Halima umeonesha mwanzo mzuri, maridhiano

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,827
35,832
Mabibi na mabwana kama nchi tumepwelewa sana katika hili la maridhiano. Kwa hakika matatizo yetu kama nchi yako hapo na ndiyo maana tuko hapa tulipo na sasa kama mazuzu tu.

Mbowe ameonyesha kwa vitendo kuwa kinachohitajika katika migogoro ukiwamo huu ni maridhiano. Jibu la Bi. Halima kwenye hili kuwa wapo tayari "kuyajenga" mbona ni la kupongezwa mno?

Ikumbukwe pana wenye kupenda kuukaanga mbuyu vilivyo ili kuwaachia wenye meno kutafuna.

Hebu wasipewe nafasi hao. Wakaanga mbuyu na wakajifunze kwa vitendo.

Kwa maneno ya bi Tshala Mwana, "bibi na bwana wakigombana nyumbani waache wataelewana wenyewe. Ukiyaingilia utabaki na aibu"

Muda wa kuwafahamisha wasiohusika bila ya kujali vyeo vyao au vyama vyao - kuufyata! Ipewe sasa nafasi ya hoja kutamalaki katika mazingira yenye kufaa. Kusamehe 7x70 ni sehemu ya maisha ya binadamu wenye utu. Wanasema waungwana, "we can live and let live!"

Nini taabu kama maridhiano yakatufikisha kwenye:

1. Kuwajua waasisi wa ghushi?
2. Kuwashugulikia waasisi wa ghushi?
3. Kuwaumbua waasisi wa ghushi?
4. Kuwapa funzo la kudumu waasisi wa ghushi?
5. Kuufunga mjadala wa ghushi hii katika namna inayokubalika?

Kamanda Mbowe na makamanda wote kwa kauli ya bi dada leo, kukaa nao rasmi au hata kivinginevyo lengo kuyajenga itakuwa ni sahihi sana. Ikumbukwe kuwa kuhitajika kuyajenga kwanza kabla ya mengine limo kwenye sehemu ya hukumu.

Walionyeshwa mlango wa kutokea ila haukupigwa kufuli. Bi Halima hakukunja ngumi. Kwa hekima amenyoosha mkono. Ni busara kuupokea.

Kwa maneno ya Jabali la Muziki: "Tukamsake mbaya wetu anaye tuchonganisha." Siku tukimpata zikawe zetu ama zake!

Mungu ibariki CHADEMA.
 
Amecheza karata vizuri, ila angeleta ujeuri wa kutishia kuhama chama basi ndio ulikua mwisho wake kisiasa.

Ange danganyika kwenda CCM kisa Dk. Bashiru amemkaribisha au kinga walioahidiwa na Speaker pamoja na A.G, angekutana na fitna nyingi sana za wana CCM kindaki ndaki.

ILA BADO ninaamini serikali ndio imemshinikiza aongee hayo kwenye hii press ya leo. Baada ya kuona dunia na taifa zima limepokea "NEGATIVELY" kulazimishwa kwa Covid-19 kuapishwa bila ridhaa ya chama chao na Mwanasheria Mkuu Wa Serikali na Speaker kujigamba kuwatetea kwa nguvu zote.

Pia Covid-19 walishagawanyika, kuna waliotaka kurudi na kuomba msamaha, na kuna waliotaka waendelee na ukauzu wao.

CHADEMA NINGEPENDA KUONA wanatumia karata zao vizuri kukubali maridhiano ya kina Halima Mdee & Co LTD. Kwa kuwapa mashart umiza;

1) Ili kupokea baraka na msamaha wa chama, basi Covid-19 wafanye press kutoa muongozo wa nani alieshinikiza wao kuapishwa. Na vikao vilifanyika vipi na wapi.

2) Covid-19 waandike barua za kujivua ubunge wa kuteuliwa kwa NEC na SPEAKER (Japo kisheria baada ya kufukuzwa uwanachama wameshaondolewa).

3) Katika press hio Covid-19 watoe tamko la kuungana na wanachama wenzao sambamba na vyama vingine vya upinzani kutotambua uchaguzi mkuu 2020 pamoja na bunge hili.

4) Pia katika press hio "WAOMBE MSAMAHA CHAMA NA WANACHAMA" kwa kukubali kufanya hayo waliofanya ya kuapishwa bila ridhaa ya chama. Na wakiri walikosea sana.
 
Hivi mbona Halima, kiongozi Wa covid -19, hajaongelea kua walipata baraka wapi za kwenda kuapa Kama wabunge Wa viti maalumu,

Na nani aliyemtoa Nusrat Hanje Nje ya utaratibu Wa mahakama na kwenda kuapa.

Hapo ndio tatizo linaponzia
 
swali la kipuuzi kama upuuzi mwingine. kurudia kufanya haramu hakuwezi kugeuza hiyo haramu kuwa safi
Hiyo miaka ya 2010 walienda kwa sababu mbowe alishinda uchaguzi

Na 2020 hawaendi kwa sababu Mbowe ameshindwa uchaguzi
 
Ivi mbona halima , kiongozi Wa covid -19 , hajaongelea kua walipata baraka wapi za kwenda kuapa Kama wabunge Wa viti maalumu,

Hapo ndio tatizo linaponzia
Hilo alilijibu technically sana ili kuepuka kuchafua hali ya hewa. Personally, I am speculating kuwa, mwamba anaweza kuwa anahusika katika hili. Halma hawezi just kuchukua decision ya hivo bila kuwa na backup ndani ya senior leaders. Hata kama mwamba alikana kushiriki kwake, ila kuna hiyo possibilities.
 
Hahahaha, hii inaitwa bytime ili kesi ikifika mahakamani waendelee kuwq wabunge wa mahakama for 5 good years. So chadema komaeni hawa wanauma na kupuliza.
 
Ivi mbona halima , kiongozi Wa covid -19 , hajaongelea kua walipata baraka wapi za kwenda kuapa Kama wabunge Wa viti maalumu,

Hapo ndio tatizo linaponzia

Wakuu kwenye kuyajenga yataongelewa hayo.

Halima kaongea kwa hekima na kama mke mwema.

"Halima umeanza vyema, mgogoro huu na ukaishe vyema."

CHADEMA ni chama cha mioyoni. Makamanda hawatakutosa kwa kosa moja ukiwa tayari kuyajenga.
 
Hilo alilijibu technically sana ili kuepuka kuchafua hali ya hewa. Personally, I am speculating kuwa, mwamba anaweza kuwa anahusika katika hili. Halma hawezi just kuchukua decision ya hivo bila kuwa na backup ndani ya senior leaders. Hata kama mwamba alikana kushiriki kwake, ila kuna hiyo possibilities.
Kwa hiyo mwamba ndio alikua na uwezo Wa kumtoa Nusrat Hanje Nje ya utaratibu Wa mahakama na kwenda kuapa?
 
Hivi hawa 19 watakuwa tayari kama sharti kuu la kuyajenga ni Halima na wenzie kuachia Ubunge kwanza na kurudi chamani kama wanachama wa kawaida bila nafasi yoyote ya uongozi harafu CHADEMA kipeleke akina mama wengine 19 bungeni?

Come to think of it, most likely dhahama hii ilianza chini kwa chini pale lilipokuja suala la nani na nani wateuliwe kwenda Bungeni
 
Back
Top Bottom