Johnny Sack
JF-Expert Member
- Jan 21, 2017
- 8,834
- 18,837
Kundi la Hamas limejibu kuhusu shutma mbalimbali zinazotolewa kwa kundi hilo kuwa limeua raia wa kigeni ambao hawahusiki na mgogoro wake na Israel
Hamas wamejibu tuhuma hizo kwa kusema kuwa raia wa kigeni kuuawa kunatuma ujumbe kwa mataifa mengine kuwa taifa haramu la Israel sio salama na raia wa nchi nyingine wasiwe wanaendelea kukaa huko,
Msemaji wao ameongeza kuwa raia wa kigeni kwenda Israel kwa ajili ya shughuli yoyote ni kama anaunga mkono taifa hilo haramu na hivyo naye ni muhusika kwenye vita yao isiyoisha dhidi ya Israel