Si amteke SSH?! Mbona alikuwa kiongozi wa genge la kuteka upinzani enzi zake? Sasa hivi anashindwa nini kwa wanaccm wenzake wasiomsikIliza hadi abaki akilialia mtaani?Inashangaza sana kuona wafuasi na wanachama wa upinzani wanafurahia uonevu anaofanyiwa Hamphrey Polepole. Hii yote ni sababu tu alipokuwa mwenezi wa CCM taifa alijenga imani ya CCM kwa wananchi na kusababisha wapinzani wengi kuunga juhudi.
Anakosea nini kukosoa na kusema kweli kuwa Ccm inafanya makosa? Anakosea nini kukosoa juu ya mradi wa JNHP kucheleweshwa bila sababu? Kama kuna harufu za kifisadi juu ya pesa umma, au miradi kama bandari ya Bagamoyo, kuna kosa?
Je, mnadhania watanzania wanaupofu? Hawaoni kuwa Polepole anasimamia wapi?
Watanzania wazalendo wapo pamoja na Polepole.