jmushi1
Platinum Member
- Nov 2, 2007
- 26,381
- 25,476
JK alikataa mkataba usivunjwe,na yeye si RICHMOND,EL alitaka uvunjwe na yeye ni RICHMOND...Ndivyo mnavyotaka nielewe.Kulikuwa na kamati tatu mkuu,
Kamati ya makatibu Wakuu (Nishati, Fedha)
Kamati ya wanasheria
Kamati ya wataalam.
JK aliongea na kamati ya maPS, akaambiwa aache Richmond, Dowans ikauchukua mkataba, na Tanesco wakalipwa hela zao due to incapacity.Hapo mimi sioni kosa.
Kamati ya wataalam, ndiyo iliyokuwa inashughulika nani apewe contract na Ofisi ya waziri mkuu ilikuwa inafuatilia kwa ukaribu mchakato mzima.
Msabaha na balozi Kazaura waliiambia kamati ya bunge kuhusu Richmond kuwa ni kampuni ya Lowassa na Rostam.... mbona hamzungumzii hili?
Mbona hamzungumzii mkataba uliosainiwa kati ya Yona na Gire kuhusu bomba la mafuta?
Tusidanganyane, Mkapa,Yona , lowassa na sumaye ni maswahiba waliojitahidi kutengeneza fedha nyingi through energy na ni lazima wawajibishwe, ikiwezekana wanyongwe.
Hii ndo shida ya kudekeza wanasiasa mantuona sisi ni kama mapunguwani.
Hii issue si ya kisiasa...Kwasababu mahakama huru haitaangalia nani alikuwa chama gani.
Kama katiba na sheria za nchi vimevunjwa na wale walioapa kuilinda,then wapi uhalali wa kuongoza?