Dr Msweden
JF-Expert Member
- Nov 3, 2020
- 2,632
- 9,445
Jioni hii nimepitia kuchukua hesabu katika moja ya pharmacy yangu iliyopo Mbande Chamazi nikakutana na hii barua kutoka serikali ya mtaa ,bahati nzuri aliyeleta hii barua alikuwa mtendaji nimeisoma yote nikaanza kumuuliza maswali kuhusu hizi tozo mpya za taka.
Maswali niliyomuuliza alishindwa kujibu akasema kuwa halmashauri ya Temeke ndio wametoa hilo tamko kwa kila kata.
Kwenu halmashauri ya Temeke
Ni sawa mama lishe kulipa 2000 kila siku?
Ni sawa gereji ya bodaboda kulipa 120,000 kwa mwezi?
Ni sawa fundi seremala kulipa 100,000 kwa mwezi?