Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,183
- 10,920
Maamuzi ya kudai uhuru kivitendo iliyofanya Hamas yanaanza kuzaa matunda japo yamepatikana kwa gharama kubwa sana ya vita kuliko vita vyote.
Waziri muhimu katika baraza la kuongoza vita nchini Israel,Gadi Eisenkot amesema malengo halisi ya vita kati ya Israel na Hamas hayako wazi na anayeyajuwa zaidi ni Benjamin Netanyahu.
Pamoja na kauli waziri Gadi ambaye mtoto wake aliuliwa na Hamas mwezi uliopita huko Gaza ameongeza kwa kusema kuishind Hamas ni kitu ambacho sio kweli.Akaongeza kwa kutaka uitishwe uchaguzi haraka ndani ya mwezi mmoja kama kwamba anapendelea Benjamin Netanyahu aondoshwe kwenye madaraka kwa kuletea janga nchi yao.
Maelezo hayo ya wazi ya waziri huyo ameyatoa mara baada ya Benjamin Netanyahu kujibu hoja za viongozi wa Marekani juu ya haja ya kuundwa kwa taifa la Palestina sambabmba na kuwepo kwa taifa la Israel na kama ilivyopendekezwa kwenye maazimio kadhaa huko nyumoa
Katika majibu yake Benjamin Netanyahu alisema hakuna wa kumzuia kuwamaliza Hamas na hatoruhusu kuundwa kwa taifa la Palestina.
Majibu hayo ya waziri Gadi yanakuja wakati jeshi la Israel likizidi kupata fedheha huko Gaza na kuongezeka kwa mapigano kaskazini ya nchi hiyo kati yake na Hizbullah na kwa upande mwengine kubadilika kwa makundi ya upinzani ukingo wa mashariki ambapo sasa makundi hayo yamekuwa yakiongezeka nguvu na kupigana vita vikali na jeshi la IDF
Waziri muhimu katika baraza la kuongoza vita nchini Israel,Gadi Eisenkot amesema malengo halisi ya vita kati ya Israel na Hamas hayako wazi na anayeyajuwa zaidi ni Benjamin Netanyahu.
Pamoja na kauli waziri Gadi ambaye mtoto wake aliuliwa na Hamas mwezi uliopita huko Gaza ameongeza kwa kusema kuishind Hamas ni kitu ambacho sio kweli.Akaongeza kwa kutaka uitishwe uchaguzi haraka ndani ya mwezi mmoja kama kwamba anapendelea Benjamin Netanyahu aondoshwe kwenye madaraka kwa kuletea janga nchi yao.
Maelezo hayo ya wazi ya waziri huyo ameyatoa mara baada ya Benjamin Netanyahu kujibu hoja za viongozi wa Marekani juu ya haja ya kuundwa kwa taifa la Palestina sambabmba na kuwepo kwa taifa la Israel na kama ilivyopendekezwa kwenye maazimio kadhaa huko nyumoa
Katika majibu yake Benjamin Netanyahu alisema hakuna wa kumzuia kuwamaliza Hamas na hatoruhusu kuundwa kwa taifa la Palestina.
Majibu hayo ya waziri Gadi yanakuja wakati jeshi la Israel likizidi kupata fedheha huko Gaza na kuongezeka kwa mapigano kaskazini ya nchi hiyo kati yake na Hizbullah na kwa upande mwengine kubadilika kwa makundi ya upinzani ukingo wa mashariki ambapo sasa makundi hayo yamekuwa yakiongezeka nguvu na kupigana vita vikali na jeshi la IDF