Kwanini naunga mkono tozo

Kamundu

Platinum Member
Nov 22, 2006
6,598
8,738
Kwanza tuweke mambo sawa tozo ni aina ya kodi. Hivyo tusiongelee tozo kama vile sio kodi.

Mimi binafsi sijaona ubaya wowote wa serikali kuweka tozo na nina fikiri hakuna njia nyingine kwa wakati huu zaidi ya tozo na nitajaribu kuweka hoja hapa vizuri. Tanzania kama nchi inayoendelea inahitaji pesa ili iweze kuwekeza kwenye miradi mingi sana kuanzia elimu, maji, barabara, umeme, kilimo, ulinzi, n.k

Sasa vyanzo vya mapato ni hivi;
  1. Missada kutoka nje
  2. kodi na tozo
  3. mikopo
Tanzania tumeshakopa na bado tutaendelea kukopa kama tutapata mikopo nafuu lakini vilevile tunakusanya kodi mbalimbali. Lakini ukiangalia vizuri budget zetu pesa ya kodi ambayo haitoshi hata kwenye budget bado inaenda kwenye shughuli ambazo sizo za kimaendeleo hivyo sio uwekezaji wa nchi bali ni matumizi.

Kuna miradi tunalipia kwenye kodi kama ya maji na umeme lakini wakati wa Kikwete pesa karibu yote ilikuwa ni kulipa mishahara na matumizi ya serikali.

Sasa kama nchi tuko kwenye kipindi cha uwekezaji kwa mara ya kwanza tunaanza kuona barabara za kisasa, shule bora, hospitali na umeme hasa vijijini. Sasa tumefikaje hapa ? Ni kuwekeza kwa kodi mpya na tozo.

Umeme mfano wa vijijini umepelekwa na tozo maalamu kwenye luku za nyumbani na barabara za vijijini nyingi zinatengenezwa na tozo kwenye mafuta. Lakini ili kama nchi tuweze kuwekeza na kuongeza walipa kodi ni lazima tuwekeze kwenye kilimo.

Kilimo kitaongeza mapato kwenye kodi lakini tatizo hatuna mfumo mzuri wa kilimo kuwa na uazalishaji wa uhakika. Bashe amekuja na mpango mzuri wa kuongeza uzalishaji kwa kufanya yafuatayo (1) Serikali itatoa ruzuku kwenye mbolea (2) Serikali itawekeza kwenye umwagiliaji (3) watatoa mbegu (4) watafuta wawekezaji wa viwanda (5) kutafuta masoko.

Hii ndiyo mojawapo kubwa ya kuongeza ajira na kodi lakini mtaji wa yote haya ni karibu Trillion moja sasa mtaji unatoka wapi? Hii ndiyo sababu imeenda kwenye tozo hivyo tozo ni muhimu kwasababu ni mtaji wa uhakika wa kuongeza kodi kwa miaka ijayo. Lakini ni tukiangalia vizuri tatizo letu ni utamaduni mbovu watu wengi walizoea kukaa bila kulipa kodi wala tozo.

