Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,200
- 10,947
Katika hali ya kuchanganyikiwa na vita vya Gaza Israel imeelezwa kukubali kimsingi vita visitishwe ili irejeshewe mateka wake.
Hali ya kuchanganyikiwa kwa Israel kumeonekana hapo juzi ambapo iliwamiminia mabomu mazito kutoka angani na kuwapiga kwa risasi watu zaidi ya mia waliokuwa wakisubiri misaada huko kaskazini ya Gaza.
Kingine kinachowachanganya ni kuona maeneo yote waliyopita na kudhani wamewamaliza Hamas wamegundua bado yana wapiganaji hao wenye silaha na wanaoendelea kuleta maafa kwa askari wake.
Leo Jumamosi IDF imetangaza kupoteza askari wake watatu eneo la Khan Younis ambalo jeshi hilo lilikwishatoa tangazo la kudhibiti eneo hilo.
Maafisa wa ngazi za juu wa ikulu ya Marekani wamesema kimsingi Israel imeshakubali kusitishwa kwa vita kati yake na Hamas kwa muda wa wiki sita.Kipindi hicho kitaambatana na kuachiwa huru kwa mateka wa Israel wanaoendelea kushikiliwa na Hamas
Baada ya kueleza hayo afisa mmoja kati yao akaongeza kuwa mpira sasa uko kwa Hamas.
Hali ya kuchanganyikiwa kwa Israel kumeonekana hapo juzi ambapo iliwamiminia mabomu mazito kutoka angani na kuwapiga kwa risasi watu zaidi ya mia waliokuwa wakisubiri misaada huko kaskazini ya Gaza.
Kingine kinachowachanganya ni kuona maeneo yote waliyopita na kudhani wamewamaliza Hamas wamegundua bado yana wapiganaji hao wenye silaha na wanaoendelea kuleta maafa kwa askari wake.
Leo Jumamosi IDF imetangaza kupoteza askari wake watatu eneo la Khan Younis ambalo jeshi hilo lilikwishatoa tangazo la kudhibiti eneo hilo.
Maafisa wa ngazi za juu wa ikulu ya Marekani wamesema kimsingi Israel imeshakubali kusitishwa kwa vita kati yake na Hamas kwa muda wa wiki sita.Kipindi hicho kitaambatana na kuachiwa huru kwa mateka wa Israel wanaoendelea kushikiliwa na Hamas
Baada ya kueleza hayo afisa mmoja kati yao akaongeza kuwa mpira sasa uko kwa Hamas.