Kwa hiyo unawahitaji Wapinzani wamsaidie Polepole kwenye harakati zake? Vi8 zake hazina msaada kwake tena?Inashangaza sana kuona wafuasi na wanachama wa upinzani wanafurahia uonevu anaofanyiwa Hamphrey Polepole. Hii yote ni sababu tu alipokuwa mwenezi wa CCM taifa alijenga imani ya CCM kwa wananchi na kusababisha wapinzani wengi kuunga juhudi.
Anakosea nini kukosoa na kusema kweli kuwa Ccm inafanya makosa? Anakosea nini kukosoa juu ya mradi wa JNHP kucheleweshwa bila sababu? Kama kuna harufu za kifisadi juu ya pesa umma, au miradi kama bandari ya Bagamoyo, kuna kosa?
Je, mnadhania watanzania wanaupofu? Hawaoni kuwa Polepole anasimamia wapi?
Watanzania wazalendo wapo pamoja na Polepole.