Mimi ni diaspora wa muda mrefu sana na naishi na kutafuta maslahi yangu jimbo la Texas. Hili jimbo letu linajulikana kwa kuwa na kodi ndogo lakini ngoja niwape data kidogo ili mgundue tonavyolipa kodi.
  • Nyumba kila mwaka nalipa 3% ya thamani ya nyumba. Hivyo kwa mfano kama nyumba pale Tanzania yenye thamani ya Tsh 100,000,000 basi unatakiwa kulipa kila mwaka Tsh 3,000,000. Hakuna mjadala kwenye hili na usikolipa unapekwa mahakamani na nyumba inapigwa mnada.
  • Jumuia na majiradi vilevile wana kitu kinaitwa HOA-Housing Owners Association hii ni jumuia ya makazi yako na majirani kila nyumba inalipa $350-$1000 kwa mwaka kwa usafi wa jumla kama kukata majani na kusafisha mitaro. Hii ni nje ya nyumba yako hii nayo ni lazima na kisheria wanaweza kwenda na utaratibu mpaka wakapiga mnada nyumba.
  • Tuna tozo za maji na kuchukuwa taka. Kila wiki wanapita kuchukuwa taka kwenye magaloni maalumu. Hii inafanywa na manispaa huwezi kuchoma matakataka ovyo ovyo. Maji unalipa kutokana ma matumizi lakini taka utalipia unataka au hautaki jumla sio chini ya $100 kila mwezi. Ukitupa uchafu ovyo ni faini, usipoweka uchafu vizuri kwenye mifuko ni faini.
  • Barabara nyingi zinajegwa kwa mikopo inayoitwa goverment bonds hivyo ni lazima ilipwe. Kila nikienda kazini kwa mfano ni lazima nipitie kwenye barabara za kulipia "toll roads" na natumia sio chini ya $5-$7 kwenda kwa siku moja na kurudi. Tena hii ni rahisi New York wanatumia $12-$15.
  • Ukienda kwenye hotel na kokodi chumba karibu 35% ni kodi na tozo, kwenye simu, cable za TV au Dish hivyohivyo.
  • Kwenye super market kila ukinunua kitu kuna 5% ya tozo inaenda kusaidia “Metro" ambayo ni kama mwendo kasi yetu.
  • Lakini hapa kuna bima ya karibu kila kitu nyumba ni lazima uwe na bima na kwenye hizi bima kuna pesa zinaenda kusaidia idara kama zimamotto na ambulance.
Hapa sijaongelea tozo na kodi za mishahara. Lakini mjue hapa bado tuna nafuu sana kulinganisha na nchi za Ulaya au Canada ambako Tozo na kodi zipo juu sana. Familia yangu ina bahati tuna nyumba Uninio sehemu ambayo ina thamani sana lakini kodi zetu pale hazifiki hata 1% ya thamani wakati bodaboda wanalipa kodi kwenye mafuta. Hivyo kuna sehemu kiukweli wanaonufaika ni matajiri tu kusema ukweli.

Kuna ambao watasema huko Ulaya na US pesa inaonekana ni kweli tuna shule kwenye kila mtaa za watoto zina mabasi na ni bure lakini tunalipa 3% kwenye thamani ya nyumba na pesa inaenda huko. Hivyo hoja ni yaanze mayai au kuku lakini kodi ni muhimu na maendeleo ni muhimu.

Ndiyo maana hoja yangu ni kwamba tozo ni muhimu kwasababu ni mtaji na utaratibu mpya wa kuongeza wigo la walipa kodi na kuweka mifumo ya kimaendeleo.

Tatizo kubwa ni mazoea ya watu wengi walikuwa wamezoea kukaa bila shughuli na kubangaiza lakini kama tunataka umeme vijijini, barabara za lami na hospitali ni lazima zitengenezwe, kuwe na pesa za matengenezo kila mara na pesa za wahudumu.

Ni lazima kuwe na mfumo wa mapato na wananchi ni lazima wazalishe ili waweze kuwa na mifumo hii. Huwezi kukaa kijijini hulipi kodi yeyote, huzalishi chochote halafu unahitaji barabara, maji, umeme ... pesa inatoka wapi? Ni lazima serikali iwekeze kwenye kilimo ili wewe mwanakijiji uweze kuchangia kodi na maendeleo na ndicho kinacho fanyika kwa sasa.
 
Kwanini hizo tozo mnazokata kila dakika kwenye miamala ya simu hatuambiwi mapato na matumizi yake kila mwezi kama ilivyokuwa mwanzo?

Kwanini kwa huo ukimya wa waziri wa fedha tusiamini sehemu ya hizo pesa za tozo zinachezewa hasa tukiskia tuhuma za kumiliki timu ya mpira wa miguu, na mabasi 60 kuingizwa nchini?

Kuna mtu anawatumia, sasa kamwambie akupe majibu ya hayo maswali ndio urudi hapa.
 
Mkuu, kueleza umeeleza vizuri tu. Shida ni kwamba...kiwango cha tozo kinalemea...na pia matumizi yake hayaeleweki.

Sio kama huko diaspora maendeleo unayaona...huku hayo matumizi hayaeleweki, hayawekwi wazi... unasikia tu, 'oooh tumetumia kiasi flani kufanya sjui nini, huku, kule, pale na hapa' lakini hatuoni stakabadhi pesa imeenda wapi na ni shingapi. Wala miradi ikitaka kuanzishwa hatushirikishwi.

Kwa mfano tozo, mtu ulikuwa unashtukia tu pap, sku izi umeanza kukatwa ela benki. Badala ya kutaarifu kwanza, na kuwaweka watu tayari.
 
