidhiwa ripoti ya Kamati ya Kuchunguza Mikataba ya Madini nchini.

Habari zilizopatikana jana zinaeleza kuwa Rais Kikwete atakabidhiwa ripoti hiyo leo saa 3 asubuhi na Mwenyekiti wa kamati hiyo, Jaji Mark Bomani.

Pamoja na Bomani, wajumbe wa kamati hiyo walioteuliwa na rais ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto (CHADEMA), Mbunge wa Msalala, Ezekiel Maige (CCM), Mbunge wa Kyela Dk. Harrison Mwakyembe (CCM), Mbunge wa Bariadi Mashariki na Mwenyekiti wa United Democratic Party (UDP), John Cheyo na mwanasiasa mkongwe, Iddi Simba.

Wapo pia Mwanasheria wa Wizara ya Nishati na Madini, Salome Makange, Kamishna wa Sera Wizara ya Fedha, Mugisha Kamugisha, Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Makazi Wizara ya Ardhi, Edward Kihundwa na Mkurugenzi wa Madai na Sheria za Kimataifa kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Maria Kejo.

Hadidu za rejea za kamati hiyo zinaonyesha kuwa itapitia mikataba ya madini na nyaraka nyingine zinazohusu migodi mikubwa na kuchambua mfumo wa kodi unaotumika katika sekta hiyo.

Aidha, kamati itapitia mfumo wa usimamizi wa shughuli za uchimbaji mkubwa unaofanywa na serikali, itachambua na kuainisha haki na wajibu wa mwekezaji na serikali na pia itakutana na ‘Chamber of Minerals’ na wadau wengine na kutoa mapendekezo kwa serikali.



Maoni ya Wasomaji
Maoni yanayotolewa na wasomaji wa safu hii ni ya kwao na sio maoni ya kampuni ya Freemedia Ltd. Aidha sio maoni ya mtunzi au mwandishi wa habari au makala husika hapo juu. Maoni haya hayajahakikiwa wala kuafikiwa na kampuni ya Freemedia Ltd.
Maoni 6 yameshatolewa. (Nawe toa maoni yako!)
kwa nini wamechelewa miezi miwili mpaka magazeti yalipowaumbua? kuna mnuko wa rushwa umepita humo!!!!

na Mzee wa MOSSAD - 24.05.08 @ 08:07 | #12997

natumai ndugu Mheshimiwa Rais upatapo ripoti hiyo ya madini, sisi watanzania tunategemea itasomwa na wote tuisikie kama ilivyokuwa ya Richmond, halafu waliohusika wawajibishwe haraka iwezekanavyo ili hizo mali walizojilimbikizia hao mafisadi zirudishwe mikononi mwa wananchi wanyonge.
Mungu ibariki Tanzania
Mungu ibariki Afrika


na nurymchunguzi, D'Salaam, - 24.05.08 @ 09:17 | #13014

Rais!
ripoti isomwe hadharani la sivyo utaisikia kambia ya upinzania itavyoitoa tena iokianisha mapungufu1 Shauri yako kama hunisikii!

na LCD, Ottawa, Canada, - 24.05.08 @ 10:21 | #13025

Pole Raisi kwa wakati huu Mgumu,lakini pokea ripoti yetu utusomee hadharani sisi wananchi,Pia elewa Baraza la MAWAZIRI wapo wabunge wachache wanaolisaliti ila,lakufanya,una changamoto mbili kuwapa wananchi Maslai yao au uwape wabunge. Ndizo kete mbili Ulizo bakiza Mheshimiwa Raisi.Gharamia KETE moja kwa garama yeyote ili Nchi ipate kupona kutoka Kwa Jinamizi ili linalotesa wananchi(UFISADI)

na Kilala M., Iringa & Arusha., - 24.05.08 @ 13:48 | #13066

Hizo hadibu za rejea zimetoka wapi? Kamati hii imetizama mikataba kama zi ile ya migodi mikubwa, kodi (royalty) na pia shughuli za usimamizi wa uchimbaji madini?

Kama vitu hivi havikupitiwa na kamati hiyo ambayo pia ilichelewesha repoti yake mpaka sasa ina maana kwamba KAMATI HIYO HAIKUFANYA KAMA VILE WALIVYOTAKIWA KUFANYA. KWA UFUPI NI KWAMBA KAMATI IMESHINDWA NA KAZI HII.

