jmushi1
Platinum Member
- Nov 2, 2007
- 26,375
- 25,453
- Thread starter
- #281
Naona hii ndio sasa kauli mbiu.....?!
Sitta afungua matawi ya CCM India
na Mwandishi Maalumu
SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samuel Sitta, amefungua matawi mawili makubwa ya CCM katika miji ya Bangalore na Mysore nchini India na kufanikiwa kupata zaidi ya wanachama 200.
Katika uzinduzi huo, Sitta ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, alifanikiwa kupata wanachama 140 katika tawi la Bangalore na zaidi ya wanachama 120 katika tawi la Mysore ambao wote ni wanafunzi katika vyuo mbalimbali vya elimu ya juu katika miji hiyo.
Akihutubia vijana hao, kwa nyakati tofauti, Sitta alisisitiza hatokata tamaa katika vita dhidi ya rushwa na ufisadi kwa kutumia Bunge kama taasisi anayoiongoza na kuwathibitishia wana CCM hao kwamba Bunge ni imara na thabiti katika vita hiyo na kwamba watafanikiwa.
"Bunge tuko imara tuungeni mkono katika hili, nawahakikishia pamoja na umbea na fitina ya wasiopenda uimara wa Bunge letu, sikatishwi tamaa na siasa zao za majitaka," alisema Spika.
Akionyesha uthabiti wa hoja zake, Spika alinukuu vifungu vya katiba vinavyomuongoza katika kulifanya Bunge lisimamie serikali na uwajibikaji wake.
"Ninalindwa na kuongozwa na katiba. Katiba yetu ibara ya 72 na 64 zipo wazi na zinaeleza majukumu ya Bunge, hivyo kelele za mlango hazimnyimi usingizi mwenye nyumba," alisema.
Aliwaagiza wanachama hao wapya wa CCM kutumia uzoefu na elimu yao kukijenga chama chao na wasisite kuleta mawazo mapya kwa chama, ili kiendane na wakati na mazingira ya siasa iliyopo.
Alikubali ombi la kuwa mlezi na mshauri wa tawi la CCM Bangalore na alichangia dola 500 katika mfuko wa tawi hilo na dola 500 nyingine katika mfuko wa tawi la CCM Mysore. Katika nasaha zake, Nape Nnauye, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (T) anayewakilisha vijana, ambaye ndiye mhamasishaji wa ufunguzi wa matawi hayo, alimthibitishia Spika kuwa vijana wa CCM wanamuunga mkono na kwamba wanatambua kazi yake nzuri anayofanya katika vita dhidi ya ufisadi. Katika risala yao tawi la CCM Mysore iliyosomwa na Mohamed Ally Shein, mtoto wa Makamu wa Rais wa Tanzania, walisisitiza hoja ya wanachama wa CCM mafisadi kuachia hata nafasi walizonazo kwenye chama.
Sitta afungua matawi ya CCM India
na Mwandishi Maalumu
SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samuel Sitta, amefungua matawi mawili makubwa ya CCM katika miji ya Bangalore na Mysore nchini India na kufanikiwa kupata zaidi ya wanachama 200.
Katika uzinduzi huo, Sitta ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, alifanikiwa kupata wanachama 140 katika tawi la Bangalore na zaidi ya wanachama 120 katika tawi la Mysore ambao wote ni wanafunzi katika vyuo mbalimbali vya elimu ya juu katika miji hiyo.
Akihutubia vijana hao, kwa nyakati tofauti, Sitta alisisitiza hatokata tamaa katika vita dhidi ya rushwa na ufisadi kwa kutumia Bunge kama taasisi anayoiongoza na kuwathibitishia wana CCM hao kwamba Bunge ni imara na thabiti katika vita hiyo na kwamba watafanikiwa.
"Bunge tuko imara tuungeni mkono katika hili, nawahakikishia pamoja na umbea na fitina ya wasiopenda uimara wa Bunge letu, sikatishwi tamaa na siasa zao za majitaka," alisema Spika.
Akionyesha uthabiti wa hoja zake, Spika alinukuu vifungu vya katiba vinavyomuongoza katika kulifanya Bunge lisimamie serikali na uwajibikaji wake.
"Ninalindwa na kuongozwa na katiba. Katiba yetu ibara ya 72 na 64 zipo wazi na zinaeleza majukumu ya Bunge, hivyo kelele za mlango hazimnyimi usingizi mwenye nyumba," alisema.
Aliwaagiza wanachama hao wapya wa CCM kutumia uzoefu na elimu yao kukijenga chama chao na wasisite kuleta mawazo mapya kwa chama, ili kiendane na wakati na mazingira ya siasa iliyopo.
Alikubali ombi la kuwa mlezi na mshauri wa tawi la CCM Bangalore na alichangia dola 500 katika mfuko wa tawi hilo na dola 500 nyingine katika mfuko wa tawi la CCM Mysore. Katika nasaha zake, Nape Nnauye, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (T) anayewakilisha vijana, ambaye ndiye mhamasishaji wa ufunguzi wa matawi hayo, alimthibitishia Spika kuwa vijana wa CCM wanamuunga mkono na kwamba wanatambua kazi yake nzuri anayofanya katika vita dhidi ya ufisadi. Katika risala yao tawi la CCM Mysore iliyosomwa na Mohamed Ally Shein, mtoto wa Makamu wa Rais wa Tanzania, walisisitiza hoja ya wanachama wa CCM mafisadi kuachia hata nafasi walizonazo kwenye chama.