Tanzania tuna madini, gesi, mafuta, misitu, mbuga za wanyama, na ipo top 4 katika nchi zinazovutia duniani , ungeishauri serikali iongeze nguvu katika vyanzo vilivyopo kuliko kuongeza Kodi mara 2.
Fikiria unapokea mshahara x , hafu hiyo x inakatwa mara 10 zaidi


Hapa US kuna watu wanaosema ni kwanini serikali inatoa misaada nchi nyingine wakati kuna ombaomba wengi na watu wasio na nyumba? Hii ni mifumo na hatuwezi kukubaliana na kila kitu wangekubaliana na hawa tusingepata $600M kama msaada kutoka US wa Afya miaka miwili iliyopita
 
Mkuu.... kueleza umeeleza vizuri tu. Shida ni kwamba...kiwango cha tozo kinalemea...na pia matumizi yake hayaeleweki...
Sio kama huko diaspora maendeleo unayaona...huku hayo matumizi hayaeleweki, hayawekwi wazi... unasikia tu, 'oooh tumetumia kiasi flani kufanya sjui nini, huku, kule, pale na hapa' lakini hatuoni stakabadhi pesa imeenda wapi na ni shingapi. Wala miradi ikitaka kuanzishwa hatushirikishwi...kwa mfano tozo, mtu ulikuwa unashtukia tu pap, sku izi umeanza kukatwa ela benki. Badala ya kutaarifu kwanza, na kuwaweka watu tayari.

Nakubaliana na wewe lakini tujue tu hizi ni tozo mpya na serikali inahitaji muda kuonyesha kimefanyika nini. Hatutaweza kujua kwasasa manufaa ya uwekezaji kwenye kilimo cha umwagiliaji wakati hata tozo na uwekezaji haujafanyika. Lakini kwenye hizi tozo tujiulize mfano hayo makato ya kibank na yale ya simu ambayo yapo je viwango vilikuwa halisi au walikuwa nao wanaweka juu sana?. Bank mfano ATM fees tunajua pesa yote hiyo ni ya nini wakati mifumo ya pesa ni rahisi na bank kuu inafanya kila kitu
 
Afrika tutawaliwe tena
Tusipende majibu marahisi tufikirie na kujadili hoja. Tatizo la vijana wengi hamtaki hata kufikiria mnahitaji mambo rahisi rahisi tu. Kwani hao wazungu sio binadamu mbona kwao kuna tozo, kodi tena zaidi ya TZ!
 
Tusipende majibu marahisi tufikirie na kujadili hoja. Tatizo la vijana wengi hamtaki hata kufikiria mnahitaji mambo rahisi rahisi tu. Kwani hao wazungu sio binadamu mbona kwao kuna tozo, kodi tena zaidi ya TZ!
Huwezi kumkata kodi Mtu mara 2 kwa pato lilelile kwa kubadilisha tu majina halafu wewe usiyeathirika uje usapoti unyama usiokugusa.
 
Ngoja nianze na mifano yako nikilinganisha hapa Nyumbani Tanzania.

Tuna Kodi ya Ardhi ambayo tunalipia kwa mwaka.
Kodi ya jengo ambayo imeingizwa kwenye mfumo wa Umeme.

Hizi Kodi mbili zinakata chanzo kimoja na mtu yule yule na eneo Lile Lile mathalani ni nyumba kwa ajili ya makazi.

Value added Tax hakuna huduma utakayo pata Tanzania ikiwemo kununua bidhaa usikatwe asilimia 18% au 15% ya huduma, hapa inategemea hiyo Vat ni inclusive au exclusive

Ukiwa unafanya biashara na taasisi za serikari, Kuna 2% withholding Tax( Kodi ya zuio) na Ile VAT ipo pale pale.

Kuna Kodi nadhani ilikuwa ya wanaotumia vyombo vya moto kuhusu Matumizi ya Barabara ikaondolewa na kujumuishwa kwenye kila Lita ya mafuta, Sasa hii inalipiwa na Watanzania wote.

Bado tunalipia huduma kama Uzoaji taka mtaani.

Bado tunalipia huduma ya maji

Mchango wa maendeleo ya elimu kata na michango mingine midogo midogo mingi.

Ukiagiza bidhaa tunalipia Import duty

Ukiagiza gari tunalipia Railway Levy, Customs duty na Kodi ya uchakavu.

Ukitaka huduma ya kifedha kwa mitandao ya simu Kuna Tozo, Vat na makato ya huduma.

Ukienda benki Kuna Vat, Tozo na makato ya huduma.

Tozo za huduma ya Zimamoto kwenye kila jengo.

Income Tax/Paye kwa walioajiriwa
Tax on Capital gain
Rental tax ni asilimia 10%

Hivyo kiuhalisia sisi tunalipia Kodi kubwa zaidi ya asilimia 45% ya makusanyo yetu, halafu unatuambia!!!????

Sasa tuje kwenye uhalisia wa maisha yetu,
Nje ya Kodi zote hizo, mkuu huku hatupati huduma zinazostahili.

Barabara zetu hazina Lami katika mitaa

Bima za afya ni shida

Hatuna huduma ya Gari za dharura(Ambulance) kila mtaa
Hatuna hata ulinzi wa uhakika huku mitaani.

Mishahara duni na midogo kuweza kuhimili inflation.

Hatuna taa za barabarani.

Hatuna mifumo ya Serikari kuwa na program ya Kutoa chakula Cha bure kwa wasionacho huko kwenu mnaita food token.

Hatuna huduma ya kutunza Wazee kwa viwango vya uhakika na Bora kutoka serikarini.

Huduma mbovu za afya

Elimu ya hovyo kutoka government schools namaanisha isiyokidhi viwango.

Mifumo mibovu ya usambaji maji na uondoshaji wa majitaka.

Ubadhirifu, Ufisadi na wizi

Halafu ufananishe Amerika na Ulaya na huku kwetu Uswahilini kuwa na heshima hata kidogo, au ni mmoja ya walamba asali
 
Kwanza tuweke mambo sawa tozo ni aina ya kodi. Hivyo tusiongelee tozo kama vile sio kodi.

Mimi binafsi sijaona ubaya wowote wa serikali kuweka tozo na nina fikiri hakuna njia nyingine kwa wakati huu zaidi ya tozo na nitajaribu kuweka hoja hapa vizuri. Tanzania kama nchi inayoendelea inahitaji pesa ili iweze kuwekeza kwenye miradi mingi sana kuanzia elimu, maji, barabara, umeme, kilimo, ulinzi.......n.k

Sasa vyanzo vya mapato ni hivi
  1. Missada kutoka nje
  2. kodi na tozo
  3. mikopo
Tanzania tumeshakopa na bado tutaendelea kukopa kama tutapata mikopo nafuu lakini vilevile tunakusanya kodi mbalimbali. Lakini ukiangalia vizuri budget zetu pesa ya kodi ambayo haitoshi hata kwenye budget bado inaenda kwenye shughuli ambazo sizo za kimaendeleo hivyo sio uwekezaji wa nchi bali ni matumizi. Kuna miradi tunalipia kwenye kodi kama ya maji na umeme lakini wakati wa Kikwete pesa karibu yote ilikuwa ni kulipa mishahara na matumizi ya serikali.

Sasa kama nchi tuko kwenye kipindi cha uwekezaji kwa mara ya kwanza tunaanza kuona barabara za kisasa, shule bora, hospitali na umeme hasa vijijini. Sasa tumefikaje hapa ? Ni kuwekeza kwa kodi mpya na tozo. Umeme mfano wa vijijini umepelekwa na tozo maalamu kwenye luku za nyumbani na barabara za vijijini nyingi zinatengenezwa na tozo kwenye mafuta. Lakini ili kama nchi tuweze kuwekeza na kuongeza walipa kodi ni lazima tuwekeze kwenye kilimo. Kilimo kitaongeza mapato kwenye kodi lakini tatizo hatuna mfumo mzuri wa kilimo kuwa na uazalishaji wa uhakika. Bashe amekuja na mpango mzuri wa kuongeza uzalishaji kwa kufanya yafuatayo (1) Serikali itatoa ruzuku kwenye mbolea (2) Serikali itawekeza kwenye umwagiliaji (3) watatoa mbegu (4) watafuta wawekezaji wa viwanda (5) kutafuta masoko. Hii ndiyo mojawapo kubwa ya kuongeza ajira na kodi lakini mtaji wa yote haya ni karibu Trillion moja sasa mtaji unatoka wapi? Hii ndiyo sababu imeenda kwenye tozo hivyo tozo ni muhimu kwasababu ni mtaji wa uhakika wa kuongeza kodi kwa miaka ijayo. Lakini ni tukiangalia vizuri tatizo letu ni utamaduni mbovu watu wengi walizoea kukaa bila kulipa kodi wala tozo

Mimi ni diaspora wa muda mrefu sana na naishi na kutafuta maslahi yangu jimbo la Texas. Hili jimbo letu linajulikana kwa kuwa na kodi ndogo lakini ngoja niwape data kidogo ili mgundue tonavyolipa kodi.

  • Nyumba kila mwaka nalipa 3% ya thamani ya nyumba. Hivyo kwa mfano kama nyumba pale Tanzania yenye thamani ya Tsh 100,000,000 basi unatakiwa kulipa kila mwaka Tsh 3,000,000. Hakuna mjadala kwenye hili na usikolipa unapekwa mahakamani na nyumba inapigwa mnada
  • Jumuia na majiradi vilevile wana kitu kinaitwa HOA-Housing Owners Association hii ni jumuia ya makazi yako na majirani kila nyumba inalipa $350-$1000 kwa mwaka kwa usafi wa jumla kama kukata majani na kusafisha mitaro. Hii ni nje ya nyumba yako hii nayo ni lazima na kisheria wanaweza kwenda na utaratibu mpaka wakapiga mnada nyumba
  • Tuna tozo za maji na kuchukuwa taka. Kila wiki wanapita kuchukuwa taka kwenye magaloni maalumu. Hii inafanywa na manispaa huwezi kuchoma matakataka ovyo ovyo. Maji unalipa kutokana ma matumizi lakini taka utalipia unataka au hautaki jumla sio chini ya $100 kila mwezi. Ukitupa uchafu ovyo ni faini, usipoweka uchafu vizuri kwenye mifuko ni faini....
  • Barabara nyingi zinajegwa kwa mikopo inayoitwa goverment bonds hivyo ni lazima ilipwe. Kila nikienda kazini kwa mfano ni lazima nipitie kwenye barabara za kupipia "toll roads" na natumia sio chini ya $5-$7 kwenda kwa siku moja na kurudi. Tena hii ni rahisi New York wanatumia $12-$15.
  • Ukienda kwenye hotel na kokodi chumba karibu 35% ni kodi na tozo, kwenye simu, cable za TV au Dish hivyohivyo
  • Kwenye super market kila ukinunua kitu kuna 5% ya tozo inaenda kusaidi "Metro" ambayo ni kama mwendo kasi yetu.
  • Lakini hapa kuna bima ya karibu kila kitu nyumba ni lazima uwe na bima na kwenye hizi bima kuna pesa zinaenda kusaidia idara kama Zimamotto... na ambulance
Hapa sijaongelea tozo na kodi za mishahara. Lakini mjue hapa bado tuna nafuu sana kulinganisha na nchi za Ulaya au Canada ambako Tozo na kodi zipo juu sana. Familia yangu ina bahati tuna nyumba Uninio sehemu ambayo ina thamani sana lakini kodi zetu pale hazifiki hata 1% ya thamani wakati bodaboda wanalipa kodi kwenye mafuta. Hivyo kuna sehemu kiukweli wanaonufaika ni matajiri tu kusema ukweli.

Kuna ambao watasema huko Ulaya na US pesa inaonekana ni kweli tuna shule kwenye kila mtaa za watoto zina mabasi na ni bure lakini tunalipa 3% kwenye thamani ya nyumba na pesa inaenda huko. Hivyo hoja ni yaanze mayai au kuku lakini kodi ni muhimu na maendeleo ni muhimu. Ndiyo maana hoja yangu ni kwamba tozo ni muhimu kwasababu ni mtaji na utaratibu mpya wa kuongeza wigo la walipa kodi na kuweka mifumo ya kimaendeleo. Tatizo kubwa ni mazoea ya watu wengi walikuwa wamezoea kukaa bila shughuli na kubangaiza lakini kama tunataka umeme vijijini, barabara za lami na hospitali ni lazima zitengenezwe, kuwe na pesa za matengenezo kila mara na pesa za wahudumu. Ni lazima kuwe na mfumo wa mapato na wananchi ni lazima wazalishe ili waweze kuwa na mifumo hii. Huwezi kukaa kijijini hulipi kodi yeyote, huzalishi chochote halafu unahitaji barabara, maji, umeme ... pesa inatoka wapi? Ni lazima serikali iwekeze kwenye kilimo ili wewe mwanakijiji uweze kuchangia kodi na maendeleo na ndicho kinacho fanyika kwa sasa
We mbeba box watanzania wanacholalamikia Ni double taxation, serikali inachofanya Ni kutoza Kodi mara mbili, umeandika upuuzi mwingi lakini ndani Ni pumba,
 
Kwanza tuweke mambo sawa tozo ni aina ya kodi. Hivyo tusiongelee tozo kama vile sio kodi.

Mimi binafsi sijaona ubaya wowote wa serikali kuweka tozo na nina fikiri hakuna njia nyingine kwa wakati huu zaidi ya tozo na nitajaribu kuweka hoja hapa vizuri. Tanzania kama nchi inayoendelea inahitaji pesa ili iweze kuwekeza kwenye miradi mingi sana kuanzia elimu, maji, barabara, umeme, kilimo, ulinzi.......n.k

Sasa vyanzo vya mapato ni hivi
  1. Missada kutoka nje
  2. kodi na tozo
  3. mikopo
Tanzania tumeshakopa na bado tutaendelea kukopa kama tutapata mikopo nafuu lakini vilevile tunakusanya kodi mbalimbali. Lakini ukiangalia vizuri budget zetu pesa ya kodi ambayo haitoshi hata kwenye budget bado inaenda kwenye shughuli ambazo sizo za kimaendeleo hivyo sio uwekezaji wa nchi bali ni matumizi. Kuna miradi tunalipia kwenye kodi kama ya maji na umeme lakini wakati wa Kikwete pesa karibu yote ilikuwa ni kulipa mishahara na matumizi ya serikali.

Sasa kama nchi tuko kwenye kipindi cha uwekezaji kwa mara ya kwanza tunaanza kuona barabara za kisasa, shule bora, hospitali na umeme hasa vijijini. Sasa tumefikaje hapa ? Ni kuwekeza kwa kodi mpya na tozo. Umeme mfano wa vijijini umepelekwa na tozo maalamu kwenye luku za nyumbani na barabara za vijijini nyingi zinatengenezwa na tozo kwenye mafuta. Lakini ili kama nchi tuweze kuwekeza na kuongeza walipa kodi ni lazima tuwekeze kwenye kilimo. Kilimo kitaongeza mapato kwenye kodi lakini tatizo hatuna mfumo mzuri wa kilimo kuwa na uazalishaji wa uhakika. Bashe amekuja na mpango mzuri wa kuongeza uzalishaji kwa kufanya yafuatayo (1) Serikali itatoa ruzuku kwenye mbolea (2) Serikali itawekeza kwenye umwagiliaji (3) watatoa mbegu (4) watafuta wawekezaji wa viwanda (5) kutafuta masoko. Hii ndiyo mojawapo kubwa ya kuongeza ajira na kodi lakini mtaji wa yote haya ni karibu Trillion moja sasa mtaji unatoka wapi? Hii ndiyo sababu imeenda kwenye tozo hivyo tozo ni muhimu kwasababu ni mtaji wa uhakika wa kuongeza kodi kwa miaka ijayo. Lakini ni tukiangalia vizuri tatizo letu ni utamaduni mbovu watu wengi walizoea kukaa bila kulipa kodi wala tozo

Mimi ni diaspora wa muda mrefu sana na naishi na kutafuta maslahi yangu jimbo la Texas. Hili jimbo letu linajulikana kwa kuwa na kodi ndogo lakini ngoja niwape data kidogo ili mgundue tonavyolipa kodi.

  • Nyumba kila mwaka nalipa 3% ya thamani ya nyumba. Hivyo kwa mfano kama nyumba pale Tanzania yenye thamani ya Tsh 100,000,000 basi unatakiwa kulipa kila mwaka Tsh 3,000,000. Hakuna mjadala kwenye hili na usikolipa unapekwa mahakamani na nyumba inapigwa mnada
  • Jumuia na majiradi vilevile wana kitu kinaitwa HOA-Housing Owners Association hii ni jumuia ya makazi yako na majirani kila nyumba inalipa $350-$1000 kwa mwaka kwa usafi wa jumla kama kukata majani na kusafisha mitaro. Hii ni nje ya nyumba yako hii nayo ni lazima na kisheria wanaweza kwenda na utaratibu mpaka wakapiga mnada nyumba
  • Tuna tozo za maji na kuchukuwa taka. Kila wiki wanapita kuchukuwa taka kwenye magaloni maalumu. Hii inafanywa na manispaa huwezi kuchoma matakataka ovyo ovyo. Maji unalipa kutokana ma matumizi lakini taka utalipia unataka au hautaki jumla sio chini ya $100 kila mwezi. Ukitupa uchafu ovyo ni faini, usipoweka uchafu vizuri kwenye mifuko ni faini....
  • Barabara nyingi zinajegwa kwa mikopo inayoitwa goverment bonds hivyo ni lazima ilipwe. Kila nikienda kazini kwa mfano ni lazima nipitie kwenye barabara za kupipia "toll roads" na natumia sio chini ya $5-$7 kwenda kwa siku moja na kurudi. Tena hii ni rahisi New York wanatumia $12-$15.
  • Ukienda kwenye hotel na kokodi chumba karibu 35% ni kodi na tozo, kwenye simu, cable za TV au Dish hivyohivyo
  • Kwenye super market kila ukinunua kitu kuna 5% ya tozo inaenda kusaidi "Metro" ambayo ni kama mwendo kasi yetu.
  • Lakini hapa kuna bima ya karibu kila kitu nyumba ni lazima uwe na bima na kwenye hizi bima kuna pesa zinaenda kusaidia idara kama Zimamotto... na ambulance
Hapa sijaongelea tozo na kodi za mishahara. Lakini mjue hapa bado tuna nafuu sana kulinganisha na nchi za Ulaya au Canada ambako Tozo na kodi zipo juu sana. Familia yangu ina bahati tuna nyumba Uninio sehemu ambayo ina thamani sana lakini kodi zetu pale hazifiki hata 1% ya thamani wakati bodaboda wanalipa kodi kwenye mafuta. Hivyo kuna sehemu kiukweli wanaonufaika ni matajiri tu kusema ukweli.

Kuna ambao watasema huko Ulaya na US pesa inaonekana ni kweli tuna shule kwenye kila mtaa za watoto zina mabasi na ni bure lakini tunalipa 3% kwenye thamani ya nyumba na pesa inaenda huko. Hivyo hoja ni yaanze mayai au kuku lakini kodi ni muhimu na maendeleo ni muhimu. Ndiyo maana hoja yangu ni kwamba tozo ni muhimu kwasababu ni mtaji na utaratibu mpya wa kuongeza wigo la walipa kodi na kuweka mifumo ya kimaendeleo. Tatizo kubwa ni mazoea ya watu wengi walikuwa wamezoea kukaa bila shughuli na kubangaiza lakini kama tunataka umeme vijijini, barabara za lami na hospitali ni lazima zitengenezwe, kuwe na pesa za matengenezo kila mara na pesa za wahudumu. Ni lazima kuwe na mfumo wa mapato na wananchi ni lazima wazalishe ili waweze kuwa na mifumo hii. Huwezi kukaa kijijini hulipi kodi yeyote, huzalishi chochote halafu unahitaji barabara, maji, umeme ... pesa inatoka wapi? Ni lazima serikali iwekeze kwenye kilimo ili wewe mwanakijiji uweze kuchangia kodi na maendeleo na ndicho kinacho fanyika kwa sasa
Naimba kujua au kupata elimu kidogo hapa...Msaada kutoka nje na mkopo unatofauti gani..? Isn't the source the same "person"...?
 
Ngoja nianze na mifano yako nikilinganisha hapa Nyumbani Tanzania.

Tuna Kodi ya Ardhi ambayo tunalipia kwa mwaka.
Kodi ya jengo ambayo imeingizwa kwenye mfumo wa Umeme.

Hizi Kodi mbili zinakata chanzo kimoja na mtu yule yule na eneo Lile Lile mathalani ni nyumba kwa ajili ya makazi.

Value added Tax hakuna huduma utakayo pata Tanzania ikiwemo kununua bidhaa usikatwe asilimia 18% au 15% ya huduma, hapa inategemea hiyo Vat ni inclusive au exclusive

Ukiwa unafanya biashara na taasisi za serikari, Kuna 2% withholding Tax( Kodi ya zuio) na Ile VAT ipo pale pale.

Kuna Kodi nadhani ilikuwa ya wanaotumia vyombo vya moto kuhusu Matumizi ya Barabara ikaondolewa na kujumuishwa kwenye kila Lita ya mafuta, Sasa hii inalipiwa na Watanzania wote.

Bado tunalipia huduma kama Uzoaji taka mtaani.

Bado tunalipia huduma ya maji

Mchango wa maendeleo ya elimu kata na michango mingine midogo midogo mingi.

Ukiagiza bidhaa tunalipia Import duty

Ukiagiza gari tunalipia Railway Levy, Customs duty na Kodi ya uchakavu.

Ukitaka huduma ya kifedha kwa mitandao ya simu Kuna Tozo, Vat na makato ya huduma.

Ukienda benki Kuna Vat, Tozo na makato ya huduma.

Tozo za huduma ya Zimamoto kwenye kila jengo.

Income Tax/Paye kwa walioajiriwa
Tax on Capital gain
Rental tax ni asilimia 10%

Hivyo kiuhalisia sisi tunalipia Kodi kubwa zaidi ya asilimia 45% ya makusanyo yetu, halafu unatuambia!!!????

Sasa tuje kwenye uhalisia wa maisha yetu,
Nje ya Kodi zote hizo, mkuu huku hatupati huduma zinazostahili.

Barabara zetu hazina Lami katika mitaa

Bima za afya ni shida

Hatuna huduma ya Gari za dharura(Ambulance) kila mtaa
Hatuna hata ulinzi wa uhakika huku mitaani.

Mishahara duni na midogo kuweza kuhimili inflation.

Hatuna taa za barabarani.

Hatuna mifumo ya Serikari kuwa na program ya Kutoa chakula Cha bure kwa wasionacho huko kwenu mnaita food token.

Hatuna huduma ya kutunza Wazee kwa viwango vya uhakika na Bora kutoka serikarini.

Huduma mbovu za afya

Elimu ya hovyo kutoka government schools namaanisha isiyokidhi viwango.

Mifumo mibovu ya usambaji maji na uondoshaji wa majitaka.

Ubadhirifu, Ufisadi na wizi

Halafu ufananishe Amerika na Ulaya na huku kwetu Uswahilini kuwa na heshima hata kidogo, au ni mmoja ya walamba asali

Kama unakunywa Bia,

Kunywa 5 Kwa bill yangu, kwa hizo fact ambazo umempa I'm very sure hatorudi tena
 
Kwanini fedha yangu uikate kodi mara mbili.Makodi tunalipa lukuki, tumeshawahi kulalamika kwani japo tunajua zunatumika ndivyo sivyo.Kwanini uikate tozo fedha yangu ambayo haujaiongezea thamani yoyote.
 
Ngoja nianze na mifano yako nikilinganisha hapa Nyumbani Tanzania.

Tuna Kodi ya Ardhi ambayo tunalipia kwa mwaka.
Kodi ya jengo ambayo imeingizwa kwenye mfumo wa Umeme.

Hizi Kodi mbili zinakata chanzo kimoja na mtu yule yule na eneo Lile Lile mathalani ni nyumba kwa ajili ya makazi.

Value added Tax hakuna huduma utakayo pata Tanzania ikiwemo kununua bidhaa usikatwe asilimia 18% au 15% ya huduma, hapa inategemea hiyo Vat ni inclusive au exclusive

Ukiwa unafanya biashara na taasisi za serikari, Kuna 2% withholding Tax( Kodi ya zuio) na Ile VAT ipo pale pale.

Kuna Kodi nadhani ilikuwa ya wanaotumia vyombo vya moto kuhusu Matumizi ya Barabara ikaondolewa na kujumuishwa kwenye kila Lita ya mafuta, Sasa hii inalipiwa na Watanzania wote.

Bado tunalipia huduma kama Uzoaji taka mtaani.

Bado tunalipia huduma ya maji

Mchango wa maendeleo ya elimu kata na michango mingine midogo midogo mingi.

Ukiagiza bidhaa tunalipia Import duty

Ukiagiza gari tunalipia Railway Levy, Customs duty na Kodi ya uchakavu.

Ukitaka huduma ya kifedha kwa mitandao ya simu Kuna Tozo, Vat na makato ya huduma.

Ukienda benki Kuna Vat, Tozo na makato ya huduma.

Tozo za huduma ya Zimamoto kwenye kila jengo.

Income Tax/Paye kwa walioajiriwa
Tax on Capital gain
Rental tax ni asilimia 10%

Hivyo kiuhalisia sisi tunalipia Kodi kubwa zaidi ya asilimia 45% ya makusanyo yetu, halafu unatuambia!!!????

Sasa tuje kwenye uhalisia wa maisha yetu,
Nje ya Kodi zote hizo, mkuu huku hatupati huduma zinazostahili.

Barabara zetu hazina Lami katika mitaa

Bima za afya ni shida

Hatuna huduma ya Gari za dharura(Ambulance) kila mtaa
Hatuna hata ulinzi wa uhakika huku mitaani.

Mishahara duni na midogo kuweza kuhimili inflation.

Hatuna taa za barabarani.

Hatuna mifumo ya Serikari kuwa na program ya Kutoa chakula Cha bure kwa wasionacho huko kwenu mnaita food token.

Hatuna huduma ya kutunza Wazee kwa viwango vya uhakika na Bora kutoka serikarini.

Huduma mbovu za afya

Elimu ya hovyo kutoka government schools namaanisha isiyokidhi viwango.

Mifumo mibovu ya usambaji maji na uondoshaji wa majitaka.

Ubadhirifu, Ufisadi na wizi

Halafu ufananishe Amerika na Ulaya na huku kwetu Uswahilini kuwa na heshima hata kidogo, au ni mmoja ya walamba asali
Liked
 
Back
Top Bottom