Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,195
- 10,929
Katika hali isiyotegemewa kabisa.Viongozi wa kundi la Hamas wamekanusha madai ya jeshi la Israel kwamba wamepoteza udhibiti wa Gaza na kwamba jeshi la Israel limesonga mbele mpaka katikati ya Gaza.
Mshangao unakuja kutokana na ukubwa wa mashambulizi yaliyofanywa na jeshi la Israel na kutoa moto mkubwa unaokaribia mawinguni kila baada ya robo saa kwa usiku na mchana.
Mapigo hayo yamefanyika huku jiji hilo likiwa limekatiwa umeme,chakula na maji.Katika hali hiyo kila mmoja alihofia kuwa wapiganaji wa Hamas wameshadhoofika na kufa ndani ya mahandaki yako.
Kinyume chake wameibuka juu na kukanusha madai ya Israel kwamba kwamba kundi hilo limepoteza udhibiti wa Gaza.Pamoja na kukanusha huko wamesambaza video ambayo imethibitishwa na televisheni kadhaa ikiwemo aljazeera ikiwaonesha wapiganaji hao wakiripua vifaru ya Israel kwa kutumia bunduki za RPG.
Video na ukanushaji huo wa Hamas unakubaliana na madai yao kuwa wameshauwa askari wengi wa Israel na kuhjaribu magari yao 136 na kwamba jeshi hilo kwa sasa limeshindwa kusonga mbele.
Uwezekano wa kutosonga mbele utaongezeka pindi Hamas wakiweza kuhimili kipigo kwa wiki chache zijazo,