Hata hivyo tunaitaka repoti yao kamilifu iwekwe hadharani ili watanzania wote waisome.


na Dr.Khamis - 24.05.08 @ 13:50 | #13067

Watanzania inabidi tumsaidie raia wetu JK tusimkatishe tamaa.Jueni kuwa anayo kazi nzito sana.songa mbele JK kazi yako itaenziwa vizazi na vizazi.Hivi sasa unaonekana kama huna lolote,lakini kazi unayoifanya ni nzuri kupindukia.Nimeamini kweli wewe ni askari mahili.

na uswege, kyungululu, - 24.05.08 @ 14:10 | #13070
 
Fine!

Mechi mpya karibu inaaanza...all get prepared!

I dont know what is coming!

.... Kitu kikali kama cha ripoti ya Mwakyembe?

The most important thing.. tusije kubabaishana na kupotezeana muda... tunahitaji kitu chenye mantiki out of it!

Please president!

Kweli mwendendo wa nchi ..sijawahi kuuona kama huu kwa umri wote tangu nchi iasisiwe.

Mambo yako Juu!

but

Sisi ni wananchi wa nchi yetu ..tunahitaji justice na haki za ki-wananchi... Kama kuna mtu anatufanyia mzaha kwenye hili...It should be understood that..every human being has got his breaking point..n wich..can not tolarate any little longer..!

Please Rais tuepushie hilo..We have trust on you!
 
Sasa mbona Zitto na Mwafrika wa Kike walisema ilishakabidhiwa?
 
JK akiikalia hii report atajishushia hadhi.
Huko nyuma, reports zoote za madini hazijawahi kuwa hewani. Ila hii tunaitaka tuisikie. Akiikalia, itume hapa kwenye JF tuwasomee wananchi. Na kama hiyo report haija include mgodi wa Kiwira na Buzwagi basi itakuwa ni batili kabisa. Tunaunda tume nyingine.
 
Usijali mkuu.... wewe endeleza mapambano dhidi ya Zitto na Kikwete. Kwa sasa mimi nimechukua half time kwa Kikwete.

Mwafika wa Kike si ulisema kamati ilisahakabidhi ripoti na Zitto kudhibitisha hivyo?
Hii ripoti ni mpya ama vipi?


JK akabidhiwa ripoti ya madini

na Mwandishi Wetu



RAIS Jakaya Kikwete, leo anakabidhiwa ripoti ya Kamati ya Kuchunguza Mikataba ya Madini nchini.
Habari zilizopatikana jana zinaeleza kuwa Rais Kikwete atakabidhiwa ripoti hiyo leo saa 3 asubuhi na Mwenyekiti wa kamati hiyo, Jaji Mark Bomani.
Pamoja na Bomani, wajumbe wa kamati hiyo walioteuliwa na rais ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto (CHADEMA), Mbunge wa Msalala, Ezekiel Maige (CCM), Mbunge wa Kyela Dk. Harrison Mwakyembe (CCM), Mbunge wa Bariadi Mashariki na Mwenyekiti wa United Democratic Party (UDP), John Cheyo na mwanasiasa mkongwe, Iddi Simba.
Wapo pia Mwanasheria wa Wizara ya Nishati na Madini, Salome Makange, Kamishna wa Sera Wizara ya Fedha, Mugisha Kamugisha, Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Makazi Wizara ya Ardhi, Edward Kihundwa na Mkurugenzi wa Madai na Sheria za Kimataifa kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Maria Kejo. Hadidu za rejea za kamati hiyo zinaonyesha kuwa itapitia mikataba ya madini na nyaraka nyingine zinazohusu migodi mikubwa na kuchambua mfumo wa kodi unaotumika katika sekta hiyo. Aidha, kamati itapitia mfumo wa usimamizi wa shughuli za uchimbaji mkubwa unaofanywa na serikali, itachambua na kuainisha haki na wajibu wa mwekezaji na serikali na pia itakutana na ‘Chamber of Minerals’ na wadau wengine na kutoa mapendekezo kwa serikali.
 
Mwafika wa Kike si ulisema kamati ilisahakabidhi ripoti na Zitto kudhibitisha hivyo?
Hii ripoti ni mpya ama vipi?


JK akabidhiwa ripoti ya madini

na Mwandishi Wetu



RAIS Jakaya Kikwete, leo anakabidhiwa ripoti ya Kamati ya Kuchunguza Mikataba ya Madini nchini.
Habari zilizopatikana jana zinaeleza kuwa Rais Kikwete atakabidhiwa ripoti hiyo leo saa 3 asubuhi na Mwenyekiti wa kamati hiyo, Jaji Mark Bomani.
Pamoja na Bomani, wajumbe wa kamati hiyo walioteuliwa na rais ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto (CHADEMA), Mbunge wa Msalala, Ezekiel Maige (CCM), Mbunge wa Kyela Dk. Harrison Mwakyembe (CCM), Mbunge wa Bariadi Mashariki na Mwenyekiti wa United Democratic Party (UDP), John Cheyo na mwanasiasa mkongwe, Iddi Simba.
Wapo pia Mwanasheria wa Wizara ya Nishati na Madini, Salome Makange, Kamishna wa Sera Wizara ya Fedha, Mugisha Kamugisha, Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Makazi Wizara ya Ardhi, Edward Kihundwa na Mkurugenzi wa Madai na Sheria za Kimataifa kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Maria Kejo. Hadidu za rejea za kamati hiyo zinaonyesha kuwa itapitia mikataba ya madini na nyaraka nyingine zinazohusu migodi mikubwa na kuchambua mfumo wa kodi unaotumika katika sekta hiyo. Aidha, kamati itapitia mfumo wa usimamizi wa shughuli za uchimbaji mkubwa unaofanywa na serikali, itachambua na kuainisha haki na wajibu wa mwekezaji na serikali na pia itakutana na ‘Chamber of Minerals’ na wadau wengine na kutoa mapendekezo kwa serikali.


Sijawahi kusema ripoti imeshakabidhiwa. Nilisema ripoti tayari. Kumbuka leo ilikuwa ni formal makabidhiano na wala sio kwamba ndio Rais kaiona kwa mara ya kwanza.

Nilisema tumemaliza ripoti na tusubiri kupewa siku ya kuwasilisha ikulu. Tulimaliza toka tarehe 10 Aprili 2008
 
Gongeni hapo muone jinsi Mwafrika wa Kike na Zitto walipotupotosha kuwa ripoti ilishatolewa kwa rais na sasa tumpe muda wa kufanya mambo?
Nini kinaendelea watanzania wenzangu?
https://www.jamiiforums.com/showthread.php?t=7747

Mushi

Sina tabia ya kupotosha na wala sijapotosha JF lolote kuhusu ripoti maana sina motovation ya kupotosha. Nipotoshe ili iweje? Nilisema ripoti tumemaliza na tusubiri Rais atupe siku ya kuwasilisha. Siku yenyewe ikawa leo na tumewasilisha.
Hata Mwafrika wa Kike hakupotosha kitu. Nadhani hakuna tuja katika mjadala unaotaka kuuleta. Jambo la msingi hivi sasa ni content ya ripoti. Kuna nini? Mapendekekezo ni yepi? Je kuna jipya? sidhani mjadala wa mwafrika wa kike alisema hivi au vile una maana hapa hasa ukizingatia kuwa hatukusema tumeshakabidhi ripoti
 
Mushi

Sina tabia ya kupotosha na wala sijapotosha JF lolote kuhusu ripoti maana sina motovation ya kupotosha. Nipotoshe ili iweje? Nilisema ripoti tumemaliza na tusubiri Rais atupe siku ya kuwasilisha. Siku yenyewe ikawa leo na tumewasilisha.
Hata Mwafrika wa Kike hakupotosha kitu. Nadhani hakuna tuja katika mjadala unaotaka kuuleta. Jambo la msingi hivi sasa ni content ya ripoti. Kuna nini? Mapendekekezo ni yepi? Je kuna jipya? sidhani mjadala wa mwafrika wa kike alisema hivi au vile una maana hapa hasa ukizingatia kuwa hatukusema tumeshakabidhi ripoti

Zitto,
Kama huatajari unaweza kudokeza kidogo yaliomo au mpaka rais atoe tamko rasmi kwanza ?
 
Back
Top Bottom