Happy born day Mwamba Mbowe

Kwanza mtu mwenyewe kwenye uongozi ameonekana kupwaya, akiwa amejikita kwenye kula pesa ya CHADEMA.
Hizi ndio propaganda za ccm katika ubora wake. Tokea baada ya uchaguzi wa 2020, CHADEMA haikupeleka akaunti ambayo ingetumiwa kuwawekea fedha ya ruzuku, ambayo ni haki yao kikatiba na kwa mujibu wa sheria na kanuni. Kwa kupata zsidi ya 13% ya kura za urais tu, CHADEMA tayari wana kiasi kikubwa tu cha fedha stahili yao kama ruzuku. Lakini kwa kujali msimamo, wamekataa kuchukua hiyo ruzuku. Sasa huko CHADEMA kuna fedha ipi ambayo Mbowe anaitafuna? Maana alifungiwa akaunti zake binafsi, hakuna akaunti ya chama iliyoguswa. Ulichoandika ni umbeya wa bei ya chini kabisa.
Kama kweli Mbowe angekuwa "amepwaya katika uongozi" basi wala asingeandamwa na serikali ya ccm. Anaandamwa kwa sababu yuko very effective katika kutekeleza malengo ya CHADEMA
 
Amkeni, tujuwe CHADEMA HAINA KIONGOZI MMOJA TU. WAPO WENGI, NA KUSHIRIKIANA KWAO NDIYO KUTALETA MABADILIKO, SIYO IMANI KWA MTU MMOJA UTAFIKIRI mUNGU.
CHADEMA ni taasisi kubwa. Ina viongozi wengi, kuanzia ngazi ya tawi, wilaya, mkoa, kanda na taifa. Viongozi wengine wapo ndani ya nchi na wengine nje ya nchi. Wengine wapo gerezani wengine hawapo gerezani. Kwa pamoja wanaongoza taasisi hii inayoisumbua serikali ya ccm. Mungu ibariki CHADEMA. Amina.
 
Tangu kuanza kwa upinzani rasmi 1995, ccm huwa wako makini kumtarget mtu au watu au taasisi ambayo ina uungwaji mkono mkubwa na watanzania, dhidi ya serikali zake za kibaradhuli. Mwaka 1995, baada ya Agustino Mrema kujiengua ccm na kujiunga NCCR, nchi ilizizima, na Mrema mara moja akawa mlengwa. Kila mara alipigwa mabomu ya machozi, na NCCR ikalengwa kwa njama za kila aina. Baada ya NCCR kuporomoka, CUF ndio ikawa namba moja katika upinzani. Mara ooohhh, chama cha waarabu. Mara ooohh, watamleta sultani, na propaganda kemkem. Lipumba alishambuliwa na polisi mara kwa mara wakati huo.
Kipindi chote hicho, CHADEMA walikuwa wapo, lakini ccm wala hawakuwa na habari CHADEMA ni kitu gani. Taratibu CHADEMA ilipata wabunge wengi zaidi kila uchaguzi. Kufika 2010, CHADEMA ilipomsimamisha dokta Slaa kugombea urais, hapoooo, mizinga ya ccm ikaelekezwa kwao. Mara ooohhh, chama cha wakristu. Sasa CHADEMA ndio chama kinachoisumbua ccm. Uchaguzi wa 2015 ccm ilipigwa chini, lakini kwa kufuata mila chafu na najisi, iliyoasisiwa na Nyerere tangu uchaguzi wa 1995, pale alipomlazimisha komandoo Salmin Amour ambaye alishatundika buti baada ya kushindwa na CUF ya maalim seif, abaki madarakani. Tokea hapo ccm wanajua hakuna mungine, ni wao tu hata kama wananchi watawakataa kwenye kura.
Kwa kutazama tu kampeni za CHADEMA 2020, ni wazi CHADEMA ndio chaguo la watanzania walio wengi. Pamoja na hujuma za serikali ya ccm, jinsi muda ulivyokuwa unakwenda, ndivyo wengi zaidi walielewa ujumbe wa mgombea wa CHADEMA , na ndivyo serikali ya ccm ilivyozidi kuchanganyikiwa, na hatimaye kufanya uporaji wa kihistoria.

Mbowe, kama ilivyokuwa Mandela, anabeba matumaini ya wengi. Haina maana wengine hawapo. Wapo kina Lissu, kina Lema, kina Msigwa, kina Heche, na wengine wengi. Ila kiukweli, jinsi ccm wanavyotumia nguvu dhidi ya Mbowe, ndio wanazidi kumpaisha.
Kumbuka pia Mbowe ni mtu wa pekee. Ameitoa CHADEMA chini na kuileta juu. Na kwa kuwa serikali ya ccm wanajua fika kwamba Mbowe ndio kaibeba CHADEMA hata kifedha, waliamua kumsambaratisha kiuchumi. Akaunti zake zote zilifungwa na Magufuli. Miradi yake ikahujumiwa. Bado jamaa wanachanja mbuga. Mwishowe wamekuja na mkakativwa kumfungulia kesi ya ugaidi. Wataweza kumdhibiti mpambanaji huyu ? Asilani hawawezi! Toka lini majambazi, wezi, waporaji wakashinda?
Punguza mihemko
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom