Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,183
- 10,921
Mapigano makali yasiyotarajiwa yametokea juzi siku ya Jumamosi maeneo yote ya Gaza,kaskazini mpaka kusini.
Katika purukushani hiyo kikosi cha Qassam kimesema kimewaua askari wengi wa Israel.
Hata hivyo Israel imekiri kupoteza askari wawili tu na kudai imewaua wapiganaji kadhaa wa Hamas na wengine kuwakamata.
Hali hiyo imeshangaza kwani imetokea maeneo mpaka ya jiji la Gaza ambako awali IDF walitangaza kuusafisha mji huo kutokana na wapiganaji wa Hamas.
Ving'ora vilisikika kwenye miji ya kusini ya Israel kuashirria kurushwa kwa makombora ya Hamas kutoka Gaza.
Matukio hayo ya kukatisha tamaa kwa IDF yametokea wakati vita vikiingia mwezi wa 5 bila kufikiwa malengo ya vita yaliyotangazwa na huku juhudi kubwa zikifanyika vita visitishwe moja kwa moja.
Katika purukushani hiyo kikosi cha Qassam kimesema kimewaua askari wengi wa Israel.
Hata hivyo Israel imekiri kupoteza askari wawili tu na kudai imewaua wapiganaji kadhaa wa Hamas na wengine kuwakamata.
Hali hiyo imeshangaza kwani imetokea maeneo mpaka ya jiji la Gaza ambako awali IDF walitangaza kuusafisha mji huo kutokana na wapiganaji wa Hamas.
Ving'ora vilisikika kwenye miji ya kusini ya Israel kuashirria kurushwa kwa makombora ya Hamas kutoka Gaza.
Matukio hayo ya kukatisha tamaa kwa IDF yametokea wakati vita vikiingia mwezi wa 5 bila kufikiwa malengo ya vita yaliyotangazwa na huku juhudi kubwa zikifanyika vita visitishwe moja kwa